Lissu ametengwa? Tazama kinachoendelea

Lissu ametengwa? Tazama kinachoendelea

Countrywide

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2015
Posts
21,193
Reaction score
33,577
Mimi binafsi huwa simkubali kabisa Lissu, lakini kuna usemi unatumika sana unasema adui yako muombe njaa, lakini hapo hapo wanasema adui yako vitani akiwa na njaa mpe chakula muendelee kupigana.

Leo nimekuja mbele yenu namuombea chakula Lissu, sio chakula hiki tunachokula bali namaanisha namuombea aonewe huruma kwa kinachoendelea. Lissu ametengwa, anapigana vita peke yake anakaribia kushindwa na kuanguka vibaya mno.

Nawaomba CHADEMA mpeni support ili muendelee kupigana vizuri. Lissu anatia huruma, amenyong'onyea, amekata tamaa

Lissu hana tena support anapopita kufanya mikutano. Sasa hivi anatumia miti kama majukwaa, hana tena support. Tuliruhusu mikutano ya hadhara ila hatujaruhusu hii minyukano yenu ya ndani kwa ndani.

Angalia hapo kinachoendelea kwa Lissu, je kweli mnakubaliana na hili?

20230521_124731.jpg
20230521_130150.jpg
20230521_130206.jpg
 
Tundu Antipas Lisu ni Kiongozi wa kitaifa hivyo miundombinu ya maeneo anayofanyia mikutano usalama wake uzingatiwe

Kuna picha nimeona huko twitter Tundu Antipas Lisu akihutubia Mkutano akiwa kwenye jukwaa mfano wa Kichanja cha kupigia Mahindi wakati wa Mavuno yaani mimesikitika mno

Natoa tu angalizo kwenu nyie akina Pambalu na Mwaipaya

Nawatakia Dominica Njema!
 
Kwa mara ya kwanza nakuunga mkono

Ilipaswa wawe na uwiano sawa wa vitendea kazi maeneo watakayo hutubia

Ukiangalia mwamba yeye kajichagulia maeneo yenye wafuasi wengi na kambi za cdm

Ingelipendeza majukwaa na menyewe yaendane na hadhi ya mtu atakayelitumia

Makamo mwenyekiti na alikuwa mgombea urais kweli jukwaa Hilo kweli ?
 
ENC
Mimi binafsi huwa simkubali kabisa lissu, lakini kuna usemi unatumika sana unasema adui yako muombe njaa. Lakini hapo hapo wanasema adui yako vitani akiwa na njaa mpe chakula muendelee kupigana...
Erythrocyte kwa nini mnaacha watu wanafanya uhuni kama huu kwa Lissu? Au mnataka kumuua?

Hilo jukwaa ni la hatari sana na hapo ni kama limetegeshwa aanguke achomwe na mbao na kuni afe. Kweli imeshindikana kuandaliwa jukwaa la kumfaa? Sometimes tunapowafokea mnatuita sisi CCM kumbe mna ujinga mwingi sana.
 
Wamemtenga
Hivi Lissu ameshindwa kutulia na kuwa mungwana kwa Chuo chake aliposomea sheria kwa kuwasaidia namna ya kuondoa mkwamo kwa wanafunzi wa shule ya Sheria?

Mtakumbuka sakata la Shule hiyo ya sheria la hivi majuzi.
 
Hata kama simpendi Lissu ila si kwa mnavyomfanyia nyinyi Chadema, acheni huu ujinga,

Lissu ni kiongozi wenu, mhakikishieni usalama wake
 
Dah! hii haikubaliki, Chadema lengo lenu nini kumpandisha Lisu kwenye hizo chaga, kweli akufukuzae hakwambii toka Lisu karibu ACT.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom