Ngaliwe
Senior Member
- Dec 30, 2015
- 161
- 364
Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Paul Makonda amembananisha Meneja wa TANROADS Geita kukihakikishia Chama Cha Mapinduzi kuwa ni lini barabara ya Kahama - Kakoro yenye urefu wa Kilomita 60 itajengwa kwa kiwango cha lami.
Mwenezi Makonda ambananisha Meneja huyo mara baada ya kutoridhishwa na majibu yake na kumtaka kuwasiliana na Viongozi wenzie kisha kutoa majibu papo hapo kwa Wananchi wa Geita ili kujua lini wataondokana na hadha hiyo.
" Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amerahisisha mifumo ya Mawasiliano hivyo wasiliana na Viongozi wenzio mjue ni lini na uje kutoa jibu ili Wananchi hawa wajue na sio kuwadanganya " Alisema Mwenezi Makonda.
Mara baada ya kufanya Mawasilano, hatimaye Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa alipiga simu na kukihakikishia Chama Cha Mapinduzi kuwa hadi kufikia mwisho wa mwezi Novemba mwaka huu hatua za manunuzi zitakuwa zimekamilika na mwishoni mwa mwezi Disemba mwaka huu Mkandarasi (CCIC) ataianza kazi rasmi ya ujenzi wa barabara hiyo.
Mwenezi Makonda amewataka Wananchi kuwa wavumilivu na kusubiria kuona utekelezaji wa ahadi hiyo iliyotolewa huku akiahidi kuweka msukumo mkubwa kufanikisha utekelezaji huo kwa haraka.
Ameyasema hayo leo tarehe 11 Novemba, 2023 wakati alipozungumza na Wananchi wa Wilaya ya Geita akiwa ziarani kikazi katika Mkoa wa Geita
#CCMKazini
#VitendoVinaSauti
#TunaendaNaMama
PIA, SOMA:
Kauli na matamko mengine ya Makonda
Mwenezi Makonda ambananisha Meneja huyo mara baada ya kutoridhishwa na majibu yake na kumtaka kuwasiliana na Viongozi wenzie kisha kutoa majibu papo hapo kwa Wananchi wa Geita ili kujua lini wataondokana na hadha hiyo.
" Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amerahisisha mifumo ya Mawasiliano hivyo wasiliana na Viongozi wenzio mjue ni lini na uje kutoa jibu ili Wananchi hawa wajue na sio kuwadanganya " Alisema Mwenezi Makonda.
Mara baada ya kufanya Mawasilano, hatimaye Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa alipiga simu na kukihakikishia Chama Cha Mapinduzi kuwa hadi kufikia mwisho wa mwezi Novemba mwaka huu hatua za manunuzi zitakuwa zimekamilika na mwishoni mwa mwezi Disemba mwaka huu Mkandarasi (CCIC) ataianza kazi rasmi ya ujenzi wa barabara hiyo.
Mwenezi Makonda amewataka Wananchi kuwa wavumilivu na kusubiria kuona utekelezaji wa ahadi hiyo iliyotolewa huku akiahidi kuweka msukumo mkubwa kufanikisha utekelezaji huo kwa haraka.
Ameyasema hayo leo tarehe 11 Novemba, 2023 wakati alipozungumza na Wananchi wa Wilaya ya Geita akiwa ziarani kikazi katika Mkoa wa Geita
#CCMKazini
#VitendoVinaSauti
#TunaendaNaMama
PIA, SOMA:
Kauli na matamko mengine ya Makonda
- Makonda: 2024 na 2025 tutakupima kwa kazi; sio kwa maneno, sio kwa kugawa kanga kipindi cha uchaguzi
- Makonda: Yetote mwenye sifa atasimamia uchaguzi
- Paul Makonda: Tumechoka na ahadi za treni za umeme
- Makonda: Ningeteuliwa kuwa Mwenezi kipindi cha Magufuli wangenyooka hawa
- Sifanyi mikutano ya kujaza watu kwa kutumia wasanii kwasababu tunataka kuona uhai wa CCM na jumuiya zake - Mwenezi Makonda
- Mwenezi Makonda amuagiza Meya na Mkurugenzi Halmshauri ya Pangani kuhakikisha kituo cha afya cha mwenbeni kinajengwa - Pangani
- Mwenezi Makonda ampatia tsh milioni 2 kijana mjasiriamali mwenye kujiendeleza kibiashara
- Makonda: Siasa imemlipa Mbowe kajenga kasri
- Mwenezi Makonda amuagiza Meya na Mkurugenzi Halmshauri ya Pangani kuhakikisha kituo cha afya cha mwenbeni kinajengwa - Pangani
- Makonda ambananisha meneja TANROADS Geita: Ahoji ni lini mkataba wa ujenzi wa barabara ya Kahama - Kakoro (km 60) utasainiwa ili ujenzi kuanza
- Paul Makonda: Lissu mjanja ameona maandamano hayana maana
- Makonda: Mbinguni walimchukulia fomu Rais Samia. Adai Mbowe anajua kama Samia ametumwa na Mungu
- Makonda: Wafanyabiashara huichangia CCM kwa kuogopa wasiletewe TRA, TAKUKURU, uhamiaji ama Polisi
- Makonda: Stendi mpya Iringa ipewe jina la Chongolo