Don Clericuzio
JF-Expert Member
- Dec 8, 2017
- 16,930
- 40,591
Jones, Salah na Gini hawastahili lawama wanazopewa kwa Matokeo ya Jana.
Tatizo lako unadhani huwa hujawahi kukosea na hutakiwi kukosolewa.
Sasa kama tusome halafu tusijibu umemuandikia nani?
Umetaja wengi wakosoaji ila umejisahau wewe pia nasi tunakukumbusha.
Unajikutaga kama vile huu Uzi ni wako
Takataka
Tuna washambuliaji 3 hawawezi kulingana ufungaji tukitamni hivi itatokea utegaji mkubwa sana utakao tunyima ushindi.Nimehisi naweza kushare hii kitu.
Wakati tulipokuwa na Coutinho/Milner/Gini/Hendo nilikuwa mkosoaji Mkubwa wa Hendo kutokana na uchezaji wake mbovu wa wakati huo! Lakini from the last season mpaka sasahivi simkosoi tena Hendo na nimeridhika aanze kila Game, unadhani namkubali ni bonge la mchezaji? Hapana! Bali ni kuwa yupo Fiti wengine ni Wagonjwa wazoefu.
Lakini ukiangalia huu Uzi (Hasa baada ya Matokeo ya jana) utagundua haya.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda Gini tu haku akisia wengine.
- Kuna Washabikia kazi yao kumponda Firmino tu haku akisifia wengine.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda Salah tu huku akisifia wengine.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda Jones tu huku akisifia wengine.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda Hendo tu huku akisifia wengine.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda Keita (Hakucheza) huku akisifia wengine.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda OX tu akisifia wengine.
Sasa hapo angalia hizo tabia za Mashabiki wetu wa Liverpool utagundua Wachezaji wote wanapondwa ambapo kila Mtu anamponda mmoja au wawili kati ya hao.
Na vilevile wote hao Kila mmoja hapo utakuta kuna Mtu humu anamsifia mchezaji husika hivyo wote hao pia wanasifiwa.
Ukija kwa wapondaji hapo siku zote hawamlaumu mchezaji kulingana na takwimu kwani hawaamini katika takwimu kitu ambacho huwezi kuwa mchambuzi au muelewa wa mpira bila ya kuwajadili kulingana na Takwimu.
Unapokuwa Beki basi msingi wa kupimwa kwako ni takwimu za duels won, tackle won and intercept.
Unapokuwa Mshambuliaji basi msingi wako mkubwa wa Takwimu utapimwa kwa Goal score + Assist. Mshambuliaji hawezi kupimwa kwa kupiga chenga na kukimbiza mipira, kama ni hivyo tungelimnunua Adama Traore badala ya Diogo Jota.
Hivyo huwezi kusema mchezaji fulani hata asipofunga anahangaika uwanjani!!! Yeye ni mshambuliaji hii kuhangaika tunaipimaje? Ni Stats? Ni lazima afunge wakati yeye ni Mshambuliaji.
Na hii ndiyo inayomfanya Salah ataendelea kupata namba game after game labda awe majeruhi. Hii ni kwasababu Takwimu zake za Ufungaji na Assist zinajieleza. Kamwe Klopp hawezi kumuweka Benchi Salah kutokana na anachokifanya kwani points hazipatikani kwasababu fulani kahangaika bali zinapatikana kwasababu Fulani kafunga.
SULUHISHO:
Wanaowashambulia wachezaji wanashindwa kuleta Facts (Takwimu) za weakness zao bali wanaishia kulalamika tu hii inaonesha wazi kuwa hawajui wanalalamikia kitu gani bali ni Haters tu kwa baadhi ya Wachezaji zilizotokana na Makala za Mitandao wanayotembelea.
Jones, Salah na Gini hawastahili lawama wanazopewa kwa Matokeo ya Jana.
Binadamu tunatofautiana namna ya jinsi ya kutambua au kutafakari vitu.
Tunaweza wote tukawa tunaangalia kitu kimoja lakini tukaibuka na maoni tofauti.
Jones amechomesha jana, lakini chomesha yake haikuwa direct, kwa sababu choma yake ilizaa kona, timu kama timu tukishindwa kuikaba kona tukafungwa. Jones is still young, mistakes are part and parcel to learning.
Kabla ya hapo hatukutengeneza nafasi za magoli pamoja na kwamba mpira tulikuwa nao sisi kwa kipindi kirefu.
My biggest worry ni kwa front three yote, some days back nilikuwa na ugomvi na Bobby, Jota kamchangamsha changamsha tukaona amerudi kidogo, Jota kaumia sasa, hapo naona kama tumerudi nyuma Tena.
Tuna washambuliaji 3 hawawezi kulingana ufungaji tukitamni hivi itatokea utegaji mkubwa sana utakao tunyima ushindi.
Mfano jana angalia eneo alocheza sana Mane kipindi cha kwanza ni kati namtazama kama vile mtu anaesema tubanane apapa kama kukosa tukose ila na mimi ni funge labda kama nimemtazama vibaya ila kama washambuliaji wata anza kukabana na mido zetu zilivyo tutakwama naamini matokeo mabovu kwenye hizi team za chini sababu ni kutegeana nimewaza tu
Ila nao mkuu hawapati matokeo mazuri!Ki ukweli Manchester United, Manchester City au Chelsea wakishindwa kulichukua kombe hili kipindi hiki tunapata matokeo ya hivi basi nao wajitazame upya...
YNWA
Ila hii ilikuwa faulo mbaya kabisa basi tu kwa watu wana mikakati yao!
Tatizo lako unadhani huwa hujawahi kukosea na hutakiwi kukosolewa.
Sasa kama tusome halafu tusijibu umemuandikia nani?
Umetaja wengi wakosoaji ila umejisahau wewe pia nasi tunakukumbusha.
Unajikutaga kama vile huu Uzi ni wako
Takataka
Ila hii ilikuwa faulo mbaya kabisa basi tu kwa watu wana mikakati yao!
Sidhani kama mimi nimetofautiana mtazamo wa kpira na wewe ila nahisi tumetofautiana uwasilishaji wa maoni.
Sitaki niwatupie lawama hao as a scapegoats tu na sio kwamba hawakufanya makosa in general.
Jana makosa yalikuwa kwa Front 3 yote kwani haijafanya serious attack yoyote coz hata lile goli la MANE walikuwa wanazurura tu mpaka uliona kuwa ni mpira mrefu uliopigwa kwa ufundi mkubwa na Mchezaji ninayemkubali kupita maelezo Jo Matip, sio Fair kumtupia Zigo Salah as Salah kama wengine walivyo mpoint.
Ukiangalia kwenye Mido Hendo na Gini ndani ya Dakika 90 basi sijaona cha mana walichokifanya zaidi ya kurandaranda tu, so, kumpoint Jones peke yake kwasababu tu kosa lake la kimpira lilizaa goli hapo Dogo tunamuonea.
Hivyo ni Timu nzima ukitoa Mabeki wote 4 na kipa basi imecheza Vibaya na ndiyomana lawama zinabidi ziende kwa wote na si kwa Jones, Salah na Gini.
Kazi kweli kweli! Yaani Klopp anatakiwa ajue kuwa tunacheza na timu na VAR. Karefa kameangalia tu mtu anadandiwa mgongoni kabisa?Tungelifunga sisi lile goli basi Refa angeenda kuangalia VAR ikisha angelikataa goli.
Kwahiyo wewe ulivyonijibu ni nini kama sio dharau kwamba wengine hatuna akili?Yani ningeliona hili neno "Takataka" tokea awali basi nisingelikujibu katika Post zangu za awali kwani umenivunjia heshima kwa kiasi kikubwa coz mimi sipo katika Kundi la kutupiana maneno ya kijinga.
Hii ndiyo itakuwa Post yangu ya mwisho kukuquote.
Kila la kheri
Ndio nimeona nami nilikuwa namkumbusha tu kama alivyotukumbusha yeye hapo..Happy birthday bosi.
Kama ukisoma vizuri, utagundua kwamba umerudia alichokiandika, amekubali kwamba alikuwa anamponda Hendo, na kadri Hendo alivyobadilika (kidogo) na yeye kaacha kumponda.
Jaribu kusoma upya alichokiandika.
Manchester City vs Everton imeahirishwa sababu ya Covid..
Baadhi ya wachezaji wa Manchester City wamaedhirika na baadhi staff wao...
YNWA
Wachezaji kama watano na staff lol balaa....Walienda Disco la Siku kuu hawa
Pazuri January 2021 anaodoka huyu akasake kwingine maisha...Misimu iliyopita ilikuwa Origi hata umuingize dakika 5 za mwisho Impact yake ilikuwa Mpinzani maji anaita mma.
Lakini sasahivi kufanya Sub ukamuingiza Origi Basi unatamani angetoka mtu na asiingie yeyote. Jamaa kachuja hafai hata kuugusa mpira basi anatimiza dakika 5 hajaugusa.
Bobby ana misumari ya kiafrika Yani.