Liyumba afungwa miaka 2 jela

Liyumba afungwa miaka 2 jela

Hilo ni changa la macho liveeeeeeeee, miaka miwili? Jamani tusiwe wajinga huyu bwana ana hela chafu, na huko jela atakuwa anaishi kama mfalme tu, kwa wale wanaojua jela ukiwa na hela unakuwa kama uko likizo bila malipo, unaweza ukala chochote cha uraiani hata bagger au pizza, wale jamaa sio malaika nao wana maisha tight ukaiwaachia posho kama kawa gambe na mlupo unaletewa, halafu miaka miwili usiku na mchana jela ni mwaka. Halafu kama kakutwa na kosa hela za walipa kodi tutazipataje? akienda jela bila kumfilisi sio kitu, atavumilia huko kisha akitoka anakula bata kama kawa. Huu ni usanii mtupu bwana na Liumba anaweza hata asikate rufani maana anajua yuko likizo bila malipo na akitoka kesho kutwa vimwana kama kawa.
 
Oh! masikini Liyumba, keshakula mvua 2!. Lazima akate rufaa!, ameonewa bure!, muhusika halisi alishatangulia mbele ya haki.
Pole Liyumba pole. Haki ya mtu kamwe haipotei, inaweza kucheleweshwa tuu!

Pamoja na kukosa uhuru, huduma muhimu kama 'conjugal visit' pia zinapatikana kwenye magereza yetu siku hizi.

Niliandika mahali.
Mode its high time kuziunganisha hizi thread za Liyumba, ziko nne (4) ukurasa mmoja!.
 
Yaani mimi kila nikiona Gazeti limeandika Liyumba na nunua sasa leo naenda kuyachoma yote!
 
Sheria imefuata mkondo wake....bado sasa MRAMBA, YONA, na nani tena yule???
 
Sheria za nchi hii kweli ni za kufikirika wala si za ukweli, huwezi amini mtu kuiba kuku wa tsh 5000 ndo afungwe miaka 3 ila Liyumba kala kama bilion 200 miaka miwili.Wanasheria hebu tusaidieni hapo jamani au behind ze scene? Pesa vipi? hajaamriwa kufilisiwa? Huu ni usanii live.:violin:
 
Watanzania hatujui tunataka nini...asingepatikana na hatia tungelalamiaka,amepatikana na hatia bado tunamuonea huruma...Miaka miwili nikichekesho!
 
Liyumba nenda jela, nenda kaone WaTz wenzako wanavyoishi kule, jela ni nyumba ya wenye Haki na wasio na haki, ni nyumba ya wenye makosa na wasio na makosa, jela za Tz ni Nusu Jehanam, mahabusu nimeambiwa ulikula vyakula ulivyoandaliwa na wakezo na wale wengine, selo ni ngumu, kwa wiki tutakuja kukujulia hali mara moja , moja. Ila ukitoka naamini utaandika kitabu cha maisha yako ukitueleza ukweli woote unao ujua katika sakata hili, maana wapo waliosema mligongana pahala na Mwajiri Mkuu wa Serikali, Mbayuwayu wetu aka Vasco.
 
Haya matumizi mabaya ya ofisi ni nini? Au alijinufaisha kwa kutumia ofisi!
Angalia kifungu cha 31 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, 2007, Na. 11/2007:
"31. Any person who intentionally abuses his position in the
performance or failure to perform an act, in violation of law, in the
discharge of his functions or use of position for the purpose of
obtaining an undue advantage for himself or for another person or
entity, commits an offence and shall be liable on conviction to a fine
not exceeding five million shillings or to imprisonment for a term not
exceeding three years or to both.
"
 
miaka miwili ni nini sasa heri angeachiwa huru
 
Miaka 2 minus mda aliokaa selo tayari=0

Hahaaaa< hii kali kuliko zote>>>> this is Tanzania jamani, japo na yeye si mhusika mkuu pamoja na kuwa ana maovu yake. Kwa kweli iko siku watu watashika viboko na kutuchapa wote, maana tunasema weee, lakini hakuna vitendo ndio maana tunadharauliwa, watu wanajiandikisha kupiga kura wapate vitambulisho vya kwenda benki na kwengineko na si kupiga kura na hii tutaona idadi ni kubwa lkn watakaopiga hawafiki nusu. Watu watapeta na mwisho wa yote, Chenge anarudi na genge lake wote
 
Nchi hii hamuijui? Wezi wote wanajulikana kwenye vyombo vya dola. Kuanzia wahindi wanaohujumu uchumi wa nchi, wanasiasa wezi wa mali ya umma, wauza unga, matapeli wa kimataifa mpaka majambazi ya kutumia silaha! Wote wanajulikana, ila hawafikishwi kwenye vyombo vya sheria, na wakifikishwa pesa zao zinawatosha kushinda kesi.

Take my words, nchi hii ukiwa na pesa, hata kama ni za wizi hufungwi. Huyu Liyumba kafungwa kama kiini macho tu!
 
lazima kate rufaa tu.
mtu kaiba mijihela ya kufa mtu halafu anahukumiwa miaka miwili?! hata kama ni matumizi mabaya ya ofisi basi angefungwa walau hata 5.
kuna jamaa yangu alishikwa kaiba kuku hakimu siku ya hukumu hakimu akaomba kuku aliyeibiwa then akahesabu manyoya ya mkian na ndo ikawa hukumu. kulikuwa na manyoya 17 na ndo ikawa hukumy yake
tanzania hii bana
 
Hahahahahahah jamani ubadhilifu wa Ma bilioni ya pesa unafungwa 2yrs, ngoja na mie nikaibeeeeeeeeeeee
 
kama adhabu ya kuiba MILLION MIA MBILI NI miezi 24 tu HATA MIMI NITACHAGUA KWENDA JELA MIAKA MIWILI ILI NTOKE NITESE MPAKA MWISHO WA MAISHA YANGU YOTE. Hivi kweli adhabu hii ni FUNDISHO KWA WENYE TABIA KAMA YAKE??? wewe m2mishi unaejifanya ni mrithi wa Nyerere Liyumba akitoka jiandae kumwagiwa tope na lile RANGE ROVER yake wakati unakimbilia daladala.

" Law is a commandment of Superiors to Inferiors" Professor Austin kama unabisha pokea rushwa ya elfu 50 halafu Takukuru wakuibukie uta prove that Quotation.
 
Back
Top Bottom