Live Updates: Tanzania Vs Ivory Coast – World Cup Qualification 2014, June 16, 2013

Live Updates: Tanzania Vs Ivory Coast – World Cup Qualification 2014, June 16, 2013

CIV wamechoka sasa....Kasi yao imepungua....Tunawashambulia....Kona....Kiemba anachezewa foul
 
Kona kuelekea lango la CIV......Tumewashika hasa hawa jamaa, tatizo ni umaliziaji
 
Nazungumzia hiki kipindi cha pili si unaona hakuna goli.

Kipindi cha kwanza kulikuwa na kujisahau na kuzubaazubaa.

Hapo sawa, ila mimi naona kama haya majamaa yamechoka basi angepatikana sijui nani mwingine aingie wasaidiane na Ulimwengu na Samata na Kiemba wayakimbize ili angalau tusawazishe.
 
Katika Siku Taifa Stars imecheza mpira basi leo kama hatujashinda au draw hapa leo ndio basi leo Sammatta kafanya makubwa kushinda wachezaji wengi top 4 ya EPL ikatokea freekick yengine akaipiga pembeni kidogo chini wameumia hawa washaanza kupigana wenyewe kwa wenyewe Ivory Coast.
 
Mtindo wa kupoteza muda IC wengi wa wamezoea kuutumia Ughaibuni.
 
Mwinyi-workfire ndo mtungua kona leo
tunawakosa sana,ila kipa wao mzuri jaman
 
Washaanza kugaragara chini kama wanamashetani ya ki west africa au drogba jin.
 
Mbwana angeshuha kidogo.

Anajitahidi sana kupiga dead balls......Comentator wa TBC anamuita Mwinyi Kazimoto(mpiga kona) dead ball speacialist.....lol

VIV wanapoteza muda sasa, wanajiangusha.....Didier Zokora anajiangusha kupoteza muda
Nini Gooooooo......Aaaah.....Kipa anadaka kama Nyani....What a header by Ulimwengu
 
Huyu Ulimwengu vipi?.....Mbona anakosa goli la wazi kabisa....

CIV wanafanya sub nyingine.....Wamezidiwa kwa kweli.....Wanapoteza muda
 
Muda unazidi kuyoyoma dakika 10 zimebakia na hii ni nafasi ya kufunga.
 
goli la pili ni uzembe wa mabeki. hakika timu yetu ya taifa bado ina hitaji maandalizi ya kutosha kuingia kwenye kombe la dunia, tusahau kwanza na ndoto za kwenda brazil tujikite na kuijenga timu yetu kuanzia viungo, mabeki na hata washatumbuliaji, wachezaji wetu wamekuwa wakipunguza hamasa wanapo fungwa na hilo si tatizo la wachezaji tuu hata mashabiki wanao kwenda uwanjani wakiona wamefungwa wananyea yani wanashangilia kwa hamasa wakiona timu yao imefungwa.

safari bado tunayo ndefu kuelekea mashindano ya kombe la dunia nafikiri tujiandae kwa mwaka 2022
 
Back
Top Bottom