Lamination mizigo airport Mwanza, ufisadi mpya

Lamination mizigo airport Mwanza, ufisadi mpya

JEKI

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2013
Posts
4,845
Reaction score
2,966
Nimejiuliza sana, kwanini lamination ya mizigo inayodhaniwa inaweza kuchafua ndege mfano ndoo ya samaki iwe lazima kufanyiwa lamination tena kwa gharama kubwa vile?

Abiria umefunga vizuri samaki zako kwenye ndoo safi lakini unalazimishwa kufanya lamination.

Kama wenye ndege hawataki kuchafua ndege yao basi wao ndo wawajibike kutengeneza sehemu ya kuhifadhia mizigo michafu.

Siku moja nimeunganisha kibox na kindoo kidogo nikaambiwa lamination ni 15,000 ilihali mzigo mmoja ni 5,000.

Halafu mbona Mwanza tu ndo wenye hizi lamination?? Au hii ni biashara ya nani??.
 
Kuna watu vichwa ngumu kweli..kwa hiyo unataka mizigo yako ipige michoro kwenye bodi unadhani hiyo ni vitz..koma kabisa..unadhani wao wameenda shule bure..labda ungesema air Tanzania waanze utaratibu wa kuuza vifungashio maalumu ya mizigo yetu kuepuka uharibifu na usumbufu.
 
Majibu ya baadhi ya watu kwa mtoa mada, yanaonyesha kiwango cha busara alichonacho mtu... MZIGO WENYE THAMANI YA 5,000/- Nilazimishwe kuweka lamination ya 15,000/-... Mapovu yenu yatoeni kwa uhalisia, si kisa wewe unapenda usafi..... kila mtu akileta akipendacho kule hakuna atakayesafiri... MAANA WENGNE HAWAPENDI KUSAFIRI NA WATU WENGINE

1. KWANI HAKUNA LAMINATION YENYE BEI CHINI YA HAPO?...
2. Kwani hawawezi kuangalia kiasi gani cha LAMINATION kitumike kwenye mzigo upi?... Maana kimzigi kidogo hakiwezi kuwa sawa na mzigo mkubwa unaotumia lamiation zaidi.

By the way, sitashangaa kusikia mmoja au zaidi, waliotoa majibu hayo hawajawahi kusafiri na ndege na kukutana na adha hiyo
 
Daladala tu wakali mno ukibeba samaki wanaogopa Basi lao kunuka shombo la samaki sembuse ndege.Mleta mada unapaswa ujue harufu ya misamaki yako yaweza rukia kwenye mizigo na mabegi ya watu wastaarabu .Mtu anashuka airport anabeba begi lake linanuka samaki wakati yeye hakubeba samaki.mindoo yako ujue inawekwa sehemu Moja na mizigo mingine.Hiyo laminationi Ni ya kudhibiti harufu pia isirukie mizigo mingine shirika likapoteza frequent flyers Kama sisi kisa midoo yako na vibox vyako vya samaki
 
Majibu ya baadhi ya watu kwa mtoa mada, yanaonyesha kiwango cha busara alichonacho mtu... MZIGO WENYE THAMANI YA 5,000/- Nilazimishwe kuweka lamination ya 15,000/-... Mapovu yenu yatoeni kwa uhalisia, si kisa wewe unapenda usafi..... kila mtu akileta akipendacho kule hakuna atakayesafiri... MAANA WENGNE HAWAPENDI KUSAFIRI NA WATU WENGINE

Haijalishi thamani ya mzigo wako.

Ina maana kama nafanyia lamination blovk ya gold intakiwa nilipe milioni 50?
 
Majibu ya baadhi ya watu kwa mtoa mada, yanaonyesha kiwango cha busara alichonacho mtu... MZIGO WENYE THAMANI YA 5,000/- Nilazimishwe kuweka lamination ya 15,000/-... Mapovu yenu yatoeni kwa uhalisia, si kisa wewe unapenda usafi..... kila mtu akileta akipendacho kule hakuna atakayesafiri... MAANA WENGNE HAWAPENDI KUSAFIRI NA WATU WENGINE
Kwa hiyo makorokocho yako yasifuate utaratibu kisa thamani yake?
 
Daladala tu wakali mno ukibeba samaki wanaogopa Basi lao kunuka shombo la samaki sembuse ndege.Mleta mada unapaswa ujue harufu ya misamaki yako yaweza rukia kwenye mizigo na mabegi ya watu wastaarabu .Mtu anashuka airport anabeba begi lake linanuka samaki wakati yeye hakubeba samaki.mindoo yako ujue inawekwa sehemu Moja na mizigo mingine.Hiyo laminationi Ni ya kudhibiti harufu pia isirukie mizigo mingine shirika likapoteza frequent flyers Kama sisi kisa midoo yako na vibox vyako vya samaki
Tatizo lipo namna mlivyomuelewa mtoa mada... hamaanishi yasifungwe, ANAMAANISHA GHARAMA SI HALISIA...
 
Majibu ya baadhi ya watu kwa mtoa mada, yanaonyesha kiwango cha busara alichonacho mtu... MZIGO WENYE THAMANI YA 5,000/- Nilazimishwe kuweka lamination ya 15,000/-... Mapovu yenu yatoeni kwa uhalisia, si kisa wewe unapenda usafi..... kila mtu akileta akipendacho kule hakuna atakayesafiri... MAANA WENGNE HAWAPENDI KUSAFIRI NA WATU WENGINE

1. KWANI HAKUNA LAMINATION YENYE BEI CHINI YA HAPO?...
2. Kwani hawawezi kuangalia kiasi gani cha LAMINATION kitumike kwenye mzigo upi?... Maana kimzigi kidogo hakiwezi kuwa sawa na mzigo mkubwa unaotumia lamiation zaidi.

By the way, sitashangaa kusikia mmoja au zaidi, waliotoa majibu hayo hawajawahi kusafiri na ndege na kukutana na adha hiyo
Kama huna hela panda basi acha kulalamika, wasukuma mkoje lakini?
 
Nadhani wanakomaa zaidi kwenye mizigo yenye possibility ya kuvuja (mfano samaki wabichi waliowekwa kwenye mabarafu) pia na hata samaki waliokaangwa na kuwekwa kwenye box ila dalili ya mafuta kuanza kuonekana. Wanafanya hivi pia kulinda mizigo ya abiria wengine isiharibike. Kumbuka sote ni abiria sawa na lazima haki itendeke

Next time nunua samaki wengi ili 15 000/= iwe justified. Lakini pia ukifanya lamination kwa mzigo wako unakuwa na amani angalau kidogo kwamba wadokozi hawatafanya yao
 
Tatizo lipo namna mlivyomuelewa mtoa mada... hamaanishi yasifungwe, ANAMAANISHA GHARAMA SI HALISIA...
Ndege sio.ya kupanda malofa yaani anabweka kulalamikia elfu 15? Aisee .Au tiketi alikatiwa na mwajiri? Kelele hizi huyu atakuwa mfanyakazi.Mtu Mwenye pesa Yake anakata tiketi Malaki kwake elfu 15 is nothing.Kelele hizi Ni za wakatiwa tiketi.Huwa wanaji shebudua Sana utasikia ohh poor service ,too expensive nk kelele na mbwembwe nyingiiiii.Siku ingine usipande ndege panda Fuso kule Wala huhitaji kufanya lamination
 
Ndege sio.ya kupanda malofa yaani anabweka kulalamikia elfu 15? Aisee .Au tiketi alikatiwa na mwajiri? Kelele hizi huyu atakuwa mfanyakazi.Mtu Mwenye pesa Yake anakata tiketi Malaki kwake elfu 15 is nothing.Kelele hizi Ni za wakatiwa tiketi.Huwa wanaji shebudua Sana utasikia ohh poor service ,too expensive nk kelele na mbwembwe nyingiiiii.Siku ingine usipande ndege panda Fuso kule Wala huhitaji kufanya lamination
Sikukuu njema
 
Mimi siku ya kwanza nilishangaa mbona bei ghali hivyo mana nililipa 16000,hiyo machine ni mtu kaweka hapo anagawana na mkubwa hapo airport yani ni ufisadi
Nimejiuliza sana, kwanini lamination ya mizigo inayodhaniwa inaweza kuchafua ndege mfano ndoo ya samaki iwe lazima kufanyiwa lamination tena kwa gharama kubwa vile?

Abiria umefunga vizuri samaki zako kwenye ndoo safi lakini unalazimishwa kufanya lamination.

Kama wenye ndege hawataki kuchafua ndege yao basi wao ndo wawajibike kutengeneza sehemu ya kuhifadhia mizigo michafu.

Siku moja nimeunganisha kibox na kindoo kidogo nikaambiwa lamination ni 15,000 ilihali mzigo mmoja ni 5,000.

Halafu mbona Mwanza tu ndo wenye hizi lamination?? Au hii ni biashara ya nani??.
 
Back
Top Bottom