Lowassa apanda chati kuelekea uchaguzi mkuu 2015

Lowassa apanda chati kuelekea uchaguzi mkuu 2015

Mi ni mmasai wa simanjiro mkuu............ najua ninachosema

kuna kuvaa vazi la kimasai kwa heshima na kuvaa vazi la kimasai kusiko kwa heshima..... Ninajua ninachosema; ukiamua kubisha endelea... ndio maana nimeweka kauli kali ili tujitazame upya kwa kusifia ujinga; hivi wajua ndugu zetu kule zanzibar wanachofanywa?? je wajua pia yanayoendelea kati ya meserani na mto wa mbu na wazungu wachache wanaotumia naivety ya vijana wetu??

TUENDELEE NA HOJA YA UBORA NA STRENGTEHNING YA EL KWENYE DURU ZA SIASA JAMII YANGU NIACHIE NAJUA NATAFUTA NINI HAPO

Kama wewe ni mmasai ndio unapata mamlaka ya kuwatukana wamasai wenzako? jiheshimu usijione wewe bora zaidi ya wenzako kuwatolea kauli za kipuuzi kila binadamu ana haki ya kuheshimiwa.
 
Hakika lowasa akisimamishwa nitamtangaza rasmi mgombea wa CHADEMA kuwa mh rais. Huyu ni mwepesi kama nini. Richmond ilimchafua mpaka basi leo hii ukiongea neno richmond watakwambia ni lowasa ata vijijini.

Ukiongea neno fisadi utaambiwa unamsema lowasa mpaka vijini. Ikiwa pale alumeru ni almost kwake kijana wake alishindwa pamoja na yeye kupanda jukwaani je leo hii lowasa atashindaje musoma huko na kwingineko?
 
Mtoa mada siku zote ni mvivu wa kufikiri (lazy affairs) .... just spinning things and justifying his capability to analyse leftovers

barking in a sound proof room
 
Mwaka 1995 Mwalimu Nyerere alimzuia Lowassa kuendelea na harakati zake za kutaka urais kwa hoja kwamba mali alizo nazo hawezi kutoa maelezo ya jinsi alivyozipata? Hapa Mwalimu alikuwa anatuonyesha wazi kuwa Lowassa si mwadirifu ndiyo maana akamwambia " urais hapana". Hadi Baba wa Taifa anaenda kaburini; Lowassa hakuwahi kujibu hoja hiyo ya Mwalimu. Maana yake ni kwamba; alikubaliana na hoja hiyo. Kama mtu ana mali lakini hawezi kueleza alivyozipata, inawezekana aliiba, alidhurumu, alitapeli? Pamoja na kwamba Nyerere hayupo nasi, lakini aliyoyasema dhidi ya Lowassa hayatafutika. Alichokisema Nyerere dhidi yake kilithibitika mara baada ya kupata u waziri mkuu pale alipojizamisha mwenyewe kwenye tope la Richmond. Kutokana na kufikiri kwa mtindo aliousema Dk. Masaburi, baadhi yetu tumejikuta tukitoa hoja kwamba eti alitolewa kafara. Hoja hii ni mfu na haina mashiko isipokuwa kwa wale tu wanaofikiri kwa kutumia makalio. Nape na hata Jakaya mwenyewe aliwahi kunukuriwa mara nyingi akimnyoshea kidole Lowassa na mafisadi wengine kiasi cha kuwaita magamba na kuwataka wajiondoe wenyewe kabla hawajaondolewa kwenye nafasi za uongozi ndani ya chama hicho. Rostitamu aliufyata mkia na kubwaga manyanga huku akisema aliamua kuachia ngazi ili kuachana na siasa uchwara za ccm. Magamba sugu yaliziba pamba masikioni, na kuanza mikakati ya kuepuka kufa peke yao. Mnakumbuka Lowassa alijitokeza na kumnyoshea kidole JK kwamba hakuna asichokijua kuhusu Richmond. Kwa kufikiri kwa mtindo ule ule; baadhi yetu tukaanza kuropoka eti Lowassa litolewa kafara. Hapo kuna kafara gani? Kama ni mzalendo na mwadirifu; kwa nini asingekataa kukubali kutumiwa kuhujumu taifa kwa kuingia mkataba na kampuni ya kitapeli ya Richmond? Kama alijali zaidi tumbo lake badala ya maslahi ya taifa; huyo ndiye leo bila haya watu wajitokeze kumpigia debe eti anapanda chati? Kwa utafiti gani uliofanyika? Huu si ushabiki, propaganda na tabia za kulamba viatu? Tangu Lowassa alipomtisha nyau, Nape na wapiga debe wengine wa CCM wamekaa kimya, wimbo wa magamba umekufa.
Moja ya sifa kuu za kiongozi wa nchi ni uzalendo na uadirifu. Lowassa hana hizo sifa. Tulipuuza ya Nyerere, akapewa u Pm, akaangukia pua kwa kashfa ya Richmond inayoligharimu taifa hadi kesho kutwa, sasa tunaendelea kupuuza, walevi wanampigia debe awe rahisi. Tafuteni tindikali ya kumsafisha, zaidi ya hapo mtalamba sana viatu na propaganda za kila aina lakini urais hakuna.
 
Mwaka 1995 Mwalimu Nyerere alimzuia Lowassa kuendelea na harakati zake za kutaka urais kwa hoja kwamba mali alizo nazo hawezi kutoa maelezo ya jinsi alivyozipata? Hapa Mwalimu alikuwa anatuonyesha wazi kuwa Lowassa si mwadirifu ndiyo maana akamwambia " urais hapana". Hadi Baba wa Taifa anaenda kaburini; Lowassa hakuwahi kujibu hoja hiyo ya Mwalimu. Maana yake ni kwamba; alikubaliana na hoja hiyo. Kama mtu ana mali lakini hawezi kueleza alivyozipata, inawezekana aliiba, alidhurumu, alitapeli? Pamoja na kwamba Nyerere hayupo nasi, lakini aliyoyasema dhidi ya Lowassa hayatafutika. Alichokisema Nyerere dhidi yake kilithibitika mara baada ya kupata u waziri mkuu pale alipojizamisha mwenyewe kwenye tope la Richmond. Kutokana na kufikiri kwa mtindo aliousema Dk. Masaburi, baadhi yetu tumejikuta tukitoa hoja kwamba eti alitolewa kafara. Hoja hii ni mfu na haina mashiko isipokuwa kwa wale tu wanaofikiri kwa kutumia makalio. Nape na hata Jakaya mwenyewe aliwahi kunukuriwa mara nyingi akimnyoshea kidole Lowassa na mafisadi wengine kiasi cha kuwaita magamba na kuwataka wajiondoe wenyewe kabla hawajaondolewa kwenye nafasi za uongozi ndani ya chama hicho. Rostitamu aliufyata mkia na kubwaga manyanga huku akisema aliamua kuachia ngazi ili kuachana na siasa uchwara za ccm. Magamba sugu yaliziba pamba masikioni, na kuanza mikakati ya kuepuka kufa peke yao. Mnakumbuka Lowassa alijitokeza na kumnyoshea kidole JK kwamba hakuna asichokijua kuhusu Richmond. Kwa kufikiri kwa mtindo ule ule; baadhi yetu tukaanza kuropoka eti Lowassa litolewa kafara. Hapo kuna kafara gani? Kama ni mzalendo na mwadirifu; kwa nini asingekataa kukubali kutumiwa kuhujumu taifa kwa kuingia mkataba na kampuni ya kitapeli ya Richmond? Kama alijali zaidi tumbo lake badala ya maslahi ya taifa; huyo ndiye leo bila haya watu wajitokeze kumpigia debe eti anapanda chati? Kwa utafiti gani uliofanyika? Huu si ushabiki, propaganda na tabia za kulamba viatu? Tangu Lowassa alipomtisha nyau, Nape na wapiga debe wengine wa CCM wamekaa kimya, wimbo wa magamba umekufa.
Moja ya sifa kuu za kiongozi wa nchi ni uzalendo na uadirifu. Lowassa hana hizo sifa. Tulipuuza ya Nyerere, akapewa u Pm, akaangukia pua kwa kashfa ya Richmond inayoligharimu taifa hadi kesho kutwa, sasa tunaendelea kupuuza, walevi wanampigia debe awe rahisi. Tafuteni tindikali ya kumsafisha, zaidi ya hapo mtalamba sana viatu na propaganda za kila aina lakini urais hakuna.
 
kwitega,
Naona unaongea maneno mengi bila data wala facts za kutosha, ni wapi imeandikwa ukiwa tajiri ni marufuku kugombea kiti cha urais Tanzania.

Mwalimu Nyerere tunamuheshimu kama rais wetu wa kwanza lakini sio anachosema yeye kwetu hiyo ni amri hapana Mwalimu ni binadamu kama binadamu wengine, labda nikuulize Mwalimu alikuwa sahihi kutuchagulia Mkapa, ambaye kauza migodi yetu kwa wazungu na kujiuzia mgodi wa makaa ya mawe.

Kwa kifupi, Lowassa si mtu wa kukaa ofisini. Ni mtu wa kufuatilia kila jambo analoamini katika dhamira yake kwamba linafaa kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania.
 
Last edited by a moderator:
CCM yote ni GAMBA.Ndani ya CCM hakuna chaguo la Watanzania kwa vile wote ninyi hata kama mngeweza kujivua magamba yenu mngebaki nyoka tu.Asante kwa Gamba CCM kutufikisha hapa tulipo ambapo ninyi na familia zenu mnaishi maisha ya mbinguni na sisi tunaishi maisha ya ahera.Tumechoka na sera zenu za kutuambia na kutuaaminisha kuwa nchi hii ni masikini ili ninyi na familia zenu muendelee kufaidi utajiri wa nchi hii.2015 ndio kiama yenu.Angalia zomeazomea kwa Waziri Mkuu(mtoto wa mkulima) pale Mwanza ni rasharasha za mwanzo wa CCM kuiaga nchi hii.CCM itabaki kuwa kwenye vitabu vya historia ya nchi hii kama ilivyo kwa KANU ya Kenya na UNIP ya Zambia.Byebye CCM na Lowassa wenu.
 
Haya ni madogo, wakati ni waziri wa maji aliwafurumusha city water in 24 hrs, lakini ule mkataba wa kihuni uliokuwa unawapa mamlaka Egypt ya kumiliki maji ya mto Nile, ukitaka kuyatumia kwa kilimo uiombe Misri aliuvunjilia mbali na hakuna anayesema hadi sasa, lakini kama hiyo haitoshi aliweza kuhamashisha kuenga shule za sekondari nchi nzima ndani ya mwaka mmoja. Hizi yuhuma za kinafiki aliwajibika kama Mzee Rukhsa. Najua wengi humu kijiweni niviraza na wanafiki lakini naamini mnajutia unafiki wenu kinafiki hivyo hivyo moyoni. Haters always are ******
 
Mkuu usitoe shutuma kwa watu kwa kuhisi weka ushahidi zaidi ya hapo utakuwa unajenga kiwanda cha uongo.


Wanaojua wote hawawezi pinga haya!!

Wewe endekeza mapenzi yaliyokuvalisha miwani ya mbao! Lowassa ni mtaji wa kuchukua nchi kwa CDM kama ulikuwa hujui! Vita kubwa kati yake na mwenyekiti wa CCM sijui kuna nani ana uwezo kuiondoa, ikiwa hata mshiriki mwenzao ameshindwa kuwapatanisha!!

Hiyo milio yako ya gitaa inaburudisha jamvi, thanks.
 
Katikahotuba zake zote sijawahi kumsikia Marehemu Mwl Nyerere anamkataza LOWASA hasigombee, huo ni uchuro wa kukata tamaa na woga. Mbona Lowasa anawatoa povu na hata hajasemakama anagombea. Je akisema si mtatoa uharo nyie viraza, Tatizo ni ndoto a kizamani kutegemea kisichokuwepo, chama cha kuitoa CCM bado kabisa miaka mingi sana mbele. Huo ndio ukweli. Sio hiyo CHAGAN DEVELOPMENT MANIFESTO (CHADEMA) na MOVEMENT FOR CHAGAN (M4C) yao (hamwoni?) wala hiyo mchakamchaka chinja ahaaaaaaaa. Kumsidikiza bwana harusi kwenda kumchukua biharusi kama wapambe rukhsa. Lowasa jembe kubali, kataa moyo ukusute
 
Wanabodi,

Wakati mchakato wa Uchaguzi ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM unaendelea kuanzia ngazi ya shina hadi taifa. Mbunge wa Monduli Edward Lowassa anaonekana kupanda chati kwa kasi ya ajabu na kuonekana ana nafasi kubwa katika mbio za urais 2015.

Uchambuzi wa kisiasa unaonesha karibu kila kona ya nchi hii, katika watanzania 10 utakaowahoji kuhusu ni nani hasa anayefaa kumrithi Rais wa sasa Kikwete, saba kati yao wanamtaja Lowassa wakidai ni "Jembe" linalopigania haki na maendeleo ya kila Mtanzania.

Makundi makubwa yanayotajwa katika mnyukanakano huo ni pamoja na kundi la Lowassa, Samwel Sitta, na Bernad Membe. Kila mmoja anapambana kufa na kupona kuhakikisha kwamba wanaingiza watu wao muhimu katika vikao vya (NEC) na ndani ya Jumuiya za chama hicho, UVCCM, UWT, na Wazazi, katika makundi yote hayo Lowassa anaonekana kuwa ni mtu makini ana nafasi kubwa ya kupenya na kupererusha bendera ya chama hicho.

Kusimama kwa Lowassa kama mgombea Urais ni pigo kubwa kwa vyama vya siasa hasa Chadema, CUF na NCCR Mageuzi. Kutokana na rekodi ya Lowassa, ni mtu wa kufuatilia kila jambo analoamini katika dhamira yake kwamba linafaa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi ni mwenye hulka ya kusaidia na kuchangia shughuli za kijamii bila kujali itikadi za kisiasa wala dini, tofauti na viongozi wengine wa kisiasa amekuwa mtu tegemeo katika shughuli za kijamii iwe za kanisani au msikitini.

Ukitaka kumjua Lowassa ni kiongozi wa namna gani, tembelea jimboni kwake Monduli ukaone namna alivyowezesha makundi ya vijana na wazee kiuchumi.
RITZ is taking a side!!!!umhaidiwa nini mkuu?Ukuu wa Mkoa nn?
 
Lowasa ni kiongozi shupavu aliyekubali kupigwa risasi kumuokoa JK na serikali yake. Nguvu ya pesa yaigawa CCM, 2015 ni Lowasa na Wapinzani
 
Ngome ya Chadema ipo Kaskazini na sehemu alizopata kura Dr Slaa zinafahamika ni sehemu chache sana, sehemu kubwa ya Kaskazini Lowassa akisimama anapita, Chadema watapata sehemu za Arusha Mjini na baadhi ya maeneo ya Karatu na Arumeru.

ukweli unaujua lakini kubali mpaka 2015
 
Bahati nzuri hata Pro-Chadema hawana cha kusema dhidi ya Lowassa, nakumbuka Lowassa alivyowambia kwa macho makavu watawala wa Misri kwamba wananchi wetu hawewezi kukabiliwa na kero ya kukosa maji wakati tuna ziwa kubwa linalotiririsha maji, Rais Mkapa aliingiwa na hofu akiamini kwamba huo mradi utaleta vita baina yetu na Misri, lakini Lowassa alisema liwalo liwe lazima watanzania wapate maji, Mirsi wakafytata mkia, na hatimaye saizi Shinyanga, Mwanza hawana tena tatizo la maji dogo hilo.
 
Last edited by a moderator:
Kinacho mbeba Lowassa ni mtu mwenye hulka ya kusaidia na kuchangia shughuli za kijamii bila kujali itikadi za kisiasa wala dini amekuwa mtu tegemeo katika shughuli za kijamii iwe Msikitini au Kanisani hata hawa makamanda nadhani wanamjua vizuri "jembe" Lowass, Mkandara, hippocratessocrates, Remmy, POMPO, MNYISANZU, Ndallo, Preta, Chasha, Mzito Kabwela, Mungi, Molemo, OSOKONI, Crashwise.
Mkuu, naona umeamua kuwa kampeni Menaja wa Edo, nasikia Kinana amekuachia mikoba, hongera sana kamanda.
ila kufikia saa4 siku ya uchaguzi tutakuwa tunasherekea kuingia magogoni!
 
Wanabodi,

Wakati mchakato wa Uchaguzi ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM unaendelea kuanzia ngazi ya shina hadi taifa. Mbunge wa Monduli Edward Lowassa anaonekana kupanda chati kwa kasi ya ajabu na kuonekana ana nafasi kubwa katika mbio za urais 2015.

Uchambuzi wa kisiasa unaonesha karibu kila kona ya nchi hii, katika watanzania 10 utakaowahoji kuhusu ni nani hasa anayefaa kumrithi Rais wa sasa Kikwete, saba kati yao wanamtaja Lowassa wakidai ni "Jembe" linalopigania haki na maendeleo ya kila Mtanzania.

Makundi makubwa yanayotajwa katika mnyukanakano huo ni pamoja na kundi la Lowassa, Samwel Sitta, na Bernad Membe. Kila mmoja anapambana kufa na kupona kuhakikisha kwamba wanaingiza watu wao muhimu katika vikao vya (NEC) na ndani ya Jumuiya za chama hicho, UVCCM, UWT, na Wazazi, katika makundi yote hayo Lowassa anaonekana kuwa ni mtu makini ana nafasi kubwa ya kupenya na kupererusha bendera ya chama hicho.

Kusimama kwa Lowassa kama mgombea Urais ni pigo kubwa kwa vyama vya siasa hasa Chadema, CUF na NCCR Mageuzi. Kutokana na rekodi ya Lowassa, ni mtu wa kufuatilia kila jambo analoamini katika dhamira yake kwamba linafaa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi ni mwenye hulka ya kusaidia na kuchangia shughuli za kijamii bila kujali itikadi za kisiasa wala dini, tofauti na viongozi wengine wa kisiasa amekuwa mtu tegemeo katika shughuli za kijamii iwe za kanisani au msikitini.

Ukitaka kumjua Lowassa ni kiongozi wa namna gani, tembelea jimboni kwake Monduli ukaone namna alivyowezesha makundi ya vijana na wazee kiuchumi.

Bora ya Fisadi ambaye amewekeza mali zake hapa Tanzania na tunaziona kuliko mafisadi ambao wametuibia na hatujui hizo mali zao ziko wapi! Naunga mkono uzi wako RITZ!
 
Back
Top Bottom