Lema: Mshahara wa Mbunge ni Mdogo sana, 4000$ Kwa mwezi anazidiwa na vijana wanaofanya cryptocurrency

Aliyekuwa mbunge wa Arusha mjini bwana Godbless Lema, katika Mazungumzo huko space twitter alisikika akikwambia Kitila Mkumbo kwamba mshahara wa mbunge ni Mdogo mno yaani ni 4000$ Kwa Mwezi hivyo aache Ubunge amfundishe cryptocurrency apate zaidi ya hiyo maana anazidiwa na vijana wanaoifanya.


Kumbe LEMA anasema mshahara wa mbunge Mdogo ama uongezwe

Britanicca
Napoteza matumaini ninaposikia watu kama Lema wakisema mshahara wa $ 4000 ni mdogo.Matumaini yangu mimi nimekuwa nayaweka kwa CHADEMA kuwa ndiyo wenye lengo la kuikomboa nchi hii kutoka kwenye lindi la umaskini. Kwa bahati mbaya maneno kama hayo nimewahi kuyasikia yakisemwa na Tundu Lissu pia. Swali langu ni kwa nini basi alitaka kufanya kazi ya ubunge huku akijua kuwa mshahara wake ni kidogo. Swali lingine ni udogo huo wa mshahara ni kwa standard gani? Analinganisha na mshahara wa akina nani hapa Tz. Madaktari wanapata kiasi gani. Walimu je wanapata kiasi gani? Asije akataka kulipwa kama mbunge wa Canada huko aliko. Napata wasiwasi kuwa Lema anachogombea sasa si ukombozi wa watz bali wa tumbo lake. Kinachomsukuma sasa ni wivu dhidi ya walio madarakani.
 
Sijui ni watu kuelewa ama la!.

Kwa nilichomuelewa Lema, ni kuwa wale wanaofanya Crypto currency wana-earn more than what MPs earn monthly.

Kwamba, bila shaka kuna vijana wanafanya biashara ya sarafu mtandao ambao kipato chao kwa mwezi ni zaidi ya kipato apatacho Mbunge.

Haimaanishi kuwa kipato cha Mbunge ni kidogo na kinapaswa kuongezwa. La Hasha.

Ila bi kidogo kulinganisha na wapatavyo hao vijana wachache.
Kwa kumshauri aache ubunge ili lema amfundishe sarafu mtandao....alimaanisha nini?
 
Hujamuelewa lema, na hilo kalizuungumza toka wiki iliyopita jumatatu kwenye space, sijui kwa nn umelileta leo

Lema anachosema yeye sio kwamba alikua anataka apate ubunge ili apate pesa Kama walivyo wabunge wengi wa CCM

Yeye alitaka ubunge ili kutumikia watu, maana hiyo pesa ya ubunge kwa mwezi anaweza kuipata kwenye crypto
Ameipata mara ngapi huko aliko?
 
nadharia mkuu sisi tunaijua cryptos
Hahahahaaa..,ukinilipa US dollar 4000 kwa mwezi au ukanipa 100k$ kwa ulazima wa kutrade/kuinvest kwenye cryptos au kutrade forex...nitakubali mshahara wa 4000$ kwa mwezi...cryptos...forex...binary...hahahahaaa.... speculation speculation speculation...not 💯 sure nn kinaenda kutokea sekunde moja ijayo...
 
Du una ushahidi mkuu.
Ndiyo, ushahidi wa kimazingira unaonyesha wazi mhusika wa shambulizi ni JPM! (wanaoweza kubisha ni wasio na akili ya kufikiria tu)

1. Press ya JPM akipokea ripoti ya akina Mruma na Osoro, ilikuwa clear kabisa, ilimlenga Lissu na alitamka wazi wazi hatua za kuchukua dhidi yake...

2. Eneo aliloshambuliwa ni lenye ulinzi mkali wakati wote, mwenye uwezo wa kuwaondoa walinzi siku ya tukio kwa vyovyote vile inahusu Amri kutoka "juu"

3. Baada ya kumshambulia hakuna namna yoyote iliyofanyika kuwakamata wahusika,wala kufunguliwa kesi inayohusiana na tukio lile, (yaani ilichukuliwa kana kwamba aliyepigwa risasi ni mbuzi tu, tena asiye na mwenyewe), kisingizio kikawa "wanamsubiri aliyrshambuliwa aje atoe ushahidi wake, (sababu ya kipumbavu kabisa) kamanda Barrow aliuawa Mwanza, nani aliyetoa ushahidi hata kukamatwa kwa wahusika maeneo mbali mbali ya nchi?

4. Kuna CCTV camera mahususi kwa ajili ya kulinda maeneo lilipotokea shambulizi, nani alizitoa? na kwa nini hazikutumika kama kielelezo cha kwanza kubaini waliohusika na shambulio?

5. Baada ya jaribio la mauaji kushindikana, iliamuriwa avuliwe ubunge, huku pesa yake ya matibabu ikizuiwa (ili afe tu), nani aliyekuwa na mamlaka ya kufanya yote hayo?

Mwenye akili timamu anafahamu, tukio zima la kupigwa risasi kwa Tundu Lissu, lilikuwa na muunganiko wa karibu kabisa na JPM, na alishindwa kuficha chuki yake dhidi ya Lissu akaionyesha wazi wazi kwa matendo baada ya tukio, angekuwa na akili angejitutumua walau kwa kumlipia matibabu na kumlipa stahiki zake kama mbunge,lakini kwa kuwa alikuwa na chuki za kipumbavu akaishia kujichoresha wazi wazi uhusika wake kwenye tukio!

Tuseme yoote, lakini ukweli unabaki kwamba JPM alikuwa na roho mbaya sana kwa "political opponents" wake, na Mungu ametoa fundisho, aliyetaka kuua amekufa yeye na sasa analiwa na funza huko chato,na aliyekusudia kumuua anaishi...

JPM alikuwa muuaji asiye na huruma kabisa, mbaya zaidi aliwalenga wapunzani wake kisiasa tu, wala hata sio wahaini au majambazi kama Sabaya!
 
Ndo maana alikopa sana mwisho wa siku madeni yakawa hayalipiki akakimbilia ulaya akidanganya watu utawala uliokuwepo ulikuwa na nia ya kumwangamiza.

Yaani Lema afuatiliwe na Magufuli kwa lipi? Baada ya Magufuli yupo mama Samia bado hataki kuja! Very stupid guy! Madeni madeni.

Hujui kuwa dhamani ya fedha inaendana na uchumi wa nchi? Canada ukiwa na dollar 8000 na Tz ukiwa na dollar 8000 yupi atafanya mambo makubwa?

Aendelee kuolewa tu na wanaume huko.
Dhamana?
 
Aliyekuwa mbunge wa Arusha mjini bwana Godbless Lema, katika Mazungumzo huko space twitter alisikika akikwambia Kitila Mkumbo kwamba mshahara wa mbunge ni Mdogo mno yaani ni 4000$ Kwa Mwezi hivyo aache Ubunge amfundishe cryptocurrency apate zaidi ya hiyo maana anazidiwa na vijana wanaoifanya.


Kumbe LEMA anasema mshahara wa mbunge Mdogo ama uongezwe

Britanicca
Ssemi-gods at work
 
Sijui ni watu kuelewa ama la!.

Kwa nilichomuelewa Lema, ni kuwa wale wanaofanya Crypto currency wana-earn more than what MPs earn monthly.

Kwamba, bila shaka kuna vijana wanafanya biashara ya sarafu mtandao ambao kipato chao kwa mwezi ni zaidi ya kipato apatacho Mbunge.

Haimaanishi kuwa kipato cha Mbunge ni kidogo na kinapaswa kuongezwa. La Hasha.

Ila bi kidogo kulinganisha na wapatavyo hao vijana wachache.

Exactly, hii ndio maana halisi ya Lema.
 
Aliyekuwa mbunge wa Arusha mjini bwana Godbless Lema, katika Mazungumzo huko space twitter alisikika akikwambia Kitila Mkumbo kwamba mshahara wa mbunge ni Mdogo mno yaani ni 4000$ Kwa Mwezi hivyo aache Ubunge amfundishe cryptocurrency apate zaidi ya hiyo maana anazidiwa na vijana wanaoifanya.


Kumbe LEMA anasema mshahara wa mbunge Mdogo ama uongezwe

Britanicca
Lema kachanganyikiwa sasa.
Hakuna mtu anapelekwa bungeni ili akawe tajiri
Yeye akitaka hela afanye hiyi crypto currency atajirike, uwakilishi wa wananchi waachie wenye moyo huo.
 
Kama ameyasema haya, basi ni mpuuzi!!

Kama kweli kayasema hayo atakuwa mwehu; kwani hizo $4000 anafananisha na mshahara wa nani? Wafanya kazi kama waalimu wanapata mshahara shilingi ngapi? Hiyo anayosema CRYPTOCURRENCY sio ajira ni kamali ya aina inayochezwa kwenye masoko ya fedha; unaweza ukapata au kukosa kutegemeana na utaalam wako . Sio kila mtu anayecheza hiyo michezo ya hizo fedha za kijitari anafanikiwa.
 
Anasema ni pesa ndogo lakini alipambana kufa na kupona ili aupata huo mshahara mdogo.

Kaukosa mpaka leo ana kinyongo, anapambania time huru ya uchaguzi ili imsaidie kushinda apate huo mshahara mdogo
Million 10 kwa mwezi ni hela ambayo akipewa mtu mwenye akili timamu baada ya term moja tu ya ubunge hahitaji tena kuji involve na mambo ya siasa bali ni kutengeneza utajiri wa vizazi na vizazi tu kupitia miradi endelevu.

10M each month + plus 250M end of the term! Mungu akupe nini kingine katika hii dunia?
 
Ndo maana alikopa sana mwisho wa siku madeni yakawa hayalipiki akakimbilia ulaya akidanganya watu utawala uliokuwepo ulikuwa na nia ya kumwangamiza.

Yaani Lema afuatiliwe na Magufuli kwa lipi? Baada ya Magufuli yupo mama Samia bado hataki kuja! Very stupid guy! Madeni madeni.

Hujui kuwa dhamani ya fedha inaendana na uchumi wa nchi? Canada ukiwa na dollar 8000 na Tz ukiwa na dollar 8000 yupi atafanya mambo makubwa?

Aendelee kuolewa tu na wanaume huko.
Kina Azori Gwanda walipotezwa Kwa lipi? Unapomwongelea Mtu mwovu usituulize Sisi atamdhuru Mtu Kwa lipi. Mwovu anajua mwenyewe ya kumdhuru Mtu hata kama wewe unaona ni ndogo.

Sent from my M2003J15SC using JamiiForums mobile app
 
Million 10 kwa mwezi ni hela ambayo akipewa mtu mwenye akili timamu baada ya term moja tu ya ubunge hahitaji tena kuji involve na mambo ya siasa bali ni kutengeneza utajiri wa vizazi na vizazi tu kupitia miradi endelevu.

10M each month + plus 250M end of the term! Mungu akupe nini kingine katika hii dunia?
Kweli ila watu wengi weusi akili ndogo sana! Wapo wengu tu vijana wanapata hela nzuri ila ukiangalia maisha yake!!! Umalaya,Ulevi na ubishoo mwisho wa siku hana la maana! Ni kama huyo Lema madeni kibao kajivika ukimbizi wa kisiasa! Maisha yanahitaji utulivu na kumwomba Mungu!
 
Million 10 kwa mwezi ni hela ambayo akipewa mtu mwenye akili timamu baada ya term moja tu ya ubunge hahitaji tena kuji involve na mambo ya siasa bali ni kutengeneza utajiri wa vizazi na vizazi tu kupitia miradi endelevu.

10M each month + plus 250M end of the term! Mungu akupe nini kingine katika hii dunia?
Lema ni aina ya watunwanaojiona smart sana.

Na sidhani kama hata amefanya chochote kwenye miaka yote 10 ya Ubunge zaidi ya madeni kibao mpaka akakimbia.

Ni mtu anajifanya ana uwezo wa kutengeneza pesa, hana shida ndogo ndogo lakini ukiamwangalia anatia huruma tu.

Siasa in pesa za bure bure, yaani ukikosana nafasi unakuwa Kama Mwehu kabisa.

Mfuatilie Sugu jinsi anavyohangaika, Mara Misuti yangu ilikuwa imezoea mjengoni, Mara niliporwa ushindi nitarudi tu🤣

Mwanasiasa kustaafu Ni mpaka AFE
 
Mtaji keshapata kwa kuwa mbunge kwa miaka 10.

Afanye biashara aachane na siasa.

Sio vizuri kuendelea kudanganya watu wakati anafahamu kabisa kuwa hana nia ya kuwasaidia bali anaangalia maslahi tu.
 
Back
Top Bottom