Nucky Thompson
JF-Expert Member
- Sep 20, 2016
- 2,194
- 4,802
Tunaweza kusena Rais au Serikali huwa hazifungi watu, ila bila msukumo kutoka kwa Rais au Serikali take basi basi mafisadi hawawezi kufungwa,
Rais huwa ndio anateua DCI, DPP, ambao ndio hukusanya ushahidi, kuandaa mashahidi, na kufungua kesi ni watu instrumental kwa mhalifu kufungwa au kutofungwa.
Rais pia anaweza kuagiza kitu fulani kipelelezwe ama kiachwe
Sikuwahi kusikia Magufuli au serikali yake ikiwafungulia mashataka wakurugenzi wa halmashauri ambao kwenye ripoti za CAG ni maarufu kwa hati chafu na upigaji au hata wa mashirika ya umma kwa ufisadi, au kwa sababu walikuwa ni wanaCCM na Magufuli aliwapenda sana wanaCCM na kuwachukia wapinzani ambao kwa kipindi chake wengi walisota jela, kupigwa risasi, kutekwa na kuuawa.....
Turudi kwenye habari
KIGOMA — MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kigoma imewahukumu kifungo miaka 22 jela watumishi wanne wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa manispaa hiyo, Athuman Msabila baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya kughushi nyaraka na utakatishaji wa fedha.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mkoa, Misana Majula katika kesi ya jinai namba 5546 ya mwaka 2024 iliyowakabili watumishi 11 wa serikali, wakiwemo maofisa kutoka idara ya fedha ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
Kwa mujibu wa hukumu hiyo, Msabila pamoja na Ofisa Uchumi wa manispaa hiyo Ferdinand Filimbi, Kaimu Mweka Hazina Salum Juma na Frank Nguvumali wamehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela kwa kosa la kughushi nyaraka.
Aidha, Msabila na Juma wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la utakatishaji fedha baada ya kutiwa hatiani kwa kuhusika kutaka kujipatia fedha isivyo halali kiasi cha Sh milioni 463.5.
#HabarileoUPDATES
Rais huwa ndio anateua DCI, DPP, ambao ndio hukusanya ushahidi, kuandaa mashahidi, na kufungua kesi ni watu instrumental kwa mhalifu kufungwa au kutofungwa.
Rais pia anaweza kuagiza kitu fulani kipelelezwe ama kiachwe
Sikuwahi kusikia Magufuli au serikali yake ikiwafungulia mashataka wakurugenzi wa halmashauri ambao kwenye ripoti za CAG ni maarufu kwa hati chafu na upigaji au hata wa mashirika ya umma kwa ufisadi, au kwa sababu walikuwa ni wanaCCM na Magufuli aliwapenda sana wanaCCM na kuwachukia wapinzani ambao kwa kipindi chake wengi walisota jela, kupigwa risasi, kutekwa na kuuawa.....
Turudi kwenye habari
KIGOMA — MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kigoma imewahukumu kifungo miaka 22 jela watumishi wanne wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa manispaa hiyo, Athuman Msabila baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya kughushi nyaraka na utakatishaji wa fedha.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mkoa, Misana Majula katika kesi ya jinai namba 5546 ya mwaka 2024 iliyowakabili watumishi 11 wa serikali, wakiwemo maofisa kutoka idara ya fedha ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
Kwa mujibu wa hukumu hiyo, Msabila pamoja na Ofisa Uchumi wa manispaa hiyo Ferdinand Filimbi, Kaimu Mweka Hazina Salum Juma na Frank Nguvumali wamehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela kwa kosa la kughushi nyaraka.
Aidha, Msabila na Juma wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la utakatishaji fedha baada ya kutiwa hatiani kwa kuhusika kutaka kujipatia fedha isivyo halali kiasi cha Sh milioni 463.5.
#HabarileoUPDATES