Naanza kwa kukubali title yangu ndiyo, kabudi ni level nyingine kwa kina Lissu na mdee,
Najua nitapigiwa kelele baada ya uzi huu wengine watasema umetumwa, wengine watasema heshima yako inashuka no sina heshima hapa, nipo kuwasilisha mawazo yangu,
Kwa uwezo wa kabudi wa uwasilishaji wa mazungumzo na mijadala huwezi kumlinganisha Lissu hata siku moja,
Lissu uonekana anajua sheria kwa wasioelewa,
Kwa kifupi lissu hupiga kelele kwa kutaja vifungu n.a. watu wanashangilia bila kujua,
Kwa ufupi nimefuatilia hata baadhi ya hoja za kibatala nikaona Lissu uanasheria wake anacheza na jukwaa tu,
Hajafika hata level za kina Marando, au Advocate Mukono, ila kwakuwa hawana platform ya kuonekana watu hawagundui
Angalia presentation style ya kabudi na relevance ya anachokisema kutokana na sheria, mwangalie LIssu presentation na relevance ya anachoongea, kwa kifupi Lissu sheria yake haijafika level hizo mnapomuweka,
Akiacha kuongea kwa kupiga kelele akiwa ametulia atakuwa mwanasheria mzuri , bado Ana nafasi afanye mazoezi
Your Prof.is very deeeeeep, but in a Shallow water. Should not be compared to Lissu at all! At all, Lissu dives in deep Seas while your Prof dives in a swimming pool! Sasa wapi na wapi?
Nitakupa mfano mmoja: Niliwahi kuchukuliwa na shirika Fulani nikapelekwa Kilolo kwenda kutoa Elimu ya Haki za Kisheria katika Umiliki wa Ardhi. Siku ya kwanza Boss wangu ndie aliefanya presentation kwa Wananchi! Yeye sii mwanasheria Kama Mimi, katika presentation Yake Kuna Mambo mengi sana ama kwa kujua au kutokujua alikuwa akipotosha! But he wasn't stammering, alinyoosha presentation Yake Safi, alijibu maswali kwa kunyoosha maelezo, na kila mtu alikubaliana na kilichoelezwa! Kesho Yake ilikuwa zamu yangu, nami kwa kuwa tulikuwa Kijiji kngine, nikatumia knowledge niliyonayo ipasavyo, nikanyoosha maelezo ipasavyo, Hadi Wananchi wa Kilolo nakumbuka walinipa kuku nikaenda kuchinja. Ninachokieleza Ni kwamba, kila mmoja wetu presentation Yake kwenye same topic aliifanya kwa uwezo Mkubwa, tofauti Ni kuwa, mmoja alipotosha, mwingine alieleza Mambo yalivyo.
Mfano mwingine, nime base Sana kwenye Haki za watoto kwa Sasa, naendesha trainings za kutosha tu huku nilipo, nikianza kuhubiri akili na masikio ya wasikilizaji Huwa havitikisiki, very attentive, nimekuwa mbobevu katika Hilo, ila Kuna siku kwa kutokujua uwepo wa kanuni mpya nilijikuta nashushuliwa na Afisa Maendeleo ya Jamii kuhusiana na masuala Fulani yanayohusu watoto! Mmi nikiilaumu serikali kwa kutowezesha utekelezaji wa baadhi ya provisions kwenye Child Act kutokana na kutokuwapo kwa kanuni, mwenzangu akaniambia kanuni zipo na akazionesha! Palamagamba nae kutokana na uzoefu wa muda mrefu na kujiamini katika maeneo mbalimbali ya kisheria, na amekuwa Kama Mimi, anajiamini hata Kama asemacho Ni upotoshaji!
Lissu hawezi lingana na kina Mkono kwa sababu labda ya Areas of concentrations! Mkono ukimpa Criminal au Land cases utakuwa unamuonea, mpe kwenye Investment, Dispute Resolutions, Corporate, etc. Halafu Mkono yeye alichoweza Ni kuajiri ama ku partner na Mawakili wengine Wazuri, yeye uliwahi kumuona kwenye debates? Mahakamani?
Marando is one of the most senior advocates na Ni mzuri Sana kwenye litigation, hao ndio mentors wa kina Lissu, so kwa vyovyote vile, Huyo Kabudi wenu akili ya chuoni kaiacha hukohuko, kwenye Serikali ya Vichaa kaja na Macho Yale na Tumbo!