Lowassa adaiwa kutaka kuuawa!

Mkuu para ya Mwisho ina Maoni yako ambayo si sahihi, yanathibitisha kuwa hujui hata Mfumo wa Uchaguzi wa CCM acheni kubuni Tuhuma zisizo na Msingi mnaweza kuhatarisha Maisha ya Watu wasio na Hatia.

Sizungumzii mfumo mkuu bali nazungumzia hali halisi iliyo ndani ya CCM. We tuelezee mfumo wao wa uchaguzi labda nimekosea mwaka wa uchaguzi but waulize wakuu wa CCM watakwambia kuwa EL ana nguvu sana kwenye chama na ndio maana hata kumvua gamab juzi wameshindwa. Mkapa aliliona hilo na ndio maana akamwambia JK funga hiyo hoja watu wasiendelee kuichangia maana aliona JK anavuliwa nguo na watu walishaandaa hoja ya kumvua uenyekiti kama ilivyokuwa kwa Thabo Mbeki wa South na issue ya Zuma.

Kumbuka JK ni mzee wa visasi, kama aliamua kuwa mpole pale Dodoma, uandhani ataendelea kuwa mpole daima? EL ametoka dodoma ameenda kujitangazia ushindi kwenye harambee za makanisa huko Singida. Bado tu huoni kuwa hali ya JK na EL ni tete??

Sina haja ya kubuni tuhuma lakini kwa kuwa wote tuna macho basi tusubiri tuone mwisho wa issue ya magamba utakuwaae. Kama EL akibaki na nguvu zake sioni JK akibaki kuwa M/Kiti wa CCM na sioni hilo likitokea kwa JK kukubali adhalilishwe akiwa madarakani. Sijui mwenzangu mfumo wako wa ucahguzi wa CCM unakwambiaje. Jipime na huo mfumo uone kama utapata majibu sahihi.
 
Atakuwa alikosea bia ilikolea lengo alitaka kusema Sitta ana mpango wa kumuua baba yake na Sitta naye anasema anataka kuwawa heee kumbe na Mwakyembe pia
 
EL ndie Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, hivyo TISS iko chini yake unless ni covert oparation kama walivyonfix Imran Kombe!.

wapo TISS wa J.K
wapo wa E.L na R.A
wapo wa Chadema
wapo wa Sitta na Mwakyembe
wapo wale after money(e.g waliomuuzia Mengi mkanda mzima wa mwanawe kubambikiwa madawa)
 
anatafuta huruma za wabongo....hiyo ni straregy tu kwa wenye akili tunajua,nani atamuua huko uwt wakati wapambe wake hapa kutwa wanatuaminisha usalama wa taifa wanamuunga mkono yeye?

kweli kiongozi naona umeusoma mchezo public sympathy is what hes after for 2015
 
afadhali mungesema ana nguvu ndani na nje ya CCM kama ni ndani tu hana ushawishi kwa umma wa watanzania na hawezi kubeba bendera ya CCM kwa kuwa na nguvu ndani tu wakati huku nje ana maadui wengi wanaomchukia kwa ufisadi wake.... Nyerere akiwa mmojawapo hata huko aliko alimwachia laana
 
chanzo cha habari hii ni gazeti la Dira ya Mtanzania, inadai CCM wananjama za kummua Lowasa
walidokezewa na Fred Lowasa, mtoto wa mjini huyu(itakuwa kweli)
mzee wa visasi,ama wafuasi wake wamekerwa na kuvuliwa nguo na E.L kuhusu Richmond

aidha Katibu Mwenezi wa ccm(Nape) amekanusha akidai chama chao hakijawahi na hakitafanya hilo
pia amesisitiza TISS haipo chini ya ccm, hivyo hawana mandate ya kutoa order hata kama wangekua waovu
 
Mara CCM mara TISS hebu wekeni kipande cha gazeti hilo hapa tusome wenyewe ni kama habari inakuzwa mno isitoshe ni ya jumatano wiki iliyopita ingekuwa hot isingechelewa kuletwa hapa Jf na members

mtoto wa kigogo mlevi kaleta balaa nyumbani kwa waziri mkuu msataafu

Usalama wa Taifa ndio jamvi la wanaotaka kuuwawa
 
Mkuu let me be clear

ukisoma post ya pasco amepost kama vile tayari anajua likelihood ya jamaa kuuwawa au la, and that ahs been our weakness as JF members we usually throw some tokens of ideas and runa away from them when asked to justify... unaporejea post ya pasco na jitahidi sana kunielewa natafuta nini

it would have been easier kusema hivi: nijuavyo mimi uwezekano wa kuuwawa lowassa upo au haupo na ni xxx.
Post ya Pasco hii hapa chini sijui hata kama inaelekea ulivyomuuliza mambo ya percentage, hivi wewe tukikuuliza una percentage ngapi ya kuuawa utatuambiaje.
EL ndie Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, hivyo TISS iko chini yake unless ni covert oparation kama walivyonfix Imran Kombe!.
 
chanzo cha habari hii ni gazetila Dira ya Mtanzania, inadai CCM wananjama za kummua Lowasa
walidokezewa na Fred Lowasa, mtoto wa mjini huyu(itakuwa kweli)
mzee wa visasi,ama wafuasi wake wamekerwa na kuvuliwa nguo na E.L kuhusu Richmond

aidha Katibu Mwenezi wa ccm(Nape) amekanusha akidai chama chao hakijawahi nahakitafanya hilo
pia amesisitiza TISS haipo chini ya ccm, hivyo hawana mandate ya kutoa orderhata kama wangekua waovu
Nape ndio kaharibu kabisa hivi CCM hainaga washauri huko ndani maana kujibu kwake ni kama anaongeza mafuta kwenye moto.
 
Kama serikali ilishindwa kumpeleka kwenye vyombo vya dola vismamie sheria basi acha wenye uwezo wa kumhukumu wamhukumu
 
@Mwanajamii nafikiri umeshindwa kunielelewa vizuri,mimi si mtumwa wa Lowasa na siko hapa kumtetea kwa lolote lile. 1./Simuungi mkono Lowasa wala CCM,kifupi watanzania hatutaki kuongozwa tena na mtu yoyote kutoka CCM hata kama ni malaika kutoka mbinguni. 2/Lowasa ni mwanasiasa mchafu sana kama walivyo wanasiasa wengi ndani ya CCM. 3/Lakini utafiti nilioufanya unaonyesha Lowasa ni mwanasiasa mwenye nguvu ndani ya CCM kwa namna alivyopandikiza watu wake kwenye nafasi nyeti na muhimu za kisiasa.Hivyo basi anaweza kujiwezesha au kumwezesha mtu wake apate nafasi ya kugombea urais 2015 ndani ya CCM au hata kwenye vyama vya upinzani!! Kama alimwezesha JK kushinda 2005 katikati ya mwanasiasa machachari(eg.Mwandosya,Salim Hamed Salim,Sumaye,Malecela) vipi asijaribu tena? 4/Kuwa mgombea Kwa tiketi ya CCM ndio jambo muhimu kwake kwa sasa,Kwa kuwa ataungwa mkono na dola,na raia watalazimisha kumkubali kwa ujanjaunja kwenye uchaguzi,kama alivyofanya JK. @Kama hukubaliani na utafiti wangu, tupe utafiti wako nasi tutaupima.
 
nimeon hii habari kwenye gazeti la dira sikumbuki tarehe ila wanadai fred ali kuwa kwenye bar/hoteli arusha akamwona jamaa watiss akamfata na kuanza kumpa shit kwamba hakutegemea mtu kama yeye wanafahamiana vile halafu na yeye anakuwemo kwenye ishu kama hiyo yule jamaa akaita polisi wakamchukua fred mpaka kituoni alipofika wakamwambia aandike statement akagoma nakuanza kulia kwa sana sijui kwa kumuogipa wakamwambia ajidhamini aje kesho pombe ikisha jamaa akaondoka akazima na simu akarudi dar kimya kimya kwa kifupi ndo hivyo
mm asijekuwa uyu mtoto wa fisadi el alikuwa ameshafakamia mibiere ndo akaanza kuongea mipwenti kwa msaada wa chicha
 
Wakuu heshima mbele, kwenye magazeti ya leo imefahamika kuwa Fredrick Lowassa mtoto mkubwa wa EL amereport kuwa UWT wana mpango wa kumuua baba yake kwa kile ambacho hakijawekwa bayana!

Kama ada wanajamvi kwa weledi, tunapenda kujua kimetokea nini ghafla hivyo au ni kujihami baada kushukiwa na kuwalisha sumu baadhi ya wapambanaji wa ufisadi?

Nawasilisha

Mimi naomba nilte sumu niambiwe sumu gani tu inahitajika ntaitafuta kokote pale
 
Back
Top Bottom