Let's face it: Bongo Flava ni rubbish

Hata Hip-Hop Ilipoanza ilikutana na vikwazo vingi sana na muziki huu ulisemekena haukuwa bora lakini miaka ilivyoenda ndio mambo yakabadilika na muziki ukazidi kuboreshwa. Bongo Flava ni Muziki unaokuwa kila siku, tena kwa hivi sasa si Bongo tu bali ndio Muziki maarufu sana hata kwa nchi jirani kama Kenya, Rwanda, Burundi, Uganda na hata baadhi ya sehemu za DRC Congo. Kila kitu kina mapungufu yake na hakuna ubaya kwenye kuchota utaalamu kutoka nchi nyingine.

Vijana wengi sana Tanzania wamejijenga na kujiajiri kimaisha kutokana na mafanikio ya muziki huu, nadhani kila mtu ana uhuru wa kusikiliza chochote anachopenda kama unaona Bongo Flava haikufai basi sikiliza aina nyingine ya muziki. Utakuta mtu anapiga madongo Bongo Flava lakini unakuta ndio huyo huyo anakuwa wa kwanza kusikiliza nyimbo kama Chicken Noodle Soup au Soulja Boy.

Chicken Noodle...that's funny!!!!Anyway, point taken.

Waeleze bwana. Hawajasikiliza lyrics na ngoma za vijana wa nyumbani hawa!
 
Peeps,
You need to understand that Music is an Art! Ukishaelewa hapo, then sidhani uta-question kwanini nyimbo zingine mbaya na nyingine ni nzuri, to say the least, will not even question why muziki wa Tanzania(BongoFlava) ni mbaya na muziki wa ki-Haiti ndio mzuri. Cheers!
 
Hata Hip-Hop Ilipoanza ilikutana na vikwazo vingi sana na muziki huu ulisemekena haukuwa bora lakini miaka ilivyoenda ndio mambo yakabadilika na muziki ukazidi kuboreshwa. Bongo Flava ni Muziki unaokuwa kila siku, tena kwa hivi sasa si Bongo tu bali ndio Muziki maarufu sana hata kwa nchi jirani kama Kenya, Rwanda, Burundi, Uganda na hata baadhi ya sehemu za DRC Congo. Kila kitu kina mapungufu yake na hakuna ubaya kwenye kuchota utaalamu kutoka nchi nyingine.

Vijana wengi sana Tanzania wamejijenga na kujiajiri kimaisha kutokana na mafanikio ya muziki huu, nadhani kila mtu ana uhuru wa kusikiliza chochote anachopenda kama unaona Bongo Flava haikufai basi sikiliza aina nyingine ya muziki. Utakuta mtu anapiga madongo Bongo Flava lakini unakuta ndio huyo huyo anakuwa wa kwanza kusikiliza nyimbo kama Chicken Noodle Soup au Soulja Boy.

Pia nadhani kila mtu ambaye hai-feel bongo flava ana haki ya kuiponda kama vile wenye kuipenda walivyo na haki ya kuitetea na kuiendeleza. Bottom line: whatever floats your boat and to each his own.
 
end of rant sasa nakaribisha watetezi wa huu upuuzi
[/SIZE][/B]

Ni ajabu sana kama wewe ndio umeona sasa, mimi niliona toka decade ago. There is ni doubt kuwa wasanii wenyewe wamepata vijisenti kutokana na Bongo flava (mimi napenda kuiita poor American flavor) na kwa sababu kuna watu ambao hawana uwezo wa kupata tunes nzuri za kusikiliza hizo ndio wanaona zinawasaidia.
No doubt kuwa so far Tanzania sijaona watu wanaojua kurekodi Muziki kama RTD, kama wasingekuwa na urasimu na mambo ya Kizamani bado wanaweza kupata soku kubwa sana. Ukijaribu kustream line kwenye Kompyuta muziki uliorekediwa kwa vyombo hafifu vya Radio Tanzania, by far unaweza kuona walifanya kazi ya kurekodi walikuwa makini. Hata ukisikia content ya nyimbo lugha inakuwa ya maana na ya kistaarabu, na sio kutajana tajana majina kama ilivyo kwenye studio nyingine mabko hata kiswahili hawawezi kukinyoosha.
Lakini baada ya kusema hvyo lazima nikubali kuwa kuna vijana wawili watatu lazima niwape heko sana. Mmoja anaitwa Joseph Haule. Ingawa nilimuona mpuuzi kwa kujiita Nigger J, lakini inaonekana kuwa nyimbo zake huwa anakaa na kufikiri na kutunga kisawa sawa na sio kulipuka tu kama walivyokuwa wengi, wa[po wengine wawili watatu i must admit this, lakini walio wengi ni kuiga tu, ujinga tu, utoto na ushororo, Hawako serious hata kidogo!!
 
BONGOLANDER .......HAWA WASANII WETU WAVAA VIKUKU,VIPINI(CHENI ZA MIGUU YA KUSHOTO) HUKU WANAWAKILISHA NCHI AMBAYO SI TANZANIA (poor american flava) HAKIKA KNOW NOTHING ABOUT ART!
 
Nabisha hodi,
Sijaipenda kichwa cha mjadala huu kwani ni kizito sana.

Bongoflava pamoja na mapungufu yake lakini haijafikia kikomo cha titled rubbish...tuangalie hata upande mwingine kwa kweli umetoa ajira kwa vijana wetu kwa mapana yake kuanzia kwa wasanii, mapromota, nk

Kuna mapungufu ambayo ni vyema tukawaweka wazi na kuyajadili.

1. naona binafsi hawa wasanii wanapaswa kuandaliwa hata kisaikolojia kwani wanapokuwa famous wanaleta baadhi shida na hii ni kwa watu wengi na si bongo flava tu.

2. Kuwepo kwa wataalamu mbalimbali waliosomea na kujikita katika nyanja za muziki mathalani Bongoflava mfano kuwa na wanasheria ambao wanaujuma sawia hivyo kuweza hata kuwatetea haki zao, wataaalamu wa masuala ya promotion na marketing stategies nk

Kwa leo hata naahidi kuja tena
 
We brazameni mikosi, sijui unalipwa kuikandia bongo flavour. Nafikiri unalipwa, kwa vyovyote vile utakuwa unalipwa. Kiasi gani unalipwa hiyo ni siri yako, kama wewe jasiri basi weka hiyo figa tuijadili. Kila biashara duniani hudumishwa na soko lake, its about demand and supply, if no demand supply faces a natural death. Sasa huu mwaka wa ngapi? Bongo flavour ipo tu, Musik ina maudhui tofauti, kuburudisha, kuelimisha, kukosoa nk. Jay aliimba "piga makofi" baada ua muda Buster Ryme aliimba klap klap. Buruduni tu.
 
Haka ni kamchango kamngu ka kwanza kwenye hii JF.

Mi naona kuwa kama kuna watu wanafanya kazi yao halali ya kutunga mashairi wakakubalika na wakapata mkate wao halali tuwaache wafanye hivyo. Kuwakandia haisaidii, ila kama kuna ambaye anafikiri kuwa anaweza kuwasaidia mawazo wafanye vizuri zaidi watoe mawazo yao. Si kukandia. Hii ni biashara halali na watu wanapata kipato. Kama wachangiaji wengine walivyosema kama Materanus ni kuwa watu watakataa kazi zao na watafikiri namna ya kuboresha ama kuishia wenye "natural death". Jamani mimi mawazo yangu ni kuwa Bongo flavorur inaweza kuboreshwa kutoa ajira kwa vijana wengi na nchi hii hakuna ajira wazee.
 
Haka ni kamchango kangu ka kwanza kwenye hii JF.

Mi naona kuwa kama kuna watu wanafanya kazi yao halali ya kutunga mashairi wakakubalika na wakapata mkate wao halali tuwaache wafanye hivyo. Kuwakandia haisaidii, ila kama kuna ambaye anafikiri kuwa anaweza kuwasaidia mawazo wafanye vizuri zaidi watoe mawazo yao. Si kukandia.

Hii ni biashara halali na watu wanapata kipato. Kama wachangiaji wengine walivyosema kama Materanus ni kuwa watu watakataa kazi zao na watafikiri namna ya kuboresha ama kuishia wenye "natural death". Jamani mimi mawazo yangu ni kuwa Bongo flavorur inaweza kuboreshwa kutoa ajira kwa vijana wengi na nchi hii hakuna ajira wazee.
 
Brazameni, nimepitia baadhi ya michango yako katika bongo flavour. Inaonyesha ufahamu wako katika biashara hiyo ni mkubwa, nahisi pia wewe ni mmoja kati ya hao waanzilishi. Pengine kinacho kusumbua ni kwamba kama mwanzilishi au shahidi hukufaidika sana na bongoflavour. Sasa roho ina kuuma ukiwaona hao waliorithi mchango wako wanamafanikio japo kidogo. Maisha ndivyo yalivyo, kwa mfano pesa alizopata Pele wakati huo siyo sawa na Ronaldo wakati huu. Rudi kwenye game kama unaweza au shut the https://jamii.app/JFUserGuide up. Kwani graph ya mafanikio ya vijana inaonyesha kuelekea juu kila kukicha.
 
hivi kwanini wasingeweka mtu ama kampuni ambayo kabla ya single yoyote iwe released kwenye maredio na tv iangaliwe kama it meets the quality needed to be published...[just my thoughts],video quality nyingine ni kama wamaefanya shooting na mobile phone video kwakweli.
 
upanzi wa sanaa ndivyo ulivyo.
Nina uhakika ukiwakuta warusi wanafurahia concert zao utawashangaa, au wahehe ha ngoma zao.
si rahisi mtu kumshawishi mwingine apende sanaa fulani ambayo haipendi.
mtu akiipenda sanaa yake huwezi kumuambia ni mbaya.
Huyu jamaa simshangai, wala msibishane nae.
manake hata mkianza kutathmini nyimbo anazopenda yeye mtakuta asilimia 90 hamzipendi na mnaweza mkatumia maneno yake mwenyewe kuzikandia.
mimi binafsi si mpenzi wa nyimbo nyingi tu za bongo fleva, japo kuna baadhi nimezikubali.
lakini maadamu wana wapenzi wao, sina neno.
 
Ukitaka kulalamikia genre kama genre usichukue mifano yake mibovu kabisa, chukua mifano yake mizuri kabisa ili ukimuua Elvis uwe hubakizi kitu katika Rock and Roll, au ukimuua Bob unakuwa hujabakisha kitu katika reggae.

Umeshawahi kusikiliza metaphors na similes za "Professor J"? Umeshawahi kusikiliza satire, sarcasm na wit za Wagosi? Umeshawahi kusikiliza delivery ya Saigon? Umeshawahi kusikiliza the almost cacophonic artful composition of that word smith and lyrics weaver known as Halfani? Umeshamsikiliza Solo Thang akikwambia "kuna marepa na marapper", ulimuelewa? Wewe unasikiliza "marepa" au "marapper"?

Nakubali kuna utumbo mwingi sana kwenye bongo flava (as in hip hop in general by the way) lakini huwezi kui-judge genre nzima kwa Dully Sykes ambaye yeye mwenyewe kashakwambia ni "mzee wa misifa" na siyo authentic hip hopper.Unasikiliza production za "Soundcrafters" unategemea vipi kusikia authentic Tanzanian hip hop.Sikiliza mitwango ya Mika Mwamba na Majani iliyoenda na watu wanaoeleweka kwenye mic, utaelewa kwa nini watu wanashabikia bongoflava.Tatizo ni kuwa kwa kila msanii mmoja wa kweli kuna wengine tisa wana jump on the bandwagon bila talent wala drive, wanatafuta fame na money.

Hayo matatizo unayoyaona kwenye bongoflava yapo mpaka kwenye hip hop na ukiikomalia bongoflava unaweza kuwa self hater au unasikiliza the wrong kind of bongoflava.

Halfani ni P-funk somehow I dont think thats who you meant
 
Brazameni kachukua mifano ya wapiga kelele wachache na kuwaweka katika group moja la watu makini kama Prof J,Ngwair,wagosi na afande sele....

C'mon brazameni rudi tena sikiliza vizuri
 
the problem with bflava ni kuwa.....! Vijana wetu (hasa wanafunzi) si wazingativu sana katika masomo kwani nafasi ya masomo imechukuliwa na bflava, something should be done to save the coming generation.....!
almost kila kijana sasa(TZ) anataka kuwa msanii. wapi anayetaka kuwa PILOT, CAPTAIN, ENGINEER, TECHNICIAN, PROGRAMMER, MILLITARY OFFICER etc bali vijana wanataka shika mic ili watoke.!!!! sawa watatoka ila tunatengeneza generation gani????
Naomba tusije tengeneza generation ya CHIEF MANGUNGO wa coming ages....!
GO ON BRAZAMEN....!
 
Back
Top Bottom