Kweli hali ya pesa ni ngumu

Kweli hali ya pesa ni ngumu

Kuna kiwanja cha jirani yangu kiko wazi. Nilimuuliza malengo yake aliniambia kwa kweli tangu mzee wake aondoke duniani ramani yake haisomeki. Mzee alikua Don serikalini. Nilimgusia kama anaweza kuniuzia hiyo ilikua 2012 aliniambia nimpe milioni 60. Mume wangu aliniambia kwa bei hiyo achana nae.

Juzi amenitumia ujumbe tukutane tuongee. Tulipokutana anasema yuko tayari kwa milioni 3 tuamdikishiane anipe kiwanja. Hapa nilipo sijaamini nilichokisikia.

Nataka kiwanja..hebu tuambizane jaman...
 
Kuna kiwanja cha jirani yangu kiko wazi. Nilimuuliza malengo yake aliniambia kwa kweli tangu mzee wake aondoke duniani ramani yake haisomeki. Mzee alikua Don serikalini. Nilimgusia kama anaweza kuniuzia hiyo ilikua 2012 aliniambia nimpe milioni 60. Mume wangu aliniambia kwa bei hiyo achana nae.

Juzi amenitumia ujumbe tukutane tuongee. Tulipokutana anasema yuko tayari kwa milioni 3 tuamdikishiane anipe kiwanja. Hapa nilipo sijaamini nilichokisikia.
Sasa cha kufanya we mwambie una laki nane au maximum 1m iko hapo kwenye mfuko wa shati sasa hivi, aje na mashahidi na dokomenti zote msainishane. Hata ukija kugundua umelizwa, utakua hujatoboka sana mfuko.
 
Ila viwanja vya uridhi kama hivyo wakati unanunua hakikisha ukoo mzima unasign lasivyo...utakuja kuchezea makofi kutoka kwa mzee baba
 
Ni kweli bei za viwanja zimeshuka sana kipindi hiki, ila bado watu wanauza na kununua kama kawaida.

Hata nyumba za kupanga zimeshuka bei ila wateja wapo wengi kama zamani.

Ni wapi ulipo hakuna wapangaji?

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijasema hakuna wapangaji, nimesema upatikanaji wa chumba/nyumba ni rahisi tofauti na miaka ya nyuma ukitaka udalali umependa tu maana matangazo ni mengi nyumba inauzwa wakati miaka ya nyuma hupati bila dalali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Temana nacho da mkubwa, juzi kati hapa nimeshuhudia nyumba zikivunjwa maeneo ya Olasiti Arusha mambo ya mirathi tena kwa wamasai ambao wao kwa mila yao mwanamke harithi kitu ila alishinda dada kesi na wote waiokuwa wameuziwa na kujenga mabungalow yao palivunjwa kama masihara watu walikua wanazimia kama mbu waliopuliziwa HIT ⚡
Olasiti sehemu gani,nina eneo huko halafu niko mbali
 
Mkuu uthamani wa kiwanja hupandishwa na fikra za kusadikika, kutokana na hadhi iliyopewa eneo.

Millioni3 ni nyingi sana kununua plain surface, isiyo na kipande hata cha jiwe la msingi, lipia, umiliki, M/Mungu kakupunguzia mkandamizo wa awali, acha kukenua meno kushereheke.
Muziki utaucheza kwenye ujenzi.

Tena usistaajabie sana, saazingine shida hazina adabu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaona mbali mkuu,kuna nyakati ukinunua mali ya dizaini hii inaweza kuwa kama na mikosi flani hivi kwa kuwa jamaa hauzi kwa kupenda. Pili inaweza kuwa kabla ya kifo cha mzee alitoa kauli kuwa nikifa isiuzwe mali yangu yeyote sasa dogo uvumilivu umemshinda,ukichukua unaweza hata shindwa kukiendeleza
 
Kuna kiwanja cha jirani yangu kiko wazi. Nilimuuliza malengo yake aliniambia kwa kweli tangu mzee wake aondoke duniani ramani yake haisomeki. Mzee alikua Don serikalini. Nilimgusia kama anaweza kuniuzia hiyo ilikua 2012 aliniambia nimpe milioni 60. Mume wangu aliniambia kwa bei hiyo achana nae.

Juzi amenitumia ujumbe tukutane tuongee. Tulipokutana anasema yuko tayari kwa milioni 3 tuamdikishiane anipe kiwanja. Hapa nilipo sijaamini nilichokisikia.
Million 60 mpaka million 3...🙄🙄🙄?

Yaani punguzo la bei ni asilimia 95..... inaonyesha jamaa ana shida ya haraka ya hela.
 
Million 60 mpaka million 3...🙄🙄🙄?

Yaani punguzo la bei ni asilimia 95..... inaonyesha jamaa ana shida ya haraka ya hela.
Hakuna kitu kama hiki. Kiwanja cha 60m miaka hio hata sasa hivi hakiwezi kushuka chini ya 30m. Kwanza kiwanja cha bei hio huwa kinakuwa yale maeneo yasiyoshuka thamani.

Hali hii imesababisha viwanja au nyumba kwenye prime areas zisiuzike kwasababu mwenye Mali hawezi kushuka chini ya bei fulani na hela ya bei aitakayo watu hawako tayari kutoa.
 
Cha kusikitisha zaidi ukute na wewe huna hiyo hela
Kuna kiwanja cha jirani yangu kiko wazi. Nilimuuliza malengo yake aliniambia kwa kweli tangu mzee wake aondoke duniani ramani yake haisomeki. Mzee alikua Don serikalini. Nilimgusia kama anaweza kuniuzia hiyo ilikua 2012 aliniambia nimpe milioni 60. Mume wangu aliniambia kwa bei hiyo achana nae.

Juzi amenitumia ujumbe tukutane tuongee. Tulipokutana anasema yuko tayari kwa milioni 3 tuamdikishiane anipe kiwanja. Hapa nilipo sijaamini nilichokisikia.
 
Back
Top Bottom