Bitabo
JF-Expert Member
- Sep 27, 2011
- 1,900
- 687
Mkuu para ya Mwisho ina Maoni yako ambayo si sahihi, yanathibitisha kuwa hujui hata Mfumo wa Uchaguzi wa CCM acheni kubuni Tuhuma zisizo na Msingi mnaweza kuhatarisha Maisha ya Watu wasio na Hatia.
Sizungumzii mfumo mkuu bali nazungumzia hali halisi iliyo ndani ya CCM. We tuelezee mfumo wao wa uchaguzi labda nimekosea mwaka wa uchaguzi but waulize wakuu wa CCM watakwambia kuwa EL ana nguvu sana kwenye chama na ndio maana hata kumvua gamab juzi wameshindwa. Mkapa aliliona hilo na ndio maana akamwambia JK funga hiyo hoja watu wasiendelee kuichangia maana aliona JK anavuliwa nguo na watu walishaandaa hoja ya kumvua uenyekiti kama ilivyokuwa kwa Thabo Mbeki wa South na issue ya Zuma.
Kumbuka JK ni mzee wa visasi, kama aliamua kuwa mpole pale Dodoma, uandhani ataendelea kuwa mpole daima? EL ametoka dodoma ameenda kujitangazia ushindi kwenye harambee za makanisa huko Singida. Bado tu huoni kuwa hali ya JK na EL ni tete??
Sina haja ya kubuni tuhuma lakini kwa kuwa wote tuna macho basi tusubiri tuone mwisho wa issue ya magamba utakuwaae. Kama EL akibaki na nguvu zake sioni JK akibaki kuwa M/Kiti wa CCM na sioni hilo likitokea kwa JK kukubali adhalilishwe akiwa madarakani. Sijui mwenzangu mfumo wako wa ucahguzi wa CCM unakwambiaje. Jipime na huo mfumo uone kama utapata majibu sahihi.