Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Kwa mujibu wa gazeti la the sun, wakinukuliwa na goal.com, club ya Al ittihad ya Saudia Arabia wameongeza dau toka 150mls mpaka 215mls ili kumpata egipytian king Mo salah. Hili dau ni kubwa jamani kwa mchezaji aliyetumika na club kwa zaidi ya misimu 6. Liverpool wachukue hii hela.

Mambo ya sijui mbadala wake, hayana maana kwa kiasi hicho cha fedha. Real Madrid walimuuza CR7 kwenda Juve kwa 100mls akiwa na miaka 32 kama sio 31. Salah kwa sasa ana 31. Club imuuze wapate hiyo pesa tutanunua mbadala wake january.
 
Kwani amewahi kuwa na akili yule? [emoji23][emoji23][emoji23]
Muache atapetape
Debe tupu haliachi kutita.


Cha muhimu ameondoka,
Hapa nasubiri Bobby aje tukajipongeze kwa kumg'oa Babu Hendo.
 
Hayana maana kwenu
Nyie msituponze


Hizo hela wangeleta mapema.
Sasahivi hatutaki. Salah ni muhimu kuliko hizo pesa.
 
Dirisha la January tu tunanunua mbadala na beki chenchi ikibaki tunaenda kenywa soda kwa Mangi.
 
Utashinda mechi ila sio makombe with like of Gakpo infront
 
Kumchezesha Gakpo as RCM ilimlazimu Klopp mechi zile mbili. Na unaona vs Newcastle Gakpo alicheza as CF.
Mwenzako Halaand as CF, wewe unamchezesha Gakpo as CF, huwezi ambulia chochote, ndio maana klopp kashtuka hamchezeshi tena CF
 
Ukiangalia Macaptain Wakubwa wote wa Liverpool FC mpaka kufikia Gerrard hakuna aliyeachwa kwa kutaliwa na Timu isipokuwa Henderson tena akiwa kwenye Umri ambao wenzake walikuwa wanacheza kikosi cha kwanza.

Hii inaonesha wazi kuwa kuwa ndiye Captain dhaifu kuliko wote ndiyomana sasahivi analialia mitandaoni anatafuta huruma huko.
 
Anyway utofauti wa mawazo haupingiki.
Lakini mkuu kuwa serious Elliot for Salah?? Doak for Salah?? Its not about kuaminiwa its all about consistency.
Consistency si inaanza kwa kuaminiwa mkuu!!! Ni hivi Klopp ana shida kwa kuwaamini vijana. Alimwamini TAA tu na mpaka sasa amekuwa regular stater wake.

Embu angalia kitu Xavi anachofanya pale barcelona. Ana madogo kibao tu kaamua kuwaamini. Wanapiga mzigo balaa. Elliott ana uwezo mzuri tu. Hiki hapa chini ni kikosi cha barcelona kitakachocheza UCL msimu huu.
M
 
Sijawahi kumkubali huyu mbaguzi
 

Barcelona wamelazimishwa na uchumi mkuu plus marungu ya kufungiwa usajili mara kadhaa. Good for them imework out kwa makombe ya ndani ila huko nje umeona wanavyo struggle kumatch with the quality iliyopo.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…