Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Khee mpya hii sijasikia mkuu ..imekuaje Tena, Ina maana UEFA mashindano ndo basi Tena? Hiyo USL inatofauti gani na UEFA?
 
Mkuu em nieleweshe kuhusu hii USL sijaelewa ni ligi mpya au ni nini? Na inaanza msimu upi kufanya kazi? Ina maana UEFA ndo basi Tena au?!
 
Khee mpya hii sijasikia mkuu ..imekuaje Tena, Ina maana UEFA mashindano ndo basi Tena? Hiyo USL inatofauti gani na UEFA?
Kumbe muda wote unapayuka humu hujui kinachoendelea ...[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Kweli wewe umekula cha arusha mkuu
 
mkuu hii format ya sasa haiwatendei haki wakongwe, wenye ucl yao (barça,madrid, liver,utd,bayern, juve, ac) hawa wanataka kila mwaka wawe wanashiriki hii michuano maana wao ndio wenye majina na waingiza pesa!


na pia wanataka share kubwa ya faida wawe wanapata wao kwa sababu wao ndio vivutio,......... ni kama big six (actually ni pool na utd) pale epl wanavotaka kupata share kubwa ya faida bila kujali perfomance yao msimu husika ikoje.....


vyovyote iwavyo, wakongwe watashida hii vita, ndio mana ukifuatilia mwanzoni walikua wanataka timu zenye historia ya CL zipewe upendeleo wa kushiriki kila mwaka (hapa mpk ajax alikua included)


kwangu naona wako sahihi, haiwezekani AC Milan acheze europa huku spurs au city akicheza CL na kufaidi pesa zote wakati CL wakiosaidia kui-brand ni MILAN
 
Ndomana namtilia mashaka akisha kariri team ndo basi tena mpaka waliopo benchi wanaondokewa na hali ya kimchezo.
Ikitokea bahati kapangwa inakua kama mtu mpya kwenye team.

Naamini team bado ni nzuri mwalimu ndo kashindwa
 
Ndomana namtilia mashaka akisha kariri team ndo basi tena mpaka waliopo benchi wanaondokewa na hali ya kimchezo.
Ikitokea bahati kapangwa inakua kama mtu mpya kwenye team.

Naamini team bado ni nzuri mwalimu ndo kashindwa
Klopp ni tatizo kubwa sana Liverpool. Hajazoea hii nafasi alipo sasa. Ni kama amechanganyikiwa aisee. Hivi kweli unatafuta ushindi unamtoa Mane na kuleta joker Ox nk like serious.

YNWA
 
Mkuu hakuna mwenye shinda ha hilo mbali la ukubwa wao ila sasa kushiriki UCL isiwe hisani you have to earn its man on the field and not otherwise.

Je wajua Big 6 ya miaka ya zamani before 80s sio hawa wa sasa. Who knows may be Big 6 ya 2040 itakua again Wolverhampton, Burnley, Aston Villa nk.

Muda mchache mambo ni mengi.

YNWA
 
Hapo kwa Milan hapana, team kama haiwezi pambana uwanjan kwa nini itafutiwe upendeleo,

Leo hii game ya man city dhid ya salzburg inaweza ikawa na mashabiki wengi kwenye viewing tofauti na game ya ac milan vs lille

Team zinabidi zioneshe ukubwa wao uwanjani na sikupitia historia

Imagine team kama leic leo labda inachukua pl je wanaenda wapi baada ya hapo,

Kutakuwa hakuna maana ya league na hiz cup maana hata uchukue league or umalize ndani ya top 4 hauqualify kwenda popote
Maana nzima ya league inakuwa ishapotea
Lep hii watu wanainvest ili wachukue league n wafudhu ucl ili kuwashawishi player kujoin
 
Mkuu em nieleweshe kuhusu hii USL sijaelewa ni ligi mpya au ni nini? Na inaanza msimu upi kufanya kazi? Ina maana UEFA ndo basi Tena au?!
Mkuu hii ni ESL kirefu chake ni European Super League sio USL.

Ki ufupi ni kwamba hawa wanaofahamika kama timu kubwa katika nchi 3 za Italy, Spain, England wamekaa na kukumbaliana waanzishe ligi hio yenye timu 20 ambazo timu 15 zitakua zipo permanently yaani hawa ni waanzilishi hawakosi kushiriki hata kama kwenye ligi za nyumbani watamaliza nafasi ya 12. Hizo timu zingine 5 bado hawajatoa maelezo zitapatikana vipi.

Hii ESL inamilikiwa na wenye timu na wanasimamia wenyewe tofauti na ya sasa ambayo ipo chini ya Uefa.

Mwenyekiti wa kwanza ni Perez raisi wa Real Madrid.

Kingine ni kwamba watakua hawashiriki tena UCL.

Muda wa kuanza ni August 2021 kama watakua wamepata baraka za Fifa na UEFA ama 2022 kama watakua wamekwama kupata bara za hao.

YNWA
 
thats why wanataka ku-protect status quo,.......

in reality mechi zinazoingia pesa mingi CL ni zile za wakubwa tu na sio hawa kina atalanta sijui spurs sijui wofsburg n.k........ sasa inakuaje wao waingize pesa mingi halafu mgawo wapate sawa.? au wazidiwe kisa tu hawajafuzu hatua inayofuata.....?


ndio mana nakwambia watashinda hii vita coz they have power, ukitaka kuthibitisha hili just imagine EPL bila liver, utd, arsenal, Chelsea kama kuna mtu ataenda kibanda umiza kutazama, au kama kuna kampuni itaweka pesa zake bila hao miamba kuwepo........


au just imagine CL bila Liver, utd, juve, Ac, madrid, Barca kama kuna kampuni itaweka pesa zake, si itageuka europa nyingine tu hii........ thats why hawa vigogo hawawezi kuadhibiwa and they will get their way!


hata FIFA hawawezi kusema lolote zaidi ya hizi kelele wanazofanya, maana nani atawekeza pesa kwenye mashindano yao wakati wachezaji wakubwa wote hawashiriki? nani atataka kujihusisha nao wakati majina makubwa ya wachezaji yamekua banned.......?
 
bado hujaelewa mantiki ya SL, wao wanataka timu waanzilishi wasiondolewe kwenye mashindano (wanalinda brand walizojenga kwa miaka mingi sana),


sasa leo atokee mwarabu kainunua watford et ije imwondoe Utd kwenye status yake unadhan watafurahi?........


kimsingi hii ishu ilianza baada ya Chelsea kununuliwa na mrusi, na kuanza kusumbua wakubwa, sasa ameongezeka city na psg..... wakongwe wanahofia huu mtindo utaendelea maana FFP imeonekana kufeli
 
Nimeeilewa , hapo nilikujibu uliposema haiwezekani milan acheze ueropa wakat spurs na city zikicheza ucl
 
At least now we agree even them pundits agree Klopp effect has made us whats we are now and yets the Yankees think they are the movers in this club that they can video call and agree to change the usual stuff without even consulting the real owners of this clubs..

At least Klopp has said he will try to resolve this and he won't run away as many fan thoughts..

Kazi ipo.

YNWA
 
Mkuu nadhani hujapitia kwenye online papers tofauti za Majuu.

Ni hivi hakuna timu inayopingana na kuboresha ndugu wanachotaka ni ushirikiswaji kwa wadau wote kwa mfano Fifa, Uefa, EPL, FA, Uk Government, Ligue One, La Liga, Seria A, Players Association, Fans Representatives nk. Hizi pingamizi zote na kwa vile ipo UCL na hawa Big 12 wanasema ilivyo inapoteza mvuto na inafifia kwa kasi ya 4G hivyo wameuamua kuungani ili kuokoa jahazi in Perez Voice.

Sie tuwe na subira ndugu yetu macho maana wenye timu zao wapo hukooooo sie hapa ni burudani tu.

Ifahamike hawa Owners ni Custodian mbali wamiliki wenyewe ni mashabiki maana mwisho wa siku wao ndio hununua jersy, hulipa membership, hulipa viingilio nk sasa wenye timu zao wanasema chase the Yankees haha.

Ngoja tuone ndugu.

YNWA
 
Developing news.

Chelsea and Manchester City will leave the proposed Super League.

Sasa tusubiri real Yankees akina Woodward na Henry walivyo viburi naona limewakuta.

YNWA
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…