Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Kwa brewster sitokupinga maana jana hajacheza mpira tuliouzoea toka kwake lkn kwa jones mkuu hapo nakupinga mbona kacheza mpira mzuri tu,sema kuna baadhi ya move alikuwa anatakiwa awe anatumia nguvu nying .
 
View attachment 1216155
Kama kawaida Man City yy team kubwa zinamkuta kombe uwanjani
FA inanuka rushwa
Acheni mawazo mgando nyie majogoo mbona mnaanza kuogopa mapema arsenal anawapa wenge eeh


Hivi southumptom ni timu ya kubeza kweli?

Et rushwa, man city?

Hata uefa angalia group lake? Na huko katoa rushwa?

Chezen mpira majogoo, mkianza kilia lia mnatuboa sanaa
 
Kwani waliolia ni wangapi
Ama kwa mawazo yako unafikiri anatuwakilisha sote
 
Mimi sijaangalia Mpira lakini mbona Ratings na comments za Wadau kwenye Platforms mbalimbali zinatofautiana na uliyoyaandika kuhusu Jones?
Wamemsifu sana kuwa ana kipaji
Achana na media comments za kiingereza nakuhakikisha brother Jones ni mchezaji wa kawaida sana na hana future yoyote ni aina ya wachezaji wa kiingereza ambao technically hawana uwezo
 
🆒🆒🆒🆒🆒🆒💯💯💯% true...Reds achievement and this lads individual honnours should motivate us in life that with the right effort anything and everything is possible...

Proud Red
 
Kwa brewster sitokupinga maana jana hajacheza mpira tuliouzoea toka kwake lkn kwa jones mkuu hapo nakupinga mbona kacheza mpira mzuri tu,sema kuna baadhi ya move alikuwa anatakiwa awe anatumia nguvu nying .
Jones kapiga soka la uhakika. Brewster hakupata sana services jana kama uliliona hilo. Ilibidi awe anashuka chini kutafuta na yeye. Lallana pale sio natural position ndo maana nae nampa 5/10...Gomez hana game time ndo maana waona kama labda hayuko poa but ni mzuri tu. KI-JANA ni noma sikujua kama anaweza cheza namba ya Anolrd vizuri vile maana ile FA cup na wolves last season alikuwa beki wa kati. Ila jana pembeni kapiga soka la kibabe na goli juu. Kipa yuko poa ana machale mazuri ya kipa asilia. Keita katoka majeruhi so nampa 6/10. Milner alisaidia madogo vzuri tu 10/10. Chambo pia 9/10. Lovren alizingua ile mara moja ila alisaidia sana mwishoni madogo walipokuwa wanakuja kwa kasi 8/10.Elliot ingawa ni type ya harry wilson lakini ni Noma. Kikosi atakachokikuta gerrard wakati kloop anasema kitakuwa moto labda aharibu tu mwenyewe.
 
Achana na media comments za kiingereza nakuhakikisha brother Jones ni mchezaji wa kawaida sana na hana future yoyote ni aina ya wachezaji wa kiingereza ambao technically hawana uwezo

Sina comment juu ya hili kwa Curtis Jones coz sikuangalia mpira
 
Siku zote ushindi na Mafanikio ndiyo Njia pekee ya kunyamazisha Washabiki kindakindaki wenye kiu ya Mafanikio.

Kuanzia Mwaka Mmoja baada ya Ujio wa Klopp mpaka kufikia Kati kati ya Msimu wa 2018/19 tulilalamika sana na Kumkosoa Klopp vikali sana ambapo sisi Wengine tulimlaumu kwa hasira zaidi kuhusiana na Strategies zake za Kuwaamini Wachezaji Wasiokuwa na Uwezo kuwa Ndiyo Chaguo lake la Kikosi cha kwanza.
Mfano wa Wachezaji tuliowalalamikia mpaka tukaonekana Hatuipendi Timu au Hatumpendi Klopp au Tunamuona Klopp hajui ni hawa:-

1) Mignolet
2) Karius
3) Clyne
4) Lovren
5) Moreno
6) Henderson
7) Lallana
8) Origi
Hao wote ni Wachezaji ambao walikuwa na Nafasi ya kucheza kikosi cha kwanza na tukapinga Vikali kuwa si Wachezaji wa kutufikisha popote kwa lolote lile! Lakini ilijaribiwa kutuaminisha kuwa ati wangeliweza kutupa Makombe hasahasa EPL.

Pia tulihuzunishwa sana kwa ile kauli Yake baada ya Mourinho kufanya Blockbuster signing ya Pogba pale aliposema 'Yeye hawezi kufanya usajili wa big signing' jambo ambalo kwa soko la sasa Mpira ni pesa tu na Wala sio Venginevyo kwani bila ya kutumbukiza zile £75m (VVD), 65m (Alison), 50m (Fabinho) n.k. Klopp na Ugenius wake tusingelifika hapa tulipo.
Kwahiyo mpira ni pesa tu na si venginevyo.

Lakini sasahivi Tunapata Matokeo Chanya na tunabeba Makombe Sote Kimya na Hakuna Mshabiki anaelogin na kuanza kulalamika. Sote humu ndani ni Furaha tu na Kusifu pamoja na kupongeza Wachezaji wetu na Kocha Wetu Mpendwa Klopp.

Kwahiyo sasa imeshathibitika wazi kuwa Sisi Hatukuwa tukimchukia Klopp! Wala hatukuwahi kumuona kuwa Hajui! Bali tulikuwa tu ni Wakosoaji dhidi ya Sera zake za Kicomenisty..

Sasahivi ameshatuondolea ile tuliyohisi kuwa ni Mizoga katika Kikosi cha kwanza basi tumekuwa na Amani kabisa.

Tumejaa Furaha
Tumejaa Amani
Tumejaa Upendo

Hongera Klopp
Hongera Liverpool FC
Tunaamini Mafanikio
Mafaniko ni Klopp himself
So, Tunamuamini Klopp
SG is the only Manager ninayeweza kumkaribisha kumrithi Klopp.

MAFANIKIO YAKITAWALA FURAHA INATAWALA NA MALALAMIKO HUPOTEA
 
Mimi sijaangalia Mpira lakini mbona Ratings na comments za Wadau kwenye Platforms mbalimbali zinatofautiana na uliyoyaandika kuhusu Jones?
Wamemsifu sana kuwa ana kipaji
Kipaji anacho ila comment ya jamaa labda anaringanisha na senior players..kwa jana alikosa confidence
 
Kweli Mpira pesa na akili pia muhimu.
 
Kipaji anacho ila comment ya jamaa labda anaringanisha na senior players..kwa jana alikosa confidence
Kwa haina ya mpira wa madogo jana..liverpool tunatakiwa kuwekeza zaidi kama tunataka kuwa na future na muendelezo mzuri,hatuna madogo wanaocheza mpira wa kipaji wote wanacheza mpira wa kufundishwa hakuna natural tarents...!
 
Kwa heshima na taadhima tafadhali mtoe Origi kwenye hiyo orodha alafu muweke Karius namba moja
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…