BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
Huyu fisadi mbona yuko kimya kuhusana na wizi wa zaidi ya shilingi bilioni mia tatu katika bank account ya Escrow? Je, anakubaliana na maamuzi ya DHAIFU au hakubaliani nayo? Je, anataka pesa zote zirudishwe hazina na wahusika wapandishwe kizimbani au la? Mtu anataka kuwa Rais ndani ya miezi 10 ijayo lakini kwenye issue nzito za Kitaifa anakuwa kimya kabisa akijaribu kuzikwepa kwa kila namna badala ya kutaka kuonyesha kama yuko tayari kutetea maslahi ya Watanzania, pale ambapo kuna wahuni na wezi wamejitajirisha, bila kujali nani ni muhusika. Ukimya wake kwenye hili sakata ni dalili nyingine huyu hafai kuwepa dhamana na Watanzania ya kuiongoza nchi.