Fred Lowassa kumshukuru Rais Samia pekee kwa matibabu ya Baba yake, atakuwa amekosea

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,162
Nilimsikia Fred Lowassa katika salaam zake za rambirambi pale Karimjee Hall, akitoa shukurani zake za dhati Kwa Rais Samia Kwa matibabu ya Baba yake, Hayati Edward Lowassa na kwenda mbali zaidi Kwa kutamka kuwa kama siyo Kwa msaada mkubwa aliotoa Rais Samia, baba yake asingeweza kufikia majuzi, wakati Mungu alipotwaa roho yake

Nimejiuliza maswali kadhaa kuhusu kauli hiyo ya mtoto wa Hayati Edward Lowassa, alikuwa akimaanisha Nini?

Najua wazi kuwa Hayati Edward Lowassa, kutokana na nyadhifa mbalmbali alizoshika hapa nchini, ikiwemo Waziri Mkuu mstaafu alistahili kupata Huduma hiyo ya matibabu katika kiwango Cha "first class"

Sasa najiuliza hivi Rais Samia alichofanya Cha ziada katika matibabu ya Hayati Lowassa ni kipi??

Swali la pili najiuliza, iwapo Rais Samia, aliidhinisha malipo ya ziada Kwa matibabu ya Lowassa, hizo sifa zilipaswa zitujie sote wananchi wa nchi hii, Kwa kuwa yeye Rais Samia, hakutoa pesa hizo kutoka mifukoni make, Bali "alizichota" kutoka kwenye hazina yetu ya Taifa, ambazo ni pesa za walipa Kodi wa sisi wananchi wa nchi hii

Hata hivyo namkosoa Fred Lowassa alipotamka kuwa kama siyo Rais Samia, Basi baba yake asingeweza hata kufikia siku hiyo aliyofariki!

Anachosahau Fred Lowassa, ni kuwa sisi binadamu wote, tunahesabiwa siku zetu za kuishi hapa duniani na Mungu pekee!

Kwa mawazo ya Fred Lowassa, kama Rais Samia, ndiye amerefisha maisha ya baba yake, ambaye amefikisha umri wa miaka 70 hadi pale alipofariki, basi tusingeweza kuwapata maelfu ya wazee masikini wasio na kitu, wanaishi hadi miaka zaidi ya 100

Ujumbe wangu Kwa sisi binadamu, tunapaswa kwanza kutoa shukurani Kwa Mungu aliyetuumba, Kwa lolote jema linalotutokea hapa duniani, badala ya kutoa sifa Kwa binadamu wenzetu, ambao nao wameumbwa na Mungu wetu
 
Siku yako ikifika unasepa mapema tuu hakuna cha nywenywenywe asingekuwepo ingekuwa nywenywenywe
Anachosahau huyo Fred Lowassa ni kuwa tuna wazee kibao huko vijijini kwetu wanafikisha umri wa zaidi ya miaka 100, wakiwa hawana hata na bima za maisha.

Sasa nashangaa Kwa huyo Fred Lowassa, kumshukuru Rais Samia na kudai kuwa kama si yeye Rais Samia, basi baba yake asingeweza kufikia umri huo!

Lazima sisi binadamu tutambue kuwa uhai wetu ni kutokana na neema zake Mungu pekee
 
Nilimsikia Fred Lowassa katika salaam zake za rambirambi pale Karimjee Hall, akitoa shukurani zake za dhati Kwa Rais Samia Kwa matibabu ya Baba yake, Hayati Edward Lowassa na kwenda mbali zaidi Kwa kutamka kuwa kama siyo Kwa msaada mkubwa aliotoa Rais Samia, baba yake asingeweza kufikia majuzi, wakati Mungu alipotwaa roho yake

Nimejiuliza maswali kadhaa kuhusu kauli hiyo ya mtoto wa Hayati Edward Lowassa, alikuwa akimaanisha Nini?

Najua wazi kuwa Hayati Edward Lowassa, kutokana na nyadhifa mbalmbali alizoshika hapa nchini, ikiwemo Waziri Mkuu mstaafu alistahili kupata Huduma hiyo ya matibabu katika kiwango Cha "first class"

Sasa najiuliza hivi Rais Samia alichofanya Cha ziada katika matibabu ya Hayati Lowassa ni kipi??

Swali la pili najiuliza, iwapo Rais Samia, aliidhinisha malipo ya ziada Kwa matibabu ya Lowassa, hizo sifa zilipaswa zitujie sote wananchi wa nchi hii, Kwa kuwa yeye Rais Samia, hakutoa pesa hizo kutoka mifukoni make, Bali "alizichota" kutoka kwenye hazina yetu ya Taifa, ambazo ni pesa za walipa Kodi wa sisi wananchi wa nchi hii

Hata hivyo namkosoa Fred Lowassa alipotamka kuwa kama siyo Rais Samia, Basi baba yake asingeweza hata kufikia siku hiyo aliyofariki!

Anachosahau Fred Lowassa, ni kuwa sisi binadamu wote, tunahesabiwa siku zetu za kuishi hapa duniani na Mungu pekee!

Kwa mawazo ya Fred Lowassa, kama Rais Samia, ndiye amerefisha maisha ya baba yake, ambaye amefikisha umri wa miaka 70 hadi pale alipofariki, basi tusingeweza kuwapata maelfu ya wazee masikini wasio na kitu, wanaishi hadi miaka zaidi ya 100

Ujumbe wangu Kwa sisi binadamu, tunapaswa kwanza kutoa shukurani Kwa Mungu aliyetuumba, Kwa lolote jema linalotutokea hapa duniani, badala ya kutoa sifa Kwa binadamu wenzetu, ambao nao wameumbwa na Mungu wetu
Rais ni muwakilisha wa waTanzania wote.

Kumshukuru rais ni sawa tu na kuwashukuru waTanzania wote.

Rais ni nembo ya Tanzania, ni alama ya umoja, amani na mshikamano wa waTanzania....

Kumshuru Mungu kwaajili ya ukarimu wa Dr.SSH kwa ENL ni muhimu zaid pia...

R.I.P Laigwanan comrade ENL
 
Rais ni muwakilisha wa waTanzania wote.

Kumshukuru rais ni sawa tu na kuwashukuru waTanzania wote.

Rais ni nembo ya Tanzania, ni alama ya umoja, amani na mshikamano wa waTanzania....

Kumshuru Mungu kwaajili ya ukarimu wa Dr.SSH kwa ENL ni muhimu zaid pia...

R.I.P Laigwanan comrade ENL
Huwa mnaanza hivihivi kidogokidogo mwisho mnawaita ni miungu.Refer mzee wa mifuko ya shati kushonwa bendera ya taifa aka Kangi.
 
Kwa hiyo S100 ana uwezo wa kurefusha maisha ya binadamu !!!!.Fred ni hopeless kabisa.
Kwa kweli inashangaza sana, hasa tukitilia maanani huyo aliyetamka hivyo ni Mbunge ambaye anawawakilisha wapiga kura wake wa Jimbo la Monduli!
 
Fred amezaliwa na kukulia katika mazingira ya kitajiri na kimamlaka za kidunia .
Hajui shida yoyote toka amezaliwa watu wa aina hii ndiyo kawaida kuongea kauli aliyoongea.

Watu wa aina hii hawajui kuwa MUNGU ndiyo muwezesha wa yote iwe ni afya , uzima, chakula na kila kitu .
Watu wa aina hii wanakuwa na viburi kwa sababu ya utajiri na mamlaka .
 
Uchawa uliaasisiwa kipindi cha magufuli umeliathiri taifa sasa hivi mtu hata mkewe akipata mimba anamshukuru rais
 
Back
Top Bottom