Live on ITV - UZALENDO: Dr Slaa vs Mangula

Live on ITV - UZALENDO: Dr Slaa vs Mangula

Status
Not open for further replies.
Katika kipindi cha Uzalendo kilichorushwa leo na ITV,Makamu Mwenyekiti wetu wa CCM Tanzania Bara,Comrade Phillip Mangula hakupewa nafasi ya kutosha. Dr.Wilbrod Slaa ndiye hasa alikuwa ndiye mgeni mlengwa wa kipindi hicho.Maswali ya kufikirisha aliulizwa Dr.Slaa. Yale ya kawaida akaulizwa Mangula.Tena,Mangula akafinyiwa muda wake wa kujibu na wakati Fulani kusahaulika katika kutupiwa swali linguine. Kwanini imefanyika hivi? ITV nao ni CHADEMA. Tujue mapema.Kuna haja kwa chama chetu cha CCM kugomea ushiriki wa vipindi kama hivi. Laasivyo, chama kitaaibika kupitia vipindi hivi vya luninga. Tusishiriki midahalo ya aina yoyote ile. Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Mtanzania mwenye utajiri wa hajabu davis mosha by le mutuz
 
Katika kipindi cha Uzalendo kilichorushwa leo na ITV,Makamu Mwenyekiti wetu wa CCM Tanzania Bara,Comrade Phillip Mangula hakupewa nafasi ya kutosha. Dr.Wilbrod Slaa ndiye hasa alikuwa ndiye mgeni mlengwa wa kipindi hicho.Maswali ya kufikirisha aliulizwa Dr.Slaa. Yale ya kawaida akaulizwa Mangula.Tena,Mangula akafinyiwa muda wake wa kujibu na wakati Fulani kusahaulika katika kutupiwa swali linguine. Kwanini imefanyika hivi? ITV nao ni CHADEMA. Tujue mapema.Kuna haja kwa chama chetu cha CCM kugomea ushiriki wa vipindi kama hivi. Laasivyo, chama kitaaibika kupitia vipindi hivi vya luninga. Tusishiriki midahalo ya aina yoyote ile. Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

si mlionywa na MAKAMBA?
 
Wakuu sikuwa katika nafasi nzuri ya kuangalia kipindi cha leo kutokana na majukumu japo naona ma-Lumumba humu JF wameanza ngebe zao. Kwa tathmini ya haraka haraka nani kamgaragaza mwenzie katika mdahalo wa leo? CDM au CCM? Na ni katika areas zipi hasa kila chama kimejipatia pointi zaidi? General appearance, confidence, and straight-to-the-point nani ka-win zaidi?

Hii kitu ni muhimu sana hasa kuelekea 2015. Usishangae kwa kipindi cha leo kila chama kikawa kimepoteza au kuingiza wanachama wapya kutokana na jinsi wawakilishi wa vyama husika walivyomudu kipindi. Midahalo inatisha hasa katika medani za kisiasa ambapo neno moja linaweza kukupotezea au kukupatia maelfu ya wananchama. Usione baadhi ya vyama vinakimbia midahalo - wanajua impacts zake hasa pale unapokuwa huna hoja za maana za kuwaambia wananchi.
 
humu ndani mbona anazungumzwa Slaa tu?kwani alikuwa mgeni pekee?unajua mtu asipokuwa na cha kujivunia,hubakia kuzungumzia vya wenzie.hebu lumumba boys tuambieni huyo mbabu mwingine kaongea nini tulinganishe hoja.wenzenu wanamzungumzia Slaa wao,what about you?
 
You don't make any sense,Just go back to school and learn more english lessons to improve your english.Your cannot even make a proper english sentence!

Teh teh teh, umesema "your cannot..?", wewe ndio wakumshauri mwenzako arudi shule?, wewe utarudi wapi?
 
Katika kipindi cha Uzalendo kilichorushwa leo na ITV,Makamu Mwenyekiti wetu wa CCM Tanzania Bara,Comrade Phillip Mangula hakupewa nafasi ya kutosha. Dr.Wilbrod Slaa ndiye hasa alikuwa ndiye mgeni mlengwa wa kipindi hicho.Maswali ya kufikirisha aliulizwa Dr.Slaa. Yale ya kawaida akaulizwa Mangula.Tena,Mangula akafinyiwa muda wake wa kujibu na wakati Fulani kusahaulika katika kutupiwa swali linguine. Kwanini imefanyika hivi? ITV nao ni CHADEMA. Tujue mapema.Kuna haja kwa chama chetu cha CCM kugomea ushiriki wa vipindi kama hivi. Laasivyo, chama kitaaibika kupitia vipindi hivi vya luninga. Tusishiriki midahalo ya aina yoyote ile. Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

umenichekesha sana. hahaha chadema inawasumbua sana.hivi kipindi cha dakika 45 huwa wanaalikwa sana watu kutoka chama gani? hili una liongeleaje?
 
Watu hamtaki kushghulisha ubongo someni bas lebo kweny heading jamaa ka indicate ITV mmekazana kuuliza chanel gan ,ina mana hamuoni hapo juu
 
hili ndio tatizo letu watanzania, tunapenda sana kupotosha.!
slaa alikuwa anatoa mfano wa mabunge ya vyama vingi huko ulimwenguni yanavyoendeshwa ambapo alisema watu wanafikia hatua ya kupigana!
pia kuhusu amani amesisitiza kama ambavyo amekuwa anasisitiza kuwa AMANI haihubiriwi bali ni matunda! Na ni matunda ya HAKI.!
Tukiwa na serikali inayotenda haki, amani itakuwepo
Uwelewa wake mdogo sana mkuu. Hajui lolote katika sentensi anachukua neno moja na kulitolea maana. All in all Dr. Slaa is next level yaani hapa inaonekana ni watu wawili tofauti sana. Big up CDM
 
mnalalamika Mangula hajatupiwa maswali ya kufikirisha kwani hamjui protocali za chama tawala?mtangazaji kashaonywa asimuulize mzee maswali magumu halafu amshughulishe slaa,matokeo yake ndio haya,binti kachumbiwa na wanaume wawili mmoja mwanamfalme,mwingine mtoto wa maskini,ugomvi inabidi uamuliwe kwa vita.kila mmoja apambane na mnyama mkali.mfalme kamuonea huruma mwanae akala njama na ba mkwe wakampa mwanamfalme kondoo na huku jamaa mwingine kapewa simba ili atafunwe.matokeo yake jamaa kamuua simba baada ya mpambano mkali na mwanamfalme kachinja kondoo bila jasho.binti alipoulizwa akajibu,"namtaka huyu jasiri aliyeua simba,atanitetea siku ya shida".wazee wakabaki wanatazamana tu kama lumumba boys mnavyochungulia screen zenu hapo!mnalalamika mmepewa kondoo wakati mlisema hammuwezi simba,wenzenu hawachagui!
 
You don't make any sense,Just go back to school and learn more english lessons to improve your english. Your cannot even make a proper english sentence!

I will be glad if you correct me where I have gone wrong as I have done on your sentence. Do the same please!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom