Lowassa is back!

i1278_img0015.jpg





Kifimbo cha Nyerere umekiona hapo? Hahahaha
 
Lowassa kweli sasa kaamua kurudi ulingoni, ndio maana;
  1. Katuma mtu wake kujiingiza JF, hii ikiwa ni post yake ya kwanza ili kutuletea hizi picha za kampeni yake.
  2. Baada ya mafanikio ya harusi ya bintiye aliyoweza kuhakikisha analambwa miguu na vibosile wote wa CCM, sasa inaelekea anaelekeza nguvu zake jimboni.
  3. Swali kwetu ni kuwa, ni vipi mtumishi wa serikalini anaweza kujilimbikizia mali na kufanya sherehe na kampeni za kifahari bila TAKUKURU kumchunguza?
 
Lowasa is back from where!!! Ajaribu kwenda mikoa mingine ndiyo utuletee hii habari!!!
 
Lowassa kweli sasa kaamua kurudi ulingoni, ndio maana;
  1. Katuma mtu wake kujiingiza JF, hii ikiwa ni post yake ya kwanza ili kutuletea hizi picha za kampeni yake.
  2. Baada ya mafanikio ya harusi ya bintiye aliyoweza kuhakikisha analambwa miguu na vibosile wote wa CCM, sasa inaelekea anaelekeza nguvu zake jimboni.
  3. Swali kwetu ni kuwa, ni vipi mtumishi wa serikalini anaweza kujilimbikizia mali na kufanya sherehe na kampeni za kifahari bila TAKUKURU kumchunguza?
Mkuu!! naomba nitofautiane nawe. Hivi ukisema takukuru unamaanisha nini? kama ni Taasisi ya kupambana na rushwa. You are very wrong!!
ile ni Registered trust ya kuwalinda wala rushwa. na ndiyo maana iko ndani ya ikulu-mahali usipoweza kuingia kirahisi.
 
lowasa is back?
where is he coming from?
as to my understanding lowasa was there, is there, and probably will be there,
huyu jamaa ni kama kingmaker,yaani kwa nguvu hata R A hatii mguu hapo
 


Hii picha nzuri sana anadumisha mila.Kuna jamaa hapo kavaa koti la suti la dark blue anasindikiza kibuyu na dole sijui anaashiria nini

Mkuu Mila ipi? Huyu jamaa si Mmasai ni Mmeru. Kavamia jimbo la kwa jeuri ya chapaa.
 
Lowassa ana haki ya kuhamasisha maendeleo katika jimbo lake kwa vile ni mbunge halali na hili haliashirii kurudi katika center stage ya siasa hapa nchini. I think we are reading too much into whatever EL is up to!
 


hivi kweli huyo jamaa analizika na maisha ya vijumba kama hivyo, hao jamaaa wako kwenye umaskini mkubwa, na siddhani kama hao jamaa wanajua kuwa huyo kiongozi wao ni billionea wa kutupwa na bado yuko kwenye mchakato wa kwenda kuchuma zaidi
 
Hakuna kiongozi ninayempenda,kuamini kama Lowasa,(sitoi sababu)

ni mchapa kazi kweli kweli

mawazo yangu tu
 
Watanzania tuna unyonge wa kupambana na viongozi wabovu. Mtu akishakuwa kiongozi basi tunamwona kama vile ni Mungu. Tusbiri tuje tuone picha za Chenge, na za Rostam Aziz huko kwao.

Hebu angalia wenzetu Marekani. Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, kuna Maseneta na Makongressmen karibu kumi waliofungwa kwa miaka 7 na zaidi kwa ajili ya ufisadi- tena mdogo sana kulingana na uchumi wa nchi yao. Hebu tuambizane kama kweli kuna mbunge au Waziri yeyote aliyewahi kufungwa kwa ufisadi wowote hapa kwetu- tena ufisadi mkubwa unaolingana na nusu ya bajeti ya wizara nzima.
 


hivi kweli huyo jamaa analizika na maisha ya vijumba kama hivyo, hao jamaaa wako kwenye umaskini mkubwa, na siddhani kama hao jamaa wanajua kuwa huyo kiongozi wao ni billionea wa kutupwa na bado yuko kwenye mchakato wa kwenda kuchuma zaidi

Mkuu nakusoma, hawa wananchi hawana future yoyote na hawaelewi chochote, wanachofurahia ni kuona magari aliyokuja nayo mbunge wao pale kijijini, ngombe na pilau la bure, duh kweli vivaa tanzaniaaa

Wangejua mbuge wao ni billionea tena kwa pesa zao wenyewe nafikiri wangemgeuka pale pale lakini lah wakishiba pilau na nyama basi watasimulia wiki nzima kushituka uchaguzi huoooo
 
Hakuna kiongozi ninayempenda,kuamini kama Lowasa,(sitoi sababu)

ni mchapa kazi kweli kweli

mawazo yangu tu

kuna maana nyingi za uchapa kazi, hata vibaka wakienda kuiba wanaaga makwao kwamba wanaenda kuchapa kazi, tufafanulie Mkuu uchapakazi wa kiongozi wako ni upi?
 
Kila la Kheri Lowasa, Tunakutakia Kila la kheri katika Urejeo wako
 
Watanzania tuna unyonge wa kupambana na viongozi wa abovu. Mtu akishakuwa kiongozi basi tunamwona kama vile ni Mungu. Tusbiri tuje tuone picha za Chenge, na za Rostam Aziz.

Hebu angalia wenzetu Marekani. Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, kuna Maseneta na Makongressmen karibu kumi waliofungwa kwa miaka 7 na zaidi kwa ajili ya ufisadi- tena mdogo sana kulingana na uchumi wa nchi yao. Hebu tuambizane kama kweli kuna mbunge au Waziri yeyote aliyewahi kufungwa kwa ufisadi wowote hapa kwetu- tena ufisadi mkubwa unaolingana na nusu ya bejeti ya wizara nzima.

Nani wa kumkamata RA, Chenge au Lowassa ndugu yangu? hayupo tanzania hii, cha msingi ni kuomba mungu tu atusaide sisi wanyonge katika nchi yetu ili wasiamue kuiuza nchi yetu tukakosa pa kwenda na watoto wetu tukabakia utumwani.

Take from me, hao ndiyo Vigogo wa CCM bwana, hawagusiki na hakuna yeyote tanzania hii anaweza kunyoosha kidogle mbele ya hawa makamanda.

Sitta akajaribu kidogo tu uliona kilichotaka kumpata ndani ya CCM, ohoo mi sisemi sana...
 
Mimi nashindwa kuwaelewa watu ambao wanataka waendelee tuu kuwa viongozi wa nchi hii. Hivi kwa nini wanakuwa wachoyo? Tanzania hii ni ya watu wote. Wapo wengine ambao nao wangeliweza kushika hatamu za uongozi na nchi ikaenda vizuri sana. Kwa nini tuendelee kung'ang'ania wale wale tu hata kama wameshadhihirisha jinsi walivyo makapi?!

Vijana mbona hatuchangamkii tenda ipasavyo?
 
njaa bwana, inakufanya uwe mtumwa kabisa...akirudi huyu, basi sitamlaumu, wakuwalaumu ni wananchi tu.
 
Back
Top Bottom