Ligi ya Hispania ni mbovu kulinganisha ya Uingereza

Ligi ya Hispania ni mbovu kulinganisha ya Uingereza

Raphinha alikuwa flop uingereza akiwa leed utd mpaka wakashuka daraja wewe unataka kusemaje
Raphinha hakuwa flop acha uongo ndugu yangu.

Raphinha sio my favorite player ila sio vizuri kumsemea uongo.

Huyo Raphinha alikuwa anatakiwa na Arteta ila Deco akakaza aende Barca na dogo akaona Barca ni timu la dunia akafanya maamuzi.
 
Uingereza kuna timu sita tofauti zimebeba uefa
Spain ni timu mbili tu unaweza ukaelewa
Sawa ila tatizo ni idadi ya hizo uefa, hizo timu huwa zinakuwa wapi hadi madrid anachukua uefa 15, barcelona anachukua tano na kina ac milan wanachukua saba
 
Sawa ila tatizo ni idadi ya hizo uefa, hizo timu huwa zinakuwa wapi hadi madrid anachukua uefa 15, barcelona anachukua tano na kina ac milan wanachukua saba
Pamoja na bayern anachukua 6 alaf epl ni lig ya wana siasa/wapga domo hakuna mpira mzur
 
Pamoja na bayern anachukua 6 alaf epl ni lig ya wana siasa/wapga domo hakuna mpira mzur
Yeah mkuu siku hizi hata ile rivalry iliyokuwepo kati ya Liverpool na Man U hainogi tena kama rivalry iliyopo kati ya Barcelona na Real Madrid, Man U ndio hao siku hizi kila mtu anajipigia tu na Liverpool nao hawaeleweki msimu mmoja wako vizuri msimu unaofuata wanaflop huku mashabiki wa Arsenal na Chelsea nao ni kama wamejikatia tamaa, yani toka Man City waanze kuchukua ubingwa back to back ni kama ligi ya EPL ikaanza kuwa hainogi tena, maana ni timu ambayo haikuwa na mashabiki ilipata mashabiki kutoka kwenye hizo timu kubwa zilizoanza kuflop, hivyo hao mashabiki ni kama walikuwa wanatafuta furaha waliyoikosa kwenye zile timu zao tu na si kwamba ni wapenzi wa Man City
 
Timu kupiga pasi tatu ni mfumo tu hii inaonesha hao wapigaji wa pasi wana ufanisi wa kutosha
Timu ikishikwa hadi Messi alikuwa anazurura uwanjani
Acha kujilisha upepo na hiyo EPL yako, kwani ndani ya miaka zaidi ya 24 iliyopita EPL yenyewe imechukua Ballon D'or imetoa wachezaji wawili tu ambao Ni Cristiano Ronaldo na Michael Owen. Huku ndani ya miaka hiyo Spain Laliga imechukua mara 14 na bado unasema si ligi bora?

Acha mahaba kwani mnazidiwa hata na Italia serie A.
 
bora uangalie mpira wa bundesliga unaweza kukuvutia ila sio epl
Ni kweli maana Bundesliga ni ligi bora ya pili kwa kucheza mpira wa kuvutia duniani. Hao kenge wa EPL baada ya kuona ligi haina mvuto bali ina promosheni kubwa wakaja na kamsemo chao cha kujificha "dah mpira mna matokeo ya kikatili sana"
Hapo unakuta timu imezuia wee wakapata kona wakochomoa goli, kumbe mbwembwe tu.
 
Sasa hizo timu za england huwa zinakwama wapi kubeba makombe ya ucl, kama tu arsenal hadi leo hawana na man city ndio kwanza wamechukua juzi juzi, bora ungesema ligi za italy na germany ila england na spain zipo kwenye level moja
Chambuzi la ball,asante
 
Vijana wengi wanaoshabikia EPL wana matatizo ya akili, kwahiyo sikushangai mkuu
 
Raphinha alikuwa flop uingereza akiwa leed utd mpaka wakashuka daraja wewe unataka kusemaje
Kwanza Raphina hajawai kuwa flop uingereza.

Pili Raphina hajawai kushuka daraja na Leeds united.

Mechi na Brentford ambayo ilikuwa inaamua hatima ya Leeds kubaki ligi kuu 2022 Raphina kafunga goli muhimu la penati mechi ikaisha 2-1 Leeds akabaki ligi kuu.

Labda wewe utuwekee mwaka ambao Raphina kashuka daraja na Leeds.

Mana Leeds imeshuka daraja msimu wa 2022/2023 Raphina akiwa tayari ameshaondoka leeds na kujiunga na Barcelona.

Tatu kabla ya Raphina kutua Barcelona alikuwa anatakiwa kwa udi na uvumba na Chelsea angekuwa mchezaji mbovu(flop)Chelsea inayotoka ligi bora isingemtaka.

Raphina akawakataa Chelsea akaja Barcelona.

Mwisho kabisa EPL sio ligi bora kuliko La Liga.

Ila ina ushindani kwa sababu timu nyingi uwezo wake mdogo unakaribiana hali inayofanya kuwe na ushindani ila quality mbovu.


La liga ina timu zenye uwezo mkubwa sana kuliko EPL.
Screenshot_20250523-183456_Google.jpg
 
Back
Top Bottom