Lowaasa Aiteka Zanzibar Xmass

Lowaasa Aiteka Zanzibar Xmass

hata mimi nasaidia kuusakanya
Pasco naomba msaada wako! Kuna uzi mmoja humu nimeupoteza na sikumbuki title wala mwandishi ila uzi ulikuwa unachambua mikakati ya el na kundi lake huku wakitajwa akina rostam na karume!
Mwenye uzi pia aligusia in a nutshell kifo cha Dr. O. Juma ktk harakati za kina jk!
Nautafuta huo uzi mkuu!
 
Hivi kushiriki ibada ndo kusema "kaiteka" Zanzibar?Mh.Lowassa wakati flan alisema kuna watu wanatamani hata kumpangia watu wa kuonana nae na wengine hata wanatamani asishiriki shughuli za kawaida za kijamii kama kushiriki ibada na misiba...hapa anashiriki ibada,mtu anasema kaiteka Zanzibar,how comes?
 
Mkuu ahsante sana mkuu, hapa sasa nimefika kwenyewe
 
pinda hamuwezi lowasa kwa sera hata kidogo, anajipeleka falme za kiarabu kama ndiko atakakopigiwa kura
 
kwako tafsiri ya unyenyekevu ni kwenye mavazi?

Sidhani kama kweli ulitegemea nitakujibu kwa ulichouliza. Kama ulijua nitakupuuza, nakusifu ila kama ulitegemea nitakujibu basi sijui nitakuonaje wewe jamaa?
Ova
 
Hamuogopi, bali anaogopesha!. EL amejaaliwa kitu kinachoitwa karama ya kukubalika ambayo JK hana!.

Wakati wa enzi ya Boys II Men, mikoani wakisikia ni ziara ya JK, ni shangwe tuu miguu juu kwani akiisha tayarishiwa ile taarifa, na kupitishwa kule alikopangiwa, jioni ni kula kunywa siku imepita!.

EL akifanya ziara, haishii kwenye taarifa ya makaratasi, kama amepangiwa kufungua mradi kambi ya Makotupora, kwenye taarifa walisema Msalato vyomba vya madarasa vimekamilika, Ihumwa kisima cha maji kimekamilika na maji yanatoka!, katika ziara yake ya kuelekea Makotupora, kwa vile ndio nji hiyo hiyo, anatangaza kuanzia Msaloto kuona vyumba vya madarasa kisha kupitia Ihumwa kuona kisima ndipo auende Makotu!. Sasa ikatokea kumbe hakuna chumba cha darasa wala mradi wa maji!, kilikuwa kinawaka hapo kwa hapo mbele ya kadamnasi ya watu kwa kutaka maelezo, na kesho yake watu hawana kazi!. Hivyo watu walikuwa wakisikia EL anakuja, ni hakuna kulala!, JK akija ni sherehe tuu!.

Na ndio maana wana CCM wote wenye akili timamu wanaitakia mema nchi hii, mwaka 2015 wanamtaka EL, wasiomtaka ni wale CCM waendekeza matumbo!.

Merry X-Mass

Pasco

Ni sahihi kabisa kama binadamu hawezi kuwa mwema kwa kila mmoja ila ukweli utabaki pale pale huyu jamaa ni Kiongozi bora.
 
Dini zimekuwa dili siku hizi najisalia nyumbani tuu.
 
Back
Top Bottom