Desprospero
JF-Expert Member
- Feb 1, 2023
- 887
- 2,201
Jana nimemsikia mtoto wa Marehemu Edward Lowassa ambaye pia ni Mtunga Sheria (Mbunge) Fred Lowassa akimshikuru Rais Samia Suluhu Hassan na kusema, "kama si Rais Samia baba asingefika Jumamosi alipofariki" kwamba ni Samia alijitolea Kwa hali na mali kuhakikisha Lowassa anapata matibabu anayostahili.
Kwanza nimwambie dogo kwamba si Rais Samia aliyemfanya baba yake achelewe kufariki bali ni Mungu wake aliyeshikilia uhai wake kwa muda wote. Na akumbule kwamba clinically Edward Lowassa alifariki zaidi ya siku 18 kabla ya tarehe 10/2/2024 isipokuwa kilichokuwa kikidunda ni moyo wake kwa usaidizi wa mashine ambayo isingechomolewa angeendelea kudunda hadi leo lakini kwa busara za madaktari wanakuambia ukweli kwamba, "kwetu clinically huyu mtu ameshafariki " kazi inabaki kwenu familia tuchomoe mashine au la?
La pili kwa dogo Mtunga Sheria ni kwamba Lowassa alitibiwa kwa mujibu wa sheria ya mafao kwa viongozi namba 14. Sheria hii inataka mstaafu kama Waziri Mkuu atibiwe kwa gharama yoyote. Kwa hiyo asimshukuru Rais Samia maana matibu yake ni TAKWA la kisheria na si hisani ya Rais au mtu yeyote. Hata mawaziri Wakuu wastaafu waliosalia kama Sumaye, Warioba, Msuya, Malechela nao wanafanyiwa au watafanyiwa hivyo hivyo ili kukidhi TAKWA la kisheria.
Wanatibiwa kwa kodi za kila raia wa nchi hii bila kuangalia Vyama vyao. Tusitumie vibaya matibabu ya wastaafu wetu na vifo vyao kisiasa. Chadema, CCM, CUF, TLP, SAU, ACT, NCCR na wasio na Vyama wamemtibia Edward Lowassa.
Tuendelee kuwaomboleza Edward Lowassa, Balozi Dk. Deo Kamara, Dk. Ibrahim Msabaha na wengine wengi ambao hawajatangazwa.
Kwanza nimwambie dogo kwamba si Rais Samia aliyemfanya baba yake achelewe kufariki bali ni Mungu wake aliyeshikilia uhai wake kwa muda wote. Na akumbule kwamba clinically Edward Lowassa alifariki zaidi ya siku 18 kabla ya tarehe 10/2/2024 isipokuwa kilichokuwa kikidunda ni moyo wake kwa usaidizi wa mashine ambayo isingechomolewa angeendelea kudunda hadi leo lakini kwa busara za madaktari wanakuambia ukweli kwamba, "kwetu clinically huyu mtu ameshafariki " kazi inabaki kwenu familia tuchomoe mashine au la?
La pili kwa dogo Mtunga Sheria ni kwamba Lowassa alitibiwa kwa mujibu wa sheria ya mafao kwa viongozi namba 14. Sheria hii inataka mstaafu kama Waziri Mkuu atibiwe kwa gharama yoyote. Kwa hiyo asimshukuru Rais Samia maana matibu yake ni TAKWA la kisheria na si hisani ya Rais au mtu yeyote. Hata mawaziri Wakuu wastaafu waliosalia kama Sumaye, Warioba, Msuya, Malechela nao wanafanyiwa au watafanyiwa hivyo hivyo ili kukidhi TAKWA la kisheria.
Wanatibiwa kwa kodi za kila raia wa nchi hii bila kuangalia Vyama vyao. Tusitumie vibaya matibabu ya wastaafu wetu na vifo vyao kisiasa. Chadema, CCM, CUF, TLP, SAU, ACT, NCCR na wasio na Vyama wamemtibia Edward Lowassa.
Tuendelee kuwaomboleza Edward Lowassa, Balozi Dk. Deo Kamara, Dk. Ibrahim Msabaha na wengine wengi ambao hawajatangazwa.