BansenBurner
JF-Expert Member
- Feb 16, 2015
- 6,809
- 5,779
Mkuu hawa jamaa nmewachoka wanasema huyu hafai huyu sio msafi halaf hawatak kusema yupi anafaa cjui wametumwa
Kweli kabisa basi wakija next time waje na mbadala wa lowassa labda nani anafaa"
Mkuu hawa jamaa nmewachoka wanasema huyu hafai huyu sio msafi halaf hawatak kusema yupi anafaa cjui wametumwa
Ikulu siyo pango la mafisadi.
VOTE FOR UKAWA.
Ukweli ikiwa Edo ataupata uraisi itakuwa ni janga la kitaifa . Kwa nini
(1) Lazima hao marafiki zake waliomchangia watataka kurudisha hela zao na yeye pia atataka kurudisha fedha zake alizotumia kwani kila mtu anajua jinsi alivyomwaga fedha kununua kuungwa mkono. Wote tunajua hakuna atakayetoa hela yake bure bila kujua atazirudisha vipi kwani kama ungekuwa ni msaada basi hata hao watoa msaada wangeweza kunipa mimi nipeleke kanisani na msikitini lakini hawakufanya hvyo kwani walikuwa wanajua wanachokitafuta kupitia kwa Edo. Uraisi wake utakuwa wa kununua na si vinginevyo. Angalia tangazo la kwenye gazeti la Mwananchi la tarehe ya leo 26/5 ni tangazo la bei mbaya. Kizuri kinajiuza kibaya kinajitangaza.
(2) Uraisi wake utaongeza mpasuko ndani ya chama cha mapinduzi na serikalini hasa kwenye vyombo vya usalama na kutakuwa na kulipiza visasi na kuhujumiana sana kuonyesha kila upande ulivyo na uwezo mdogo wa utendaji jambo litakaloongeza gharama za uendeshaji na matumizi mabaya wa taasisi za serikali
(3) Kutokana na mambo hayo mawili ufanisi wa serikali na vyombo vyake utakuwa mdogo sana hivyo uchumi utayumba, rushwa itaongezeka sana na itatuumiza, kutakuwa na Serikali ya kulazimishana na kutokana na hilo vyama vya upinzania vitapata nguvu sana (4) Kuongezeka kwa nguvu ya vyama vya upinzania kutafanya Serikali izidi kuwa ya kigandamizi kuua kabisa haki za msingi za kiraia. Hivyo fedha nyingi sana na nchi zitatumika kwa ajili ya kugandamiza haki za binadamu badala kulipia gharama za maendeleo.
Kitendo cha kusema eti kama angeendelea kuwa Waziri Mkuu hii nchi ingekuwa na maendeleo zaidi ni kitendo cha kuiponda Chama Chake na Serikali iliyoko madarakani ambayo ni kitu kibaya sana kwa mshikamano wa Chama na Serikali. Sidhani kitu hicho kitavumiliwa na Watanzania wenye nia njema na nchi hii.
Vile vile kule kusema kuwa eti walimvizia Mkurugenzi wa Kampuni ya Maji ili wamfukuze kabla hajaenda mahakamani kupata zuio la kimahakama inaonyesha kabisa akipata Urais atakuwa Rais wa namna gani. Kila mtu awe mtanzania au sio ana haki ya kupata haki yake kupitia mahakami na hairuhusiwi Serikali wala mtu yeyote kuzuia haki kwa sababu yeyote.
Ninaomba Watanzania watafakari hilo.
Elimu jimboni kwake imemshinda , ataiweza nchi Nzima?
Mamvi akipata urais basi wakulima waandike wameumia hasa wale wa kilosa ambao kila uchao wanaugomvi Na wafugaji !
Huwezi kuwa Na elimu bora kama huna uhakika wa chakula !
Nimesoma post nyingi sana hapa jf za kumkubali na kumkataa mh. Lowasa. Ila cha ajabu wanaomkataa lowasa hawasemi ni nani hasa anaweza kuchaguliwa ndani ya ccm mwenye uwezo wa kuchuana na upinzani. Inaonekana maji yamewakaa shingoni hawana la kusema. Sasa tuwe wawazi semeni sasa nani ni mbadala wa Lowasa. Kama hamna jengeni umoja mmsapoti kwenye mbio hiz za urais.
Nimesoma post nyingi sana hapa jf za kumkubali na kumkataa mh. Lowasa. Ila cha ajabu wanaomkataa lowasa hawasemi ni nani hasa anaweza kuchaguliwa ndani ya ccm mwenye uwezo wa kuchuana na upinzani. Inaonekana maji yamewakaa shingoni hawana la kusema. Sasa tuwe wawazi semeni sasa nani ni mbadala wa Lowasa. Kama hamna jengeni umoja mmsapoti kwenye mbio hiz za urais.
Mimi naenda mbali zaidi na kusema kuwa CCM yote haifai kuchaguliwa tena.
Swali ni je, ni nani anayefaa zaidi ya CCM?
Nani anafaa?