Lowassa kapita dirishani kwangu

Lowassa kapita dirishani kwangu

Kapita.kimya kimya ila hilo nyomi.sasa ni.noma sana

Yaani leo nalala raha sana
 
CCM inadhani kuwa Watanzania tutaendelea kuwa vipofu daima.

Nasikitika kwani hata sasa tumevunja rekodi ya upofu, ilitupasa tuone miaka mingi iliyopita sijui watanzania tunawaza vipi. Nadhani ndiyo maana tunaitwa wapumbavu na malofa na waliotufanya kuwa malofa.
 
Sema kipenzi cha wapumbavu na malofa

Vibaka ,wapumbavu na wajinga tuna imani na raisi wetu mtarajiwa Edward Lowasa.nyie maccm mpigieni debe huyo Magufuli wenu
POMBE MWISHO KAUNTA MTAANI NA IKULU LOWASA ANATOSHA.
 
Mkuu GAZETI umeongea ukweli big up mkuu yayo ndo maono watanzania wote watafakari miaka 50 wameshindwa sasa wataweza miaka 5 sio rahisi

mkuu ngajone, hawa watu wamesha shindwa ndio maana wamebaki kutukana wapiga kura,
 
Lowasa njoo na mtaani kwetu pliz, this is not fair kabisa maana hata cc wa mbagala tunakupenda
 
Mkapa ndo anafiri kuwa kura zinapatikana KWA matusi kejeli na vitisho!! Hakuna nchi isiyotambua mchango WA ccm ya mwlimu ktk ukombozi WA afrika na uonevu WA ccm baada ya mwalimu, KWA kura zetu tutamwonesha ulofa wetu, lnshaallah mwenyeenzi Mungu atakuwa upande WA "malofa"

big up mkuu watajuta kuwajua malofa na wapumbavu,
 
Lowasa anadhani kuwa Watanzania wanadanganyika kirahisi

Umesahau kinana amevaa malapa, anasafiri kwa reli kwenda Kigoma, anajenga nyumba, analima shambani, anavuna mahindi, anakula wali maharage, anakula vitumbua??

Au ni kuona mambo ya upande mmoja tu? Wadanganyika unawajua sana. Vilemba, chumvi, pilau, tamasha la muziki, khanga na baada ya hapo unapata kura na wanabaki wanasubiri miaka mitano tena!!
 
Watu wa Gongolamboto tumefarijika Sana kuona Rais mtarajiwa akipita mtaani kwetu kwenye kila aina ya uchafu akitaka kujua matatizo yetu ya kimaisha yaliyosababishwa na CCM ili ayatatue atakapochaguliwa kuwa rais.Kwa bahati nzuri kapita dirishani kwangu ilinilazimu nitoke nje kwani nilikuwa na watu wengi wakiimba LOWASSA!LOWASSA!LOWASSA HAKUNA KAMA WEWE.Lazima nimpatie kura yangu rais huyu

Alipokuwa madarakani mbona hakupita huko?

Hakika wapumbavu na malofa ni wengi sana.
 
Magufuli kila anapopita hawezi kuzomewa. Hata huyo fisadi wako kapita kwenye barabara zilizojengwa na Magufuli

kweli nyie ccm nimeshanganyikiwa barabara zimejengwa na Magufuli kwa pesa za Magufuli?
 
Heeee!!!!
Mimi nilitegemea anayajua matatizo ya Watanzania ndio maana alichukua fomu ya kugombea urais. Kumbe sasa ndio anaanza kuyatafuta, poor him.

Mzee wa kazi Mhe. Magufuli alianzisha na kuyafahamu matatizo ya watanzania. Aidha familia Yake inaishi katikati ya hao watanzania wenye shida. Watoto wake wanasoma shule za Serikali, wanapanda daladala, wanatibiwa kwenye dispensary na wanavaa Nguo za bongo.

Yeye familia Yake wanaendesha magari ya ki kifahari tena wote, wanatibiwa Ujerumani, wanasoma ughaibuni, wanavaa Nguo za Ma designers nk

Yeye aendelee kutembelea watu siku za kampeni zinazidi kuyoyoma. Nasikia anatafuta nyomi ya kujaza uwanja Jumamosi.

Mzee wa kazi alikuwa Mpanda. Mwendo mdundo.

Queen Esther

Watu wa Gongolamboto tumefarijika Sana kuona Rais mtarajiwa akipita mtaani kwetu kwenye kila aina ya uchafu akitaka kujua matatizo yetu ya kimaisha yaliyosababishwa na CCM ili ayatatue atakapochaguliwa kuwa rais.Kwa bahati nzuri kapita dirishani kwangu ilinilazimu nitoke nje kwani nilikuwa na watu wengi wakiimba LOWASSA!LOWASSA!LOWASSA HAKUNA KAMA WEWE.Lazima nimpatie kura yangu rais huyu
 
Magufuli kila anapopita hawezi kuzomewa. Hata huyo fisadi wako kapita kwenye barabara zilizojengwa na Magufuli

Duuu!hizo barabara kumbe kajenga Magufuli!!basi ana fedha nyingi sana huyu mtu.
 
Jamani mwaka huu ndiyo nauona upinzani wa kweli, sasa kuna wengine matumbo joto safari hii hawalali duh, sisi tumeshachagua rais tunayemtaka tunasubiri tu kulikamilisha hili 25.Oktoba,
 
Alikuwa wapi siku zote?

alikuwa bado hajajiunga na watu wenye roho nzuri. kule alipotoka watu wana roho mbaya sana. angefanya kama alivyofanya leo angeitwa chamani na kupewa adhabu au kalipio. ccm wana roho mbaya sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom