Kweli hali ya pesa ni ngumu

Kweli hali ya pesa ni ngumu

Kuna kiwanja cha jirani yangu kiko wazi. Nilimuuliza malengo yake aliniambia kwa kweli tangu mzee wake aondoke duniani ramani yake haisomeki. Mzee alikua Don serikalini. Nilimgusia kama anaweza kuniuzia hiyo ilikua 2012 aliniambia nimpe milioni 60. Mume wangu aliniambia kwa bei hiyo achana nae.

Juzi amenitumia ujumbe tukutane tuongee. Tulipokutana anasema yuko tayari kwa milioni 3 tuamdikishiane anipe kiwanja. Hapa nilipo sijaamini nilichokisikia.
Mpe tu huko ccm hali ni mbaya sana,utapata thawabu kwa shetani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu awamu hii kuna nyumba, viwañja vinauzwa wateja hakuna hata madalali hawana maana nyumba za kupanga nyingi zipo wazi

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli bei za viwanja zimeshuka sana kipindi hiki, ila bado watu wanauza na kununua kama kawaida.

Hata nyumba za kupanga zimeshuka bei ila wateja wapo wengi kama zamani.

Ni wapi ulipo hakuna wapangaji?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiwanja toka 60M hadi 3M na thamani ya ardhi mara zote inapandaga kila uchao.
Just do it kama unabet vile
Awamu hii ardhi haina thamani. Kila siku watu wanatulilia wanataka walau 3M ili watoe 600 sqm


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Na huyo mumeo ni mimi
Kuna kiwanja cha jirani yangu kiko wazi. Nilimuuliza malengo yake aliniambia kwa kweli tangu mzee wake aondoke duniani ramani yake haisomeki. Mzee alikua Don serikalini. Nilimgusia kama anaweza kuniuzia hiyo ilikua 2012 aliniambia nimpe milioni 60. Mume wangu aliniambia kwa bei hiyo achana nae.

Juzi amenitumia ujumbe tukutane tuongee. Tulipokutana anasema yuko tayari kwa milioni 3 tuamdikishiane anipe kiwanja. Hapa nilipo sijaamini nilichokisikia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu uko sahihi zaidi. nmewahi kununua shamba kikaniletea dhahama kama hzo ila mwisho wa siku nlikipata, na kufidiwa gharama zangu za usumbufu, since then nko makini sana!
Haya mambo ya urithi sijui mirathi ni ujinga mtupu na kupotezeana muda..mimi kuna sehemu niliacha mpaka hicho kibanda. Kuna mahala nikanunua shamba kama hekari 15 nikalipa kwa mwenye mali mbele ya ushahidi wa serikali ya kijiji. Alivyokufa mzee wao kukazuka kuwa ndani ya mali za kugawana na shamba langu lipo nikaona hawa wataniumiza nikamtafuta mtu nikampiga nalo tena mahakamani kwa document za ushahidi wa kijiji. Huyu anachekelea kutoka 60 mpk 3M. Akianza kwenda mahakamani atajutia uamuzi wake. Ila tumpe ushauri ataelewa kama ana tabia kama za kenge mpk atoke damu masikioni tupo hapa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watz mnapenda sana rushwa na ubwerere. Kaza raisi Magu. Mimi nikiwa raisi mtakula mchanga. Fanya kazi
 
Kuna kiwanja cha jirani yangu kiko wazi. Nilimuuliza malengo yake aliniambia kwa kweli tangu mzee wake aondoke duniani ramani yake haisomeki. Mzee alikua Don serikalini. Nilimgusia kama anaweza kuniuzia hiyo ilikua 2012 aliniambia nimpe milioni 60. Mume wangu aliniambia kwa bei hiyo achana nae.

Juzi amenitumia ujumbe tukutane tuongee. Tulipokutana anasema yuko tayari kwa milioni 3 tuamdikishiane anipe kiwanja. Hapa nilipo sijaamini nilichokisikia.
Kiwanja kiko sehemu gani na kina vipimo gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu uthamani wa kiwanja hupandishwa na fikra za kusadikika, kutokana na hadhi iliyopewa eneo.

Millioni3 ni nyingi sana kununua plain surface, isiyo na kipande hata cha jiwe la msingi, lipia, umiliki, M/Mungu kakupunguzia mkandamizo wa awali, acha kukenua meno kushereheke.
Muziki utaucheza kwenye ujenzi.

Tena usistaajabie sana, saazingine shida hazina adabu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pamoja na kwamba upatikanaji wa pesa nchini umekuwa mgumu lakini kwa vyovyote vile kiwanja cha milioni 60 mwaka 2012 leo hii hakiwezi kuwa kimeshuka thamani hadi kufikia kuuzwa milioni tatu! Angalau ingeeleweka bei kuwa hata milioni 30 au 20 lakini siyo huko kwenye milioni 3. Hicho kiwanja kitakuwa na changamoto zake kwenye umiliki na ukinunua bila kujiridhisha kwa 100% kama hakina mgogoro wowote wa kifamilia baadae utakuja kujutia.
 
milion 60 mpaka milion 3 na wewe unaamini kabisa, iko siku utauziwa jengo la Mlimani City u kwa laki 5 utanunua kweli, nyie ndio mnaotapeliwa , huyo ana nia anashimda na hiyo ela, na hicho kiwanja kitakuletea migogoro tu ya familia,
 
Back
Top Bottom