Lowassa afunika dar

Lowassa afunika dar

Imedhihirika leo kwamba mh Edward Lowassa sio tu kwamba anapendwa bali pia ni tegemeo kubwa kwa watanzania wanyonge na wa hali ya chini.
Umati wa watu ambao haujawahi kuonekana pamoja na waendesha bodaboda wapatao elfu zaidi ya elfu ishiriki wamejumuika nae leo wakati alipokaribishwa kuwa mgeni rasmi wa chama chao.
Tuache uzuzu, EL hatufai. Labda kama tunataka miaka 10 mingine ya misery. Alichofanya yeye, JK na Rostam kupitia Richmond itufungue macho. HATUFAI!!!
 
Huyu jamaa ni kiboko.cdm wakisikia jina lake kitu kinagonga chupi

hahaha hahaha kweli anawatia cdm kiwewe sana kuna mtu yupo jkoni cdm pale knondon ananiambia hofu yao kubwa ni ccm ikimptsha lowasa hali yao itakua ngumu si tu atashnda urais kwa kshndo ila ata majmbo yanayoshkiliwa na cdm yatapungua sana.
mfano halisi ben saanane hakuna thread yenye jina la lowasa asiyochangia ambaye inaaminika ni mfuasi wa mbowe na membe
 
alikuwa lowasa huyuhuyu fisadi,
huyu aliyekataliwa na nyerere!,
kweli watz tuna vichwa vya panzi.
Gharama za umeme bado zinatutesa kwa sababu yake, watu wanamshabikia, dah! hii ni hatari!
 
Kuna Mijitu inatia hasira ***** zao ..Hata kama ni njaa ya pesa huku ni kujidhalilisha..Maisha yetu yamekuwa Maigizo!!..Mtu anaigiza mbele yetu na tunajua kabisa anaigiza..Leo Inasukuma gari kama Mishyoga..Kaifanyia nini nchi zaidi ya kuiingiza kwenye madeni na kuipa hasara??

Lini tutaelimika na kuacha siasa za ushabiki??

Masikini wa Akili ni Masikini kuliko Masikini yeyote yule..

Hii ndiyo Tanzania..Bado tuna safari ndefu sana..🙁

kweli nimeamini hicho kichwa umebeba kwaajili ya kufugia nywele tu,badala ya kufikiria,kwahy maisha magumu kwako yamechangiwa na lowassa,sass nikwambie tu maisha magumu yamesababishwa na wazaz wako,kama cyo wazaz ni ww pekeyako kutotaka kunijishughulisha
 
Tuache uzuzu, EL hatufai. Labda kama tunataka miaka 10 mingine ya misery. Alichofanya yeye, JK na Rostam kupitia Richmond itufungue macho. HATUFAI!!!

wewe nenda kaandamane kama mlvyozoea..sisi wstanzania tunaojtambua tunamtaka lowasa kiongoz jasri tumechoka na business as usual
 
Imedhihirika leo kwamba mh Edward Lowassa sio tu kwamba anapendwa bali pia ni tegemeo kubwa kwa watanzania wanyonge na wa hali ya chini.
Umati wa watu ambao haujawahi kuonekana pamoja na waendesha bodaboda wapatao elfu zaidi ya elfu ishiriki wamejumuika nae leo wakati alipokaribishwa kuwa mgeni rasmi wa chama chao.

Huko kupendeka kwake unakuona wewe tu na wenzako wa aina yako (mliopewa vi-pesa ili mpe promo). But rest assured kuwa project yenu imeshindwa hata kabla haijaanza kuwa implemented! Kumbukeni KIBAYA CHAJIUZA...!
 
Watanzania bwana noma sana.Wanashabikia kifo.Mmm,haya ngoja aingie Ikulu wamalizie kazi.
Imedhihirika leo kwamba mh
Edward Lowassa sio tu kwamba anapendwa bali pia ni tegemeo kubwa kwa
watanzania wanyonge na wa hali ya chini.
Umati wa watu ambao haujawahi kuonekana pamoja na waendesha bodaboda
wapatao elfu zaidi ya elfu ishiriki wamejumuika nae leo wakati
alipokaribishwa kuwa mgeni rasmi wa chama chao.
 
attachment.php
 
Ndo nashagaa kuna watu wamebeba bango jana eti zitto kama mandela..!!! Ujinga mtupu
Mimi jana watu hao niliwaeleza hivi (soma bolded text) hapo chini

>>>https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-katika-mapokezi-ya-zitto-27.html#post8157753


Kwanza ninampa Hongera sana Zitto kwa kufika salama nyumbani kwao Kigoma ya watanzania. Nina imani ujio wake huko utakuwa na maana sana kwa watanzania wanaoishi huko. Kwa kuangalia viunga vya mahali msafara umepita unaonyesha kabisa Zitto hajamaliza kazi ya kusaidia kuwaletea maendeleo watanzania waishio Kigoma.

Madhumuni ya 'post' hii ni kuonyesha kutofurahishwa na maneno ambayo yasemekana Zitto. Maneno hayo nimeyapaka rangi Nyekundu hapo juu.

Kama kweli Zitto ameyasema , basi amethibitisha kuwa ana udhaifu mkubwa wa kiuongozi. Ni udhaifu mkubwa kwa sababu huwezi kumtofautisha na Idd Amini (aliyekuwa Rais wa Uganda). Ni watu jamii ya Idd Amini waliokuwa wanajikweza kwa kujipa vyeo lukuki mbele ya wale anaowaongoza ni hii ni dalili ya ubinafsi, ambayo haifai kuwa sifa ya kiongozi bora. Sote tunajua alichoifanyia Uganda na Tanzania Idd Amini.

Pia nimesoma baadhi ya mabango kwenye picha yakisema " Zitto kama Mandela, Zitto kama Nyerere". Hao wote waliofananishwa naye hakuna hata mmoja ambaye alikuwa anajikweza juu ya wenzake , kama kumbukumbu zangu ziko sahihi.

Ni haki ya watanzania waishio Kigoma kumpokea mbunge wao kama walivyofanya, lakini kama wanataka aendelea kuwawakirisha basi hawana budi ku'mfunda' Zitto zaidi kuwa kiongozi mwenye sifa zinazofaa.
 
Acheni Watqnzania wamchague mtu yeyote wanayemtaka awe rais wao. Nyie na Nyerere ndiyo nani wa kutuchagulia rais? Hata awe munchafue vipi, kama Watanzania wengi wanamtaka Lowasa awe rais wao na itakuwa hivyo. Zama za kuchaguliwa rais na mtu mmoja akiongozwa na maslahi yake yamepitwa na wakati...
 
Anayejua kuhesabu mojaaa, mbiliiii hana haja ya kuujua uwezo wa Fisadi yeyote. Fisadi yeyote akiitaka nchi ataichukua alfajiri kabla ya saa sita mchana.
Kumbuka kidogo tu. Richmond ililipwa Tshs. milion 150 kwa siku kwa muda wa siku 180. Mnaojua mahesabu, Ningekuwa ni mimi nasaka Ikulu. Nikitoa malipo ya siku moja tu. Katika fedha zenu wenyewe mlizoniwekea benki. Naweza kumpa kila Mtz. aliye hai leo Tshs.millioni 3 na bado chenchi ikabakia hapo.
Sasa, kututishia kuwa kulikuwa na boda boda 1000 ndiyo nini kwa ukwasi wake huyu mtu? TAFAKARI. Jamani mie napita tu, nilikuwa naota mchana
 
Baadhi ya Watanzania ni vichwa vya wendawazimu wanachangia kwa kiwango kikubwa sana nchi yetu kubaki nyuma kimaendeleo pamoja na kuwa na utajiri mkubwa sana wa rasilimali mbali mbali. Huyu amekuwa ndani ya Serikali tangu awamu ya kwanza ukiwauliza huyu katika miaka yote hiyo aliyokuwa ndani ya Serikali amefanya lipi ambalo linaonyesha anastahili kupewa ridhaa na Watanzania ili kuiongoza Tanzania!? Wanaanza kung'aa macho!!!! Mtu yupo yupo tu hana vision yoyote ya kuleta maendeleo nchini yuko busy kutoa rushwa huku na kule ikiwemo nyumba za ibada ili anunue Urais kama mwenzie Kikwete!!! Hivi wale wataalamu wake wa kuleta mvua toka Thailand waliishia wapi!?

Watanzania wote tupimwe akili huenda hatujitambui!

Mara hii ya Lowassa wameshayasahau!
 
itafahamika tu siku bado zipo twendeni pamoja kwanza tutaanza kuachana njia panda.

Sasa wewe so utapasuka msamba. Zitto nae anagombea Urais kwa CDM, Lowassa kwa CCM sasa utaenda upande upi
 
Watanzania wote tupimwe akili huenda hatujitambui!

Mara hii ya Lowassa wameshayasahau!

Wengi wanaomshabikia Lowassa hapa ni bendera fuata upepo, ukimuuliza mtu Who's Lowassa, unampendea nini?? Wengi hawana jibu sahihi la kukupa na wachache wenye majibu watakwambia ametupa HELA, hela kiasi gani utajibiwa elfu20 kila mtu na T-shirt.Only that.
 
kweli nimeamini hicho kichwa umebeba kwaajili ya kufugia nywele tu,badala ya kufikiria,kwahy maisha magumu kwako yamechangiwa na lowassa,sass nikwambie tu maisha magumu yamesababishwa na wazaz wako,kama cyo wazaz ni ww pekeyako kutotaka kunijishughulisha

Wapi nilipotaja maisha magumu?

Nimesema ameingiza nchi kwenye madeni na hasara..au huoni hilo wewe unaejiona una akili?

Nazungumzia maisha ya wa-Tanzania kwa ujumla na siyo maisha yangu..

Wewe ni moja kati ya wale niliyo wasema..
 
Chezeaaa EL weweeeeee mtajibebaaaa ambao hamtaaakii
NANI AMENUNAAAAAAAAAAAA??????????
hakuna kama Lowassaaa wengine wasindikizaji tuuuuuu
 
Huko kupendeka kwake unakuona wewe tu na wenzako wa aina yako (mliopewa vi-pesa ili mpe promo). But rest assured kuwa project yenu imeshindwa hata kabla haijaanza kuwa implemented! Kumbukeni KIBAYA CHAJIUZA...!

mtajiharshia sana mpaka 2015...lowasa ndiye rais 2015....lowasa ndye tumain pekee...membe..sta na wala ruzuku tupa kuleeee....lowasa ndio habar ya mjn na vjijin
 
Wengi wanaomshabikia Lowassa hapa ni bendera fuata upepo, ukimuuliza mtu Who's Lowassa, unampendea nini?? Wengi hawana jibu sahihi la kukupa na wachache wenye majibu watakwambia ametupa HELA, hela kiasi gani utajibiwa elfu20 kila mtu na T-shirt.Only that.

vote for lowaaaaaaaaaaaaaaa 2015...kiongoz mchapa kaz aliyebak ni lowasa tuuuuuu
 
Back
Top Bottom