Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,886
Wakuu Kwema!
Usiku wa leo nimefadhaika Sana, nimesononeshwa mno, nimepatwa na uchungu usioelezeka mpaka usingizi ukakata nikaamka yapata saa saba na dakika ishirini na mbili Kwa saa ya ukutani.
Mwaka Jana niliota ndoto ya namna hii hii lakini nikashindwa kuipandisha hapa kutokana na sababu kadha wa kadha, nilimuona Mzee Magufuli amefariki, kisha nikamuota na Mzee mwingine wa CCM naye kafariki Ila huyo Mzee mpaka sasa hivi ninapoongea yupo hai na hi mzima ea Afya. Sitamtaja, Ila ni mstaafu wa CCM katika nafasi ya Ukaribu taifa bara.
Nikirejea kwenye ndoto ya Leo inayonifanya niandike hapa;
Iweje niote mtu aliyekufa kafa tena?
Ndoto inaanzia tukiwa ofisini mahali, nikiwa na watu kadhaa waserikali. Ofisi ilikuwa kubwa yakutosha yenye meza za kisasa, ukutani ikiwepo picha ya Magufuli, pembeni kabisa kwenye dirisha likiwepo Sofa moja la watu Kama watano hivi lenye rangi ya ugoro la ngozi kwenye pembe lilikuwepo Ua sijajua ni ua bandia au ua kabisa.
Waserikali walikuwa watatu Mimi nikiwa wanne. Wawili walikuwa wamesimama, Mimi na mwingine tukiwa tumekaa kwenye viti(sio sofa)
Tukiwa tunapiga soga, punde bila kutarajia mlango wa Ile ofisi ulifunguliwa, akaingia mtu mmoja wa usalama akifuatwa na watu wa nne kisha Magufuli akafuatia. Mioyo yetu wote ikalipuka Sisi tuliokutwa mule ndani.
Mshtuko wetu ulisababishwa na kumuona mtu ambaye tunajua ameshakufa.
Tukiwa wote tumesimama Kama ishara ya heshima na adabu Kwa Rais, bado tukishangaa Magufuli WA kwenye ndoto akatusalimia Kwa matani Kama ilivyo desturi yake.
Kisha baadaye akasema hajafa, kama mtu anayejibu maswali yaliyomo mioyoni mwetu yaliyochorwa katika Sura zetu zenye wasiwasi..
Wakati akiwa anaongea, mlango wa pili unaoingia ndani kabisa kwenye ofisi zile, ukafunguka na akatokea mtu mmoja aliyevalia suti nadhifu akiwa kaongozana na mtu mwingine mwenye mwili wa kawaida Kama wangu. Walipotokea watu hao, nikashangaa kumuona Magufuli akishika katikati ya Kufua, akilalama kichomi, akilalama hivyo Kwa muda.
Mpaka machozi yakawa yanamtoka.
Wale watu aliokuja nao wakawa wanamshika ili kumpa msaada ili wambebe wamtoe pale wampeleke Hospitalini. Lakini akakataa, mwishowe akaanguka chini lakin kabla hajaanguka kabisa wakamdaka.
Alikufa.
Basi moyo wangu ukafadhaika Sana mpaka nikashtuka usingizini, bado nikiwa nimefadhaika.
Iweje niote mtu aliyekufa kafa tena?
Hii imekaaje kitaalamu.
Na Kwa nini moyo wangu ulifadhaika mno kiasi kile?
Wakati mwaka Jana, nilivyomuota Amekufa sikuwa na wasiwasi na hofu kama hivi leo?
Wataalamu wa tafsiri mje
Ndimi;
Taikon
Usiku wa leo nimefadhaika Sana, nimesononeshwa mno, nimepatwa na uchungu usioelezeka mpaka usingizi ukakata nikaamka yapata saa saba na dakika ishirini na mbili Kwa saa ya ukutani.
Mwaka Jana niliota ndoto ya namna hii hii lakini nikashindwa kuipandisha hapa kutokana na sababu kadha wa kadha, nilimuona Mzee Magufuli amefariki, kisha nikamuota na Mzee mwingine wa CCM naye kafariki Ila huyo Mzee mpaka sasa hivi ninapoongea yupo hai na hi mzima ea Afya. Sitamtaja, Ila ni mstaafu wa CCM katika nafasi ya Ukaribu taifa bara.
Nikirejea kwenye ndoto ya Leo inayonifanya niandike hapa;
Iweje niote mtu aliyekufa kafa tena?
Ndoto inaanzia tukiwa ofisini mahali, nikiwa na watu kadhaa waserikali. Ofisi ilikuwa kubwa yakutosha yenye meza za kisasa, ukutani ikiwepo picha ya Magufuli, pembeni kabisa kwenye dirisha likiwepo Sofa moja la watu Kama watano hivi lenye rangi ya ugoro la ngozi kwenye pembe lilikuwepo Ua sijajua ni ua bandia au ua kabisa.
Waserikali walikuwa watatu Mimi nikiwa wanne. Wawili walikuwa wamesimama, Mimi na mwingine tukiwa tumekaa kwenye viti(sio sofa)
Tukiwa tunapiga soga, punde bila kutarajia mlango wa Ile ofisi ulifunguliwa, akaingia mtu mmoja wa usalama akifuatwa na watu wa nne kisha Magufuli akafuatia. Mioyo yetu wote ikalipuka Sisi tuliokutwa mule ndani.
Mshtuko wetu ulisababishwa na kumuona mtu ambaye tunajua ameshakufa.
Tukiwa wote tumesimama Kama ishara ya heshima na adabu Kwa Rais, bado tukishangaa Magufuli WA kwenye ndoto akatusalimia Kwa matani Kama ilivyo desturi yake.
Kisha baadaye akasema hajafa, kama mtu anayejibu maswali yaliyomo mioyoni mwetu yaliyochorwa katika Sura zetu zenye wasiwasi..
Wakati akiwa anaongea, mlango wa pili unaoingia ndani kabisa kwenye ofisi zile, ukafunguka na akatokea mtu mmoja aliyevalia suti nadhifu akiwa kaongozana na mtu mwingine mwenye mwili wa kawaida Kama wangu. Walipotokea watu hao, nikashangaa kumuona Magufuli akishika katikati ya Kufua, akilalama kichomi, akilalama hivyo Kwa muda.
Mpaka machozi yakawa yanamtoka.
Wale watu aliokuja nao wakawa wanamshika ili kumpa msaada ili wambebe wamtoe pale wampeleke Hospitalini. Lakini akakataa, mwishowe akaanguka chini lakin kabla hajaanguka kabisa wakamdaka.
Alikufa.
Basi moyo wangu ukafadhaika Sana mpaka nikashtuka usingizini, bado nikiwa nimefadhaika.
Iweje niote mtu aliyekufa kafa tena?
Hii imekaaje kitaalamu.
Na Kwa nini moyo wangu ulifadhaika mno kiasi kile?
Wakati mwaka Jana, nilivyomuota Amekufa sikuwa na wasiwasi na hofu kama hivi leo?
Wataalamu wa tafsiri mje
Ndimi;
Taikon