Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

EMBU MUACHENI KAPTENJ WETU CHUKI ZENU PELEKENI HUKO HUKO. KAMA HUNA CHETI CHA UKOCHA KINACHOFANANA NA KLOOP USIPIGE KELELE KUHUSU KAPTENI JORDAN MAANA YEYE ANAJUA NI BORA NA NDIO MAANA ANAANZA KWENYE KIKOSI CHAKE...NA ALIPOGONGWA MGUUNI ILE MECHI YA BARCA HOME KLOOP ALING'ATA MENO KUONYESHA UOGA WAKE KAMA JAMAA AKITOKA ITAKUAJE....NI KAPTENI NA MCHEZAJI BORA.....LA CAPITANO

Sent using Jamii Forums mobile app
Whistling
 
Hivi bill shankly alipomkabidhi timu Bob paisley , alimkabidhi kama assistant wake au Bob paisley kuna timu alikuwa anafundisha ndio akapewa liverpool?

Na vip kuhusu Joe (Joseph) Fagan
Unajua Shankly alistukuza sana kustaafu kwake mwaka 1974 na klabu haikua na plan B ya hapo kwa hapo na kwa vile tangu Shakily anateuliwa kua kocha wa Liverpool mwaka 1959 alimteua Paisley kama msaidizi wake basi uongozi ukaona kumpa hio kazi mwaka 1974 itakua ni mwedelezo Wa yale mazuri aliyokua anafanya Shankly...

Shankly alimkuta Paisley Liverpool akiwemo na Fagan na hapo hapo wakaanza kazi maridadi kabisa kujenga kikosi..

Bob Paisley alikua pia ni daktari Wa viungo pale Liverpool kazi yake ya kwanza baada ya kustaafu soka, inasemekana Kwa kuangalia tu mchezaji bila hata kupima aliweza kujua nini kinamsubua. Kazi hii hakwenda chuo mbali alijifundisha mwenyewe.

Bob Paisley alijiunga Liverpool mwaka 1939 na alikuja kustaafu mwaka 1983. Aliitumikia Liverpool miaka 44. Alishinda mataji 20 ndani ya misimu 9 aliyodumu kama meneja.
Alikua ni real scouser mzaliwa Wa jiji la Liverpool, alifariki mwaka 1992.

Joseph Francis Fagan alijiunga na Liverpool mwaka 1958 kama kocha wa reserve team kazi aliyoifanya mpaka mwaka 1971, baada ya hapo alifanya kazi na kikosi cha kwanza mpaka 1974 alivyopandishwa rasmi kua kocha msaidizi Wa Bob Paisley.

Baada ya Bob Paisley kustaafu mwaka 1983 klabu iliona itumie mbinu ile ile ya kuedeleza aliyoifanya Paisley na wakampa kazi hio Joe Fagan.

Msimu wake Wa kwanza alishinda vikombe viatu League Championship, League Cup na European Cup.

Alistaafu mwaka 1985 japo alipanga kustaafu mwaka 1984 na hakushinda taji lolote msimu wake Wa mwisho ikiwa ni mara ya kwanza kwa Liverpool kutoshinda chochote ndani ya miaka 10. Baada ya Fagan klabu ikamteua kocha mchezaji King Kenny Dalglish mwaka 1985.

Tukio ambalo lilipelekea akumbwe na msongo Wa mawazo ni ile Fainali ya Ulaya kati ya Liverpool vs Juventus iliyochezwa uwanja Wa Heysel Ubelgiji na ikatokea ajali ukuta kuangukia mashabiki wengi wakiwa ni Wa Juventus. Baada ya ile ajali mechi ilichezwa na Juventus wakashinda moja bila goli akifunga Platini Kwa penati. Hili Tukio lilipelekea Liverpool kufungiwa kushiriki mashindano ya Uefa Kwa takribani miaka 6 na vilabu vingine Kwa Uingereza miaka 5.

Joe Fagan alikua ni scouser pia mzaliwa Wa Liverpool, aliitumikia Liverpool Kwa miaka 27. Alifariki mwaka 2001.
 
you're right.... technically Keita is miles ahead of Hendo if he (Keita) can stay fit - and staying fit has been Keita's major downside.

sasa imagine if Klopp were only to rely wholly on Keita, nini kingetokea bila ya kuwa na wagumu kama kina Milner/Hendo/Gini?

for us LFC fans, the end should justify the means. happy with the trophies regardless of which player was better than the other.
sisi ni familia moja...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
below is an excerpt from Jurgen Klopp's Christmas message to the LFC fans.
what a great man!

20191226_114047.jpg
20191226_114146.jpg
 
Hivi kwa nn leo Liverpool anaanza mech Round ya pili? wakati round ya kwanza haijaisha!
Liverpool amecheza mechi 17 na anakipolo kimoja= mechi 18 jumla. Cha kushangaza leo ni mechi ya round pili. Round ya kwanza mechi 19 na Round ya pili ni mech 19.

Jumla mechi 38.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nadhan ni timu zote, sijui kwann.....
Hivi kwa nn leo Liverpool anaanza mech Round ya pili? wakati round ya kwanza haijaisha!
Liverpool amecheza mechi 17 na anakipolo kimoja= mechi 18 jumla. Cha kushangaza leo ni mechi ya round pili. Round ya kwanza mechi 19 na Round ya pili ni mech 19.

Jumla mechi 38.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa anashambuliwa nanyi mashabiki kwa kosa gani?
Unadhani Jorgen anawapuuza mashabiki pasipo sbb za msingi?
Hendo anapigiwa *poooow"?
Mi mswahili ninakamilisha kwa kusema,"Hendo Hana nyota ya kupendwa" lakini ni Capt atakaebeba vikombe vinne ambavyo haijawahi kutokea kwa nahodha yeyote wa Liverpool.
He will prove all of you wrong! Na jina lake litaandikwa"This is Anfield- Congrats Our Skipper Hendo"
 
Kila binadamu anayemdharau binadamu mwenziye kwa Mambo untouchable Hana maarifa. Ujue Kila binadamu anazo akili. Mwaka wa 3 Hendo ni Capt. Na 85+% ameanza kucheza unless awe na injuries. Sasa mjinga mie au Jorgen Klop na benc lake?
Because football is a lunatic favourate game and watched by 90% hooligans it might be mostly we are laying on that side.


Halafu tajiri Watery akisema humu kuna watu hawana akili tunambishia.

Ukute anamaanisha watu kama hao.
 
Hivi kwa nn leo Liverpool anaanza mech Round ya pili? wakati round ya kwanza haijaisha!
Liverpool amecheza mechi 17 na anakipolo kimoja= mechi 18 jumla. Cha kushangaza leo ni mechi ya round pili. Round ya kwanza mechi 19 na Round ya pili ni mech 19.

Jumla mechi 38.

Sent using Jamii Forums mobile app
hii nitokea msimu uliopita nakumbuka vizur sana, sijui ndio utaratibu wao sifahamu, wajuz tunaomba ufafanuzi hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa anashambuliwa nanyi mashabiki kwa kosa gani?
Unadhani Jorgen anawapuuza mashabiki pasipo sbb za msingi?
Hendo anapigiwa *poooow"?
Mi mswahili ninakamilisha kwa kusema,"Hendo Hana nyota ya kupendwa" lakini ni Capt atakaebeba vikombe vinne ambavyo haijawahi kutokea kwa nahodha yeyote wa Liverpool.
He will prove all of you wrong! Na jina lake litaandikwa"This is Anfield- Congrats Our Skipper Hendo"

Hivyo Vikombe 4 atabeba peke yake? Au umemaanisha nini? Still the same nonsense
 
Hivi kwa nn leo Liverpool anaanza mech Round ya pili? wakati round ya kwanza haijaisha!
Liverpool amecheza mechi 17 na anakipolo kimoja= mechi 18 jumla. Cha kushangaza leo ni mechi ya round pili. Round ya kwanza mechi 19 na Round ya pili ni mech 19.

Jumla mechi 38.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu umeanza kuangalia EPL msimu huu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom