Hii ni moja ya conspiracy theories ambazo tumezoea kuzisikia kwa msiolijua Kanisa Katoliki. Unasimuliwa vihadithi huko mtaani halafu ndio unavibeba kama vilivyo unatuletea hapa.
Kama unajua, Sakramenti zote za Kanisa Katoliki ukishazipokea, tunasema haziondoki. Zinaacha alama ya milele, isiyofutika. Mfano: ukishafunga ndoa, hauwezi kuifungua kokote; ukishabatizwa, wewe ni Mkristu wa milele hivyohivyo kwa Sakramenti nyingine ikiwemo upadre. Na kwa upadre, ni mapdre wote, sio kwa Jesuits pekee. Huu ulioandika ni upotoshaji.
Haya ni mambo ambayo kila mtu anayajua. Hizo hatua wanazozipitia Jesuits ndio almost wanazozipitia mapadre wa majimbo na mashirika yote duniani kote. Kila Jimbo na shirika lina utaratibu wake, lakini mapadre wote ni lazima wapitie malezi, wasome falsafa (diploma au shahada), wasome theolojia (diploma au shahada), wapitie mwaka wa uchungaji, wapewe ushemasi ndio wawe mapadri. Shida haujui na unaandika mambo usiyoyajua. Unapotosha.
Dhambi haiondoi Sakramenti. Kwahiyo hata ukiua au kuzini, au kuiba bado utaendelea kuwa Padri (kupitia Sakramenti ya Upadre), utaendelea kuwa mwanandoa (kupitia Sakramenti ya Ndoa) utaendelea kuwa Mkristu (kupitia Sakramenti ya Ubatizo), n.k. Acha upotoshaji.
Mapdre wote huwa hawalipwi. Na ikitokea ukaacha kutoa huduma za Kipadre, maana yake unajitegemea kwa kila kitu. Ndio maana akina Padri Slaa unawaona wanapambana na hali zao.
Ndio. Majimbo yote na mashirika, ambayo kimsingi ndiyo hulea na kutoa mapadre, yapo ndani na chini ya Kanisa Katoliki.
Uongo mwingine ambao kila siku tunaupinga humu. Nani ameshaona mtu ameshikwa eti kisa ameungama kwa Padri, huyo mtu, atoe ushuhuda na uthibitisho humu. Acheni uongo.
Kwanza CIA ni shirika la ujasusi la Marekani linalohusika na mambo ya intelijensia na ujasusi nje ya ardhi ya Marekani. Halina uhusiano wa aina na namna yoyote ile na Kanisa Katoliki.
Ukishakuwa mchungaji, au sheikh, n.k. maana yake unapingana na mafundisho walau ya Mama Kanisa. Hiyo inapelekea excommunication. Ukiwa excommunicated maana yake umejitenga na Kanisa. Wewe inahesabika kuwa sawa na mpagani. Kwahiyo hii hoja yako inakosa mashiko automatically. Unachotaka kutuambia wewe, kwa hoja hii, ni kuwa Jesuits sio Wakatoliki, kitu ambacho sio kweli.
Ninaomba mleta uzi uwe unafanya utafiti kabla ya kuanzisha uzi, tena kwenye jukwaa hili tunaloliheshimu. Mambo uliyoyaleta, hata kwa Mkatoliki wa kawaida tu ambaye anajua taratibu hizi ndogondogo za Kanisa, atakushangaa sana.
Umeleta upotoshaji tu. Inaonekana umeandika kitu usichokijua. Shame on you!