BungelaKatiba2014tz
JF-Expert Member
- Feb 18, 2014
- 1,231
- 649
Akizungumza kwenye mdahalo uliondaliwa na kurushwa na AZAM TV jana, Mgombea Ubunge jimbo la Ubungo, , Dr. Didas Masaburi(CCM), alisema anayepaswa kulaumiwa kwa uuzwaji holela wa Shirika la Usafiri Dar es Salaam(UDA) ni LOWASSA, aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo, kwani ndiye aliyekuwa msimamizi wa mchakato huo mwaka 2006 hadi 2008.
"Kwa mujibu wa sheria , Waziri Mkuu ndiye msimamizi wa Serikali za Mitaa", alisema Dr. Didas Masaburi katika mdahalo uliohudhuriwa pia na wgombea wengine, Said Kubenea wa Chadema, Zangina Shangana(ACT-Wazalendo) na Renatus Muhabi(CCK).
Awali ilidhaniwa kuwa hoja ya uuzwaji wa UDA ungempa wakati mgumu Dr. Masaburi, lakini hali haikuwa hivyo kwani alitumia nafasi hiyo kutoa ufafanuzi ulioeleweka na kumtupia lawama Lowassa. Mbali na Richmond, Lowassa pia anatuhumiwa kuwa na hisa katika kampuni ya Integrated Property Limited inayohusishwa na ujenzi ambayo haikuiorodhesha kwenye Tume ya Maadili kwa mujibu wa sheria kama mtumishi wa Umma.
Mimi sijahusika na ufisadi katika uuzwaji wa UDA, nilichokifanya ni kupandisha bei yake kutoka bil.1 hadi sh.bil. 5.7nilipoingia kwenye UMEYA na kukuta shirika hilo limeuzwa isivyo halali.
Meya 2011niligundua mkataba usio sawa wa uuzwaji wa UDA baada ya kuajiri kampuni ya Ukaguzi wa hesabu ya KPMG, Bei yake haikulingana na thamani ya mali za shirika hilo, hivyo niliamuru mnunuzi, Simon group kuongeza fedha.
Soma zaidi RAIA TANZANIA.
"Kwa mujibu wa sheria , Waziri Mkuu ndiye msimamizi wa Serikali za Mitaa", alisema Dr. Didas Masaburi katika mdahalo uliohudhuriwa pia na wgombea wengine, Said Kubenea wa Chadema, Zangina Shangana(ACT-Wazalendo) na Renatus Muhabi(CCK).
Awali ilidhaniwa kuwa hoja ya uuzwaji wa UDA ungempa wakati mgumu Dr. Masaburi, lakini hali haikuwa hivyo kwani alitumia nafasi hiyo kutoa ufafanuzi ulioeleweka na kumtupia lawama Lowassa. Mbali na Richmond, Lowassa pia anatuhumiwa kuwa na hisa katika kampuni ya Integrated Property Limited inayohusishwa na ujenzi ambayo haikuiorodhesha kwenye Tume ya Maadili kwa mujibu wa sheria kama mtumishi wa Umma.
Mimi sijahusika na ufisadi katika uuzwaji wa UDA, nilichokifanya ni kupandisha bei yake kutoka bil.1 hadi sh.bil. 5.7nilipoingia kwenye UMEYA na kukuta shirika hilo limeuzwa isivyo halali.
Meya 2011niligundua mkataba usio sawa wa uuzwaji wa UDA baada ya kuajiri kampuni ya Ukaguzi wa hesabu ya KPMG, Bei yake haikulingana na thamani ya mali za shirika hilo, hivyo niliamuru mnunuzi, Simon group kuongeza fedha.
Soma zaidi RAIA TANZANIA.