CCM itafanya kosa kubwa sana kumsimamisha Lowassa kuwa mgombea wa Uraisi kwa tiketi ya CCM. Lowassa ana machafu na mabaya mengi ambayo yanaweza kumuangusha vibaya sana. Hii ni ishara ya kuiachia Chadema kuingia Ikulu.
Tukumbuke katika uchaguzi wa jimbo la Arumeru mashariki jinsi Lowassa alivyouumbuka wakati akijaribu kumpigia kampeni mkwe wake dhidi ya mgombea wa Chadema.
Kuna watu safi na wazuri ndani ya CCM ambao wanakubalika nje na ndani ya chama. Hawana doa la ufisadi na ni waadilifu, wana uzalendo wa kweli na Tanzania yetu na wana uwezo wa kujenga na kupangua hoja.
Kwa maoni yangu ninamuona Mh Wassira tu ndiye mwenye uwezo wa kusimama na kupeperusha bendera ya CCM katika kugombea kiti cha Uraisi.