London Evening Standard

London Evening Standard

CNN hapa saizi wametoa habari ya Acid attack kwa hao mabinti huko Zanzibar wanarudishwa nyumbani..
JK na watu wake wa usalama waamke sio ishara nzuri hata kidogo..

wala hawajali lolote .
 
Naapa rasmi hapa jf leo , sitoenda tena Zanzibar katika kipindi hiki kifupi nilichobakiwa nacho hapa duniani , afadhali Hata KABUL .
 
Nchi ya Tindikali,unga,ufisadi.ung'oaji watu meno na kucha,mauaji,wizi wa mali ya umma,kuua tembo,udini nk


Waulizwe hao WAISLAMU wa Zanzibar hao watoto wenye miaka 18 wamewakosea nini hadi kuwapa adhabu isiyowafaa kiasi hicho?

Walikuwa kwenye Mfungo wa Ramadhani,ndiyo mawaidha yaliyokuwa yakitolewa hayo kuwafanyizia watu wasio na kosa lolote bila sababu za msingi?


TUNAOMBA MAJIBU TOKA ZANZIBAR

Sasa mkuu unategemea nani atakujibu haya maswali??
 
Naapa rasmi hapa jf leo , sitoenda tena Zanzibar katika kipindi hiki kifupi nilichobakiwa nacho hapa duniani , afadhali Hata KABUL .

haha kwikwi,utamkomoa nani sasa na hicho kiapo chako.
zanzibar ni njema na atakaye na aje_kar
 
Nina gazeti la jana la London Evening Standard.Ni gazeti linalotolewa free kwenye station zote za reli.Linasomwa na watu 1.69 million jijini London.
Page ya kwanza iliochukua uzito inasoma hivi:

CHARITY GIRLS IN ACID HORROR halafu kuna picha 2 za hawa teenage girls,Kirstie Trup & Katie Gee.

Hii feature article inaendelea hadi page 5 kuna picha zao tena ,kwa ufupi inaelezea walikuwa Zanzibar kuvolunteer kwenye art charity .Katie anatarajiwa kujiunga na Nottingham University kusoma sociology next month na mwingine Bristol Uni kusoma History.

Page 5 also kuna sub-heading "Island paradise with a dark underbelly"
Inaelezea uzuri wa Zanzibar,hata developers kujaribu kuiturn into another Seychelles.Lakini sio hivyo tena ,inasimulia
allegations za uchakachuazi wa matokeo ya uchaguzi na CUF kutaka uhuru toka Tanzania.
Inazungumzia the rise of Islamic Party Uamsho(The Awakening).Pamoja na boom ya utalii,bado kuna matatizo ya ajira,a heroin epidemic na umaskini.


Hii ni PR mbaya sana .Ziara za Obama,Bush,Clinton au Shinawatra nchini haziwezi kupewa heading kama hii.

Kwani toka lini Tz in PR nzuri
 
shehe ponda alikuwa huko siku chache zilizopita kabla ya tukio.
 
hili la watoto wa london litatupeleka pabaya!muingereza kwa kukuza maneno hajambo!

Ni kweli bwana. Waingereza ni noma sana. Hawana dogo. Halafu na mataifa mengine wanawasikiliza sana. Kwa kweli hii itatuathiri. Something must be done.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Good, vyombo vya habari vya nje vitaanza kuelezea maovu ya CCM na serikali yake
 
Naapa rasmi hapa jf leo , sitoenda tena Zanzibar katika kipindi hiki kifupi nilichobakiwa nacho hapa duniani , afadhali Hata KABUL .

Sijawahi kufika huko ingawa nilikuwa napanga niende huko. Sasa ni basi tena. I cannot risk.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Zanzibar sio sehemu salama kama wewe sio Mwislamu, kuna watu wamejazwa ujinga kuwa Zanzibar ni ya waislam pekee kana kwamba wao hawaendi nchi za wenzao.!!
 
zanzibar ni mkoa wetu tu hawana lolote,ila wasiwasi wangu sio ndani ya zanzibar inawezekana hizi kampeni zinafanywa toka nchi za jirani yaani rwanda na kenya,kenya wanawivu sana na sisi mana kwenye balozi zao zote ulaya wametangaza tanzania kuna mabomu na magaidi hivyo watalii wasije na inawezekana pia hata haya matukio ya arusha asili yake ni kenya pia ili kutarnish our image,kuhusu rwanda,amini usiamini kuna uhusiano wa chini kwa chini kati ya rwanda na wapemba na aadhi ya waunguja,wanaagenda ya siri sijui ni ipi kwa upande wa wapemba watanufaika ila kwa sisi tuliokaa sana uganda tunajua hayo ingawa serkali inaweza isijue.inawezekana ni mkono wa rwanda pia kuchochea hao wapemba ili kuiharibia sifa tz iliyoipata hivi karibuni,yote yanaweza yakawa yanaukweli ndani yake inaweza ikawa ni kinyume kabisa nasuggestion mbili nilizozitoa,ila kuhusu waznzbr kama wenyewe kujiorganize hivyo siamini,lazima kuna mkono wa mbai hapo na kama waliofanya hivyo hawana msaada wowote hawatafika mbali bali watakamatwa tu hivi karibuni.
 
hili la watoto wa london litatupeleka pabaya!muingereza kwa kukuza maneno hajambo!

Hili ndilo tatizo letu kubwa Watanzania - tunaona ni jambo dogo! Kwa wenzetu kila uhai wa mtu unathaminiwa. Hakuna kifo au tukio la kumtdhuru mtu linalochukuliwa kirahisi. Mauaji au ujambazi kama huo utachunguzwa ili kuahakikisha chanzo au wahusika wanapelekwa mbele ya sheria. Kwa mtazomo wako na wetu wote, na hususan wa watawala wetu kuuwawa kwa padri huko Zanzibar au kumwagiwa tindikali Shehe mmoja huko huko Zanzibar ni jambo dogo - hatupendi kukuza maneno! Kutekwa na kuteswa kwa Dr Uli na Kibanda ni jambo dogo sana - hatutaki kukuza maneno! Kumwagiwa tindikali yule mkurugenzi wa sijui Home Center ni jambo dogo - upepo utapita! Kumwagiwa tindikali yule kijana wa Igunga 0 jambo dogo lakini tualitumia kama mtajai wa kisiasa na upepo utapita!!! Hiii ndio worldview yetu finyu (watawala na watawaliwa) na ndio imetufikisha hapa. Tukio lilanalohusu uhai wa binadamu lazima 'likuzwe', lipigiwe kelele to the highest volume ili lisitokee tena kwa binadamu mwingine. Hiyo ndio worldview ya wenzetu and it works perfectly katika masuala ya haki na uwajibikaji.
 
Dkt Shein afanye maamuzi mazito kama alivofanya Jk. Timua wahamiaji "haramu" wote. Watanganyika must go.
 
Back
Top Bottom