Lela Mussa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar: Rais Samia anastahili kupewa Uprofesa

Nyafwili

JF-Expert Member
Nov 27, 2023
2,774
6,885
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Mohammed Mussa amesema kwa kazi kubwa ambayo Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa akiifanya tangu ashike hatamu ya Urais, anastahili kupewa Uprofesa.

Lela ameongea hayo mbele ya Rais Samia leo December 28,2023 wakati wa Hafla ya Mahafali ya 19 ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) ambapo Chuo hicho ambacho Mkuu wake ni Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi, kimemtunuku Rais Samia Shahada ya Uzamivu ya Heshima ya Utalii na Usimamizi wa Masoko kwa kutambua mchango wake wa kuifungua Nchi kiuchumi kupitia Sekta ya Utalii.

Lela amenukuliwa akisema “Nataka niungane na wote ambao wametoa wasifu wa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa anastahili kupewa tuzo na sio tu katika ngazi ya PhD lakini kwa kazi kubwa ambayo amekuwa akiifanya tangu ashike hatamu anastahili Uprofesa”

“Uthubutu mkubwa ambao amekuwa akionesha katika uongozi wake, ukomavu wa kisiasa na uvumilivu wa hali ya juu ni zaidi ya PhD na niliuliza wakati linakuja wazo la kuwa anataka kupewa PhD nikauliza kwani haiwezekani kumpa Uprofesa moja kwa moja tukamaliza kazi, nikaambiwa kuna taratibu zake lakini Mheshimiwa (Rais Samia) tutazishughulikia”

“Kwa Mh. Rais Samia hii ni PhD ya tatu ametunukiwa tangu awe Rais wa Tanzania, ya kwanza alikabidhiwa UDSM na Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete na leo hapa anakabidhiwa na Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi lakini ya pili alikabidhiwa nchini India na alipopewa akasema anawazawadia Mabinti wa Tanzania”
Screenshot_20231228-144517.png
 
La msingi hawezi kumzidi mwanangu Idd Amin kwa vyeo.
His Excellency, President for life, Field Marshal Al Hadji Doctor Idi Amin Dada, VC, DSO, MC, Lord of all Beasts of the Earth and the Fishes of the Sea and the Conqueror of the British Empire in Africa in General and Uganda in particular
 
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Mohammed Mussa amesema kwa kazi kubwa ambayo Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa akiifanya tangu ashike hatamu ya Urais, anastahili kupewa Uprofesa.

Lela ameongea hayo mbele ya Rais Samia leo December 28,2023 wakati wa Hafla ya Mahafali ya 19 ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) ambapo Chuo hicho ambacho Mkuu wake ni Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi, kimemtunuku Rais Samia Shahada ya Uzamivu ya Heshima ya Utalii na Usimamizi wa Masoko kwa kutambua mchango wake wa kuifungua Nchi kiuchumi kupitia Sekta ya Utalii.

Lela amenukuliwa akisema “Nataka niungane na wote ambao wametoa wasifu wa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa anastahili kupewa tuzo na sio tu katika ngazi ya PhD lakini kwa kazi kubwa ambayo amekuwa akiifanya tangu ashike hatamu anastahili Uprofesa”

“Uthubutu mkubwa ambao amekuwa akionesha katika uongozi wake, ukomavu wa kisiasa na uvumilivu wa hali ya juu ni zaidi ya PhD na niliuliza wakati linakuja wazo la kuwa anataka kupewa PhD nikauliza kwani haiwezekani kumpa Uprofesa moja kwa moja tukamaliza kazi, nikaambiwa kuna taratibu zake lakini Mheshimiwa (Rais Samia) tutazishughulikia”

“Kwa Mh. Rais Samia hii ni PhD ya tatu ametunukiwa tangu awe Rais wa Tanzania, ya kwanza alikabidhiwa UDSM na Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete na leo hapa anakabidhiwa na Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi lakini ya pili alikabidhiwa nchini India na alipopewa akasema anawazawadia Mabinti wa Tanzania”
View attachment 2855480
Hii nchi inavituko sana, 😀, kwa kazi ipi aliyo Ifanya??
 
Ona hii shenzi na pua lake kama "gambuti" la kisukuma kuiweka nchi gizani na kushusha uchumi wa nchi na wananchi ndio kazi kubwa 🤔🤔 shenzi kabisa 😡
Basi mkuu, usiwe na hasira sana... 2025 muhimu kupunguza idadi ya viongozi kutoka CCM,
 
Kila siku nazidi kuelewa, kauli ya Prof Assad, kuwa "asilimia 60 ya watumishi wa umma, ni vilaza, wajinga, hawana uwezo"
Na alipendekeza, ni Bora kupiga chini wote, uanze upya na asilimia 40 iliyobaki.
 
Back
Top Bottom