Ligi Kuu Bara: Kocha Afungiwa Miaka Mitano Kwa Kushawishi Wachezaji Kugomea Mchezo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,814
11,991
Makata.jpg

Mbwana Makata
Kocha Mbwana Makata na Meneja David Naftali wa Mbeya Kwanza wamefungiwa kwa kipindi cha miaka mitano kila mmoja kwa kosa la kushawishi/kuamuru wachezaji wasiingie uwanjani kuanza mchezo tukio lililosababisha mchezo wa timu yao dhidi ya Namungo FC kutofanyika.

Kamati ya Saa 72 ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania imeipa Namungo FC pointi 3 na mabao matatu na kusema kuwa imejiridhisha Mbeya Kwanza waligomea mchezo huo licha ya taratibu kuwa sawa dakika ya 23 ikiwa ni dakika saba kabla ya kutimu nusu saa.

Aidha, Kocha wa Dodoma Jiji, Masoud Djuma na mchezaji wa timu hiyo, Jamali Mtegeta wamefungiwa michezo mitatu na faini ya Tsh 500,000 kila mmoja kwa kosa la kushambuliana kwa mateke wakati wa mechi ya timu yao dhidi ya Biashara United, Mei 5, 2022.

1.jpg

2.jpg

3.jpg

4.jpg


5.jpg
 
Huko ni kukomoana. Umfungie kocha Kwa kosa ambalo lilikuwa na Sababu zake. Wangetumia busara Zaid. Miaka mitano Mtu ambaye anategemea hyo Kazi....
 
Duh! Ila Mbwana Makata na huyo Meneja wako David Naftali, mlitakiwa kutumia tu busara. Mnafahamu fika hii nchi ni ngumu sana!

Ona sasa adhabu mliyopewa! Usawa huu ukae nje ya uwanja kwa miaka mitano siyo jambo jepesi hata kidogo.
 
TFF ni kukomoana Tu, Nchi hii mpira kupiga hatua ni kazi kweli.
Sasa miaka mitano yote ya NN hiyo. Si wangemfungia hata mwaka Mmoja halafu faini akapewa kubwa.

Yani TFF bwana ndo maana wanasema Tanzania Football Failure
 
View attachment 2228200
Mbwana Makata
Kocha Mbwana Makata na Meneja David Naftali wa Mbeya Kwanza wamefungiwa kwa kipindi cha miaka mitano kila mmoja kwa kosa la kushawishi/kuamuru wachezaji wasiingie uwanjani kuanza mchezo tukio lililosababisha mchezo wa timu yao dhidi ya Namungo FC kutofanyika.

Kamati ya Saa 72 ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania imeipa Namungo FC pointi 3 na mabao matatu na kusema kuwa imejiridhisha Mbeya Kwanza waligomea mchezo huo licha ya taratibu kuwa sawa dakika ya 23 ikiwa ni dakika saba kabla ya kutimu nusu saa.

Aidha, Kocha wa Dodoma Jiji, Masoud Djuma na mchezaji wa timu hiyo, Jamali Mtegeta wamefungiwa michezo mitatu na faini ya Tsh 500,000 kila mmoja kwa kosa la kushambuliana kwa mateke wakati wa mechi ya timu yao dhidi ya Biashara United, Mei 5, 2022.

Hopeless TFF
 
Sheria nachijua mm inasema baada ya dk 15 kama gar halijafika uwanjan bas timu mwenyeji atapokwa point 3

Au imebadirika Tena ?

Pm anaogopwa Sana
 
Tff wanatabia za kijangili, adhabu za namna hii hazileti afya Kwa ustawi wa mpira wetu. Waziri wa michezo aingilie kati Ili kukomesha adhabu za kipuuzi za namna hii. Kwa Nini umfungie mtu miaka mitano na si mechi Tano!!
Hii ni dalili ya Tff kujiona miungu watu.
 
Tff wanatabia za kijangili, adhabu za namna hii hazileti afya Kwa ustawi wa mpira wetu. Waziri wa michezo aingilie kati Ili kukomesha adhabu za kipuuzi za namna hii. Kwa Nini umfungie mtu miaka mitano na si mechi Tano!!
Hii ni dalili ya Tff kujiona miungu watu.
Hivi ni wakati Gani Wanaotuumiwa na Hyo Kamati wanapata Mda wa kujitetea?
.
Ts means Hii Kamati Ya Msaa 72 Kanuni zake Haziruhusu wenye makosa Kupewa nafasi ya Kujitetea Kwa Makosa Yao then Hyo Kamati itoe Maamuzi??

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom