Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Huyu jamaa sijamuelewa kabisa. Mchezaji kupata red card ni sehemu ya mchezo. Hakuna cha kusema wangekuwa wamekamilika. Kwani hakuna timu zinazokuwaga pungufu na kushinda? Acha bana habari zako za kishamba...mtu kacheza utumbo afu unataka aachwe.....hyo haipo vijana walicheza tena vizuri sana. Ile move ya Mane asongekamatwa na Cristensen alikuwa anaweka kamba. Sasa unasemaje timu foward yake ni butu?
 
Wewe Bengalisis na huyo mwenzako Octa_dre96 wote mmekaza vichwa, ushabiki umewajaa mnaropoka tu!

Jamaa Econometrician hajasema kama ile red card sio halali, ile ni straight hakuna anaipinga..

Lakini kama isingetokea ile ajali, ile game ingekuwa ngumu kwenu. Ukiangalia kabla ya Chelsea kupata umeme, ile game ilishaanza kuwa tight kwa timu zote 2.

Tukiweka ushabiki pembeni kipindi cha kwanza nawapa credit Chelsea, walicheza vizuri.. Mashambulizi yao yalikuwa ni hatari zaidi.
Hata kwenye ukuta wao Chelsea wakina Zouma waliweza kumzuia vizuri yule mwarabu wenu.

Kwenye back four yenu bado hakujakaa sawa.. Pamoja na kumrudisha chini Fabinho sijaona kama ile namba itamfaa msimu mzima.

Huyo Fabinho mwenyewe alivyokuwa nyonde nyonde vile tukisema zipigwe zile counter attack kutoka kwa timu pinzani halafu abakie yeye na straika kama Vardy au Auba tunahesabu chuma tu!

Kuna attempt moja aliifanya Timo Werner kwenye 1st half, nje ya dimba.. Alimgongesha mpira Fabinho usoni, ukamrudia tena akasogea akapiga ikaenda nje.
Nikiiangalia ile najisemea tu mwenyewe hawa Liverpool wakiendelea kumpanga huyu Fabinho kwenye position ile, sina shaka na yeye ataanza kuwa wakala wa assist kama mwenzake VVD.

Its just matter of time![emoji16]
 
Wishful thoughts...
 
Asingemshika lilikua bao lile
 
Wewe ni mshabiki wa timu gani pale England
 
Kunywa maji mkuu
 
Mpira haupo hivyo huenda tungewapiga nyingi tu ile kadi imewaongezea umakini

Lile ilikua la kwanza wangefunguka ili wasawazishe tungetengeneza nafasi zaidi ya ile
 
Alcantara alipo ulizwa na waandishi wa habari kwamba kwann hajaigusa Nembo ya THIS IS ANFIELD wakati ana tambulishwa kama mchezaji wa Liverpool alisema kwamba👇

" Fernando Torres alinambia nisiiguse nembo ya THIS IS ANFIELD kabla sijaipatia timu kitu chochote bora ,nilimsikiliza ni niliheshimu pia maana hii ni kama utamaduni wa klabu na Mimi na paswa kuheshimu hili, na nita hakikisha najituma na kushinda mataji ili nifanikiwe kuishika nembo ambayo ina maana kubwa kama mchezaji wa Liverpool ".

👉 Zamani kabla ya ujio wa Jurgen Klopp ndani ya Liverpool kila mchezaji alikuwa ana uwezo wa kuigusa nembo ya THIS IS ANFIELD lakini baada ya ujio wake aliondoa hio desturi na kuweka sheria nyingine kwamba ili mchezaji aweze kuigusa nembo hio lazima ahakikishe ameipatia timu taji la aina yoyote ile, Hivyo Torres ameamua kumshauri Thiago kwenda sambamba na kanuni alio iweka Klopp kama wenzie walivyo Fanya na Thiago mwenyewe amesema hakuna kabaya.
#Ynwa
 

Kwenye Mpira hakuna Kitu 'Ingekuwa'.
Kashabikie Rede huko.
 
Ulichokinena ni sahihi, ukitathimini mechi hizi mbili za ligi utagundua timu bado haipo vizuri,tunacheza slow sana, back passess ni nyingi na hakuna mashambulizi ya kueleweka katika lango la wapinzani, Kiufupi magoli na ushindi wetu umekuwa kama wa bahati.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…