Kwaya ya Barabara ya 13 Ulyankulu

Kwaya ya Barabara ya 13 Ulyankulu

Hawa watu waliimba wakiongozwa na Roho wa Mungu ndio maana nyimbo hizi zina uhai kama Biblia.
 
Mkuu Sikonge

Mkuu wangu Usharika wa KKKT Mjini Kati ulikuwa na kwaya mbili zilizotikisa anga za muziki wa Injili enzi hizo.Ilikuwepo kwaya ya vijana au ukipenda Uinjilisti ambayo ilikuwa inakwenda Nairobi na kugharamiwa kila kitu na Rais wa Kenya Mzee D Arap Moi,kumbuka enzi hizo uhusiano baina ya Tanzania na Kenya haukuwa mzuri baada ya kuvunjika EAC mwaka 1977 mpaka wa Namanga ulifungwa lakini utashangaa kwaya ya Uinjilisti ilikuwa inakwenda Nairobi bila taabu yoyote.Wakati huo kwenda Nairobi ilikuwa shughuli pevu kidigo hadi Mzee Mwinyi,Moi na Museveni walipoamua kuanzisha tena ushirikiano wa Afrika Mashariki.Kwaya ya Uinjilisti ilikuwa na waalimu wengi bahati mbaya leo siwakumbuki wote lakini nitakupatia wasifu wa kila mwalimu aliyepitia hapo kuanzia Mwl Mjema,Msuya .......na mwaka walioingia pamoja na nyimbo walizotunga kuna baadhi ya nyimbo za Kwaya ya Uinjilisti zimeingizwa katika kitabu rasmi cha nyimbo za kanisa la KKKT "Mwimbieni Bwana" nitazitafuata pia bahati mbaya kitabu cha Mwimbieni Bwana sinacho leo.Ni kweli kwaya ilikuwa na waalimu wazuri waliosomea fani ya muziki nje ya nchi hasa Ujerumani magharibi wakati huo.

Ilikuwepo tena kwaya nyingine kali hapo mjini kati ikijulikana zaidi kama Kwaya Kuu hii nayo ilikuwa ikikimbizana sana na kwaya Uijilisti ni kwaya kongwe haswa ilianzishwa miaka ya 70s nayo ilikuwa ikirekodi nyimbo zake nchini Kenya Mzee Moi pia alikuwa akiwaalika sana hasa kipindi cha siku yake ya kuzaliwa na sikuuu nyingine za kiserekali.Mpiga solo wa Kwaya Kuu alikuwa jamaa mmoja akiitwa Sheggy yeye alikuwa akipiga copy za muziki wa majuu hotel 77 baada Kanda Bongo Man alipokuja Tanzania alimzimikia sana akamchukua katika maonyesho yake mbali mbali nchini na nje ya nchi sijui siku hizi yuko wapi jamaa alikuwa balaa katika mpini wa solo magita yote alikuwa akiyamudu sana labda ulikuwa unamzunguzia huyu alikuwa akjipenda sana.Kuna Mwingine jina limenitoka yeye alikuwa akipiga bass gita kabla ajajiunga na kwaya kuu alikuwa akipiga Maquiz enzi za Babu Seya akitamba sana hapa nchi.Nimejaribu kukupa kahistoria kafupi ili ujue hizi kwaya zilikuwa juu kiasi gani

Jambo lingine muhimu wimbo wa Kila mtu atauchukua mzigo wake mwenyewe ulishinda tunzo ya dhahabu baada ya kufanya vizuri katika mauzo kwa zaidi ya miaka kumi mfululuzo.Tunzo hiyo ilileta mgogoro kidogo baada ya Mwalimu na mtunzi wa mwimbo huo kudai alistahili kupewa tunzo hiyo na si Kwaya ya Uinjilisti mgogoro ulitatuliwa na mahakama na tunzo kubaki kama mali ya kanisa kwasababu vyombo,waimbaji na kwaya ni mali ya kanisa.Tunzo ya dhahabu uambatana na fungu zito kiasi sikumbuki ilikuwa ni kiasi gani.

Mchg Mtango ni marehemu baada ya kustaafu akahamia Dodoma mauti yalimkuta akiwa ameshahama Arusha.Huyu alikuwa mchungaji wa kanisa la Anglikan Kaloleni ana vijana wake wana kwaya wazuri sana wanapiga vyombo kama akina Fred na mwingine ni taabibu ni mwalimu wa kwaya mzuri sana.Kuna mjukuu wake mwingine yeye ndiye aliyepiga vyombo na kuupangilia muziki wa Beatrice Mhone mwanakwaya wa kizazi kipya kama umewahi kuusikiliza wimbo wa "Ingoje safari", "Kijito cha Utakaso....... huyu kijana alishiriki haswa tatizo watu wanamjua Beatrice tu kwakuwa kaimba lakini nyuma ya pazia wapo wataalamu waliomfikisha juu sana huyu Dada ingawa hawajulikani.

Mkuu wangu nitawasiliana na uongozi wa kwaya wakinipatia jina la hicho kinanda nitawasilisha mara moja.Nipatie muda kidogo nitakutumia wasifu wa kila Mwalimu wa hizi kwaya akiwemo mwalimu aka Madevu.

Natanguliza shukrani.


Ngongo asante kwa maelezo ila hebu subiri kidogo nikusumbue maana mie siyo mwenyeji tena Arusha.

Nakumbuka kulikuwa na Waalimu wawili wakali sana wa Kwaya KKKT hapo Arusha. Mmoja alikuwa anasemekana ni mtu aliyesomea Music kwelikweli na alikuwa na kichuma fulani cha kutune sauti wakati anaimbisha. Nimekisahau hicho chuma ila kipo hata kwenye Physics somo la SOUND. Huyu jamaa kama sikosei kwaya yao ilishinda kwenye mashindao ya Kwaya za Arusha mwaka 1988 kama sikosei yaliyofanyikia TENGERU huku watu wakiwatakia heri maana huko Dar, kulikuwa na Mwalimu Mbajo aliyekuwa akiogopwa sana kwa ufundi na utundu wake kwenye kwaya. Huyu Mwalimu alikuwa au wa Kijenge au Tengeru, sina uhakika kwa sasa maana miaka mingi.

Pia alikuwepo mwingine mwenye Madevu aliyekuwa Mwalimu wa kwaya ya kanisa kuu kama sikosei (kubwa lililokupo mjini). Nilikuwa nawapenda sana na kwaya yao hawa jamaa ila nilikuwa nasita kwenda kanisani hapo kusali kwani ukifika muda wa kutoa sadaka, ndiyo utagundua jinsi ulivyo masikini. Mie na hela yangu ya uanafunzi, nikaamua kukimbilia kanisa la Mzee Mtangoo (@Stephen Mtangoo, huyu ni Babu yako? Nakumbuka ile story ya kuku akisema "kamata nambaaa") na Mzee yule wa Kigogo alivyoniona tu akanifuata na kuongea na mimi na akasema ingawa mie ni Moravian na hapo Arusha hakuna Moravian, basi ananikaribisha sana kwake. Hapo nilijisikia kweli nyumbani ingawa walikuwepo matajiri pia kama Mzee Mollel sijui (Owner wa Tanalec, kampuni ya kutengeneza majiko na vifaa vya umeme) ila wengi walikuwa ni watu wa mikoa kama ya Dodoma, Singida na Iringa, masikini wenzangu.
Huyu Mwalimu wa hii kwaya mwenye madevu kwa kweli nilikuwa nampenda kwa sababu nyimbo zake zilikuwa zimetulia sana na Classic. kuna Kaseti walirekodi miaka hiyo ya 80 mwishoni kabisa na nilisikia tu baadhi ya nyimbo zake walipokuja Arusha Tech kuimba ila bahati mbaya sikubahatika kununua kaseti zao. Hii kwaya ya Mzee wa midevu ilikuwa inaitwaje? Ukisinisaidia hilo jina utakuwa umenisaidia sana kuzipata nyimbo zao. Ahhh, walikuwa wanampiga gitaa kijana mmoja ameweka Curl nywele zake...... na alikuwa akipigia gitaa sijui Band gani ya muziki hapo Arusha.

Again: Asante kwa maelezo yako ambayo naona wewe u mwenyeji kweli kweli wa Arusha.

BTW: Unaweza kunitumia jina la hicho kinanda na kifaa kinachokosekana/kilichoharibika kwenye Email? Naweza kujaribu kuwaulizia jamaa zangu fulani huko labda wataweza kukitafuta au hata kukitengeneza. Siahidi lolote zaidi ya kusema ntajaribu kama itawezekana.
 
Ngongo,

Sasa nina uhakika kuwa ilikuwa KWAYA KUU. Walikuwa na wimbo wao mmoja hadi leo naukumbuka maneno kadhaa ingawa nilisikia mara moja tu. "Njooni tumwimbie bwana......" ambao waliimba kwenye nyimbo zao za miaka ya 80 mwishoni. Huyu Mpiga gitaa atakuwa ni huyo Sheggy kijana mmoja anayejipenda sana na kweli alikuwa akipiga solo vizuri sana. Pia Mpiga BASS nilikuwa nimemsahau, ndiyo alikuwa mpiga Bass wa kwanza ambaye nilimuona akipiga Bass kama Professional wote duniani, yaani anapiga kwa kutumia vidole vitatu vya katikati vikiwa vyote vimeelekewa chini. Nilisimama na kuwa namshangaa upigaje wake huo wa ajabu huko Tengeru kwenye mashindao.

Mwaka huo Kwaya Kuu hawakushiriki mashindano, nafikiri ili kuwaachia kwaya nyingine wawakilishe Kanisa. Mwalimu wa hii Kwaya ndiyo alikuwa huyo jamaa mwenye Madevu. Tulikuwa na uhusiano mzuri sana na Kwaya Kuu na hasa ukichukulia kwa miaka nikiwa hapo, Mwenyekiti wa UKWATA Mkoa wa Arusha walikuwa vijana wa TCA. Pia hii ilifanya hata Chuo pia kikawa karibu sana na Askofu Alpha Mohamed na gari lake la Alpha Romeo 🙂

Basi ntamuagiza Mdogo wangu akija hapo Arusha mjini, anitafutie hiyo kaseti ya hii Kwaya Kuu.

Siku hizi wamebaki Wakata viuno na Ndombolo zao majukwaani. Anyway, wakati ukuta, ukipigana nao..... Itafika muda watu watawakumbuka hata Wapiga ndombolo Makanisani na kuwasifu na kusema, hawa wa siku hizi (mwaka sijui 2050) ndiyo wabovu sana heri yao........

Nakusubiri kwenye kesi ya Kinanda na habari zaidi.

Naburudika sasa tayari: Kwaya kuu Arusha - YouTube
Mkuu Sikonge
Ilikuwepo tena kwaya nyingine kali hapo mjini kati ikijulikana zaidi kama Kwaya Kuu hii nayo ilikuwa ikikimbizana sana na kwaya Uijilisti ni kwaya kongwe haswa ilianzishwa miaka ya 70s nayo ilikuwa ikirekodi nyimbo zake nchini Kenya Mzee Moi pia alikuwa akiwaalika sana hasa kipindi cha siku yake ya kuzaliwa na sikuuu nyingine za kiserekali.Mpiga solo wa Kwaya Kuu alikuwa jamaa mmoja akiitwa Sheggy yeye alikuwa akipiga copy za muziki wa majuu hotel 77 baada Kanda Bongo Man alipokuja Tanzania alimzimikia sana akamchukua katika maonyesho yake mbali mbali nchini na nje ya nchi sijui siku hizi yuko wapi jamaa alikuwa balaa katika mpini wa solo magita yote alikuwa akiyamudu sana labda ulikuwa unamzunguzia huyu alikuwa akjipenda sana.Kuna Mwingine jina limenitoka yeye alikuwa akipiga bass gita kabla ajajiunga na kwaya kuu alikuwa akipiga Maquiz enzi za Babu Seya akitamba sana hapa nchi.Nimejaribu kukupa kahistoria kafupi ili ujue hizi kwaya zilikuwa juu kiasi gani

Mkuu wangu nitawasiliana na uongozi wa kwaya wakinipatia jina la hicho kinanda nitawasilisha mara moja.Nipatie muda kidogo nitakutumia wasifu wa kila Mwalimu wa hizi kwaya akiwemo mwalimu aka Madevu.

Natanguliza shukrani.
 
Mkuu Sikonge

Masahihisho kidogo kinanda kilitengenezwa Italy na hapa Tanzania hivyo vinanda vilikuja viwili tu kimoja kwaya ya Uinjilisti na kingine Kwaya ya St Theresa Arusha mpaka leo bado kinatumika.Hii kwaya ya St Theresa iliupiga tena wimbo wa kila mtu atauchukua mzigo wake mwenyewe kwasababu walikuwa na kinanda kinachofanana na kinanda cha kwaya ya Uinjilisti.

Masahihisho mengine wimbo wa kila mtu atauchukua mzigo wake mwenyewe ulitungwa na marehemu Mchg Silas Msangi na ulifundishwa na Mwalimu Msuya.Mpaka sasa kwaya ya Uinjilisti inafundishwa na Mwalimu Mjema aliyempokea Mwalimu Msuya kijiti tangu miaka ya 80s.Kuna nyimbo kadhaa za kwaya ya Uinjilisti ambazo zimeingizwa katika katibu cha Mwimbieni Bwana 1. Siku zote kanisa uanzia nyumbani utunzi wa Mwalimu Mjema 2 Nitume mimi Bwana utunzi wa marehemu Mchungaji Silas Msangi.

Jina la kinanda nimeshindwa kulipata leo kwasababu kinanda kipo store ambayo ina makorokoro mengi lakini nimepewa ahadi ya kupewa jina la kinanda siku watakayokuwa na nafasi kwasababu pia mtunza vyombo hayuko kwa sasa.


Ngongo,

Sasa nina uhakika kuwa ilikuwa KWAYA KUU. Walikuwa na wimbo wao mmoja hadi leo naukumbuka maneno kadhaa ingawa nilisikia mara moja tu. "Njooni tumwimbie bwana......" ambao waliimba kwenye nyimbo zao za miaka ya 80 mwishoni. Huyu Mpiga gitaa atakuwa ni huyo Sheggy kijana mmoja anayejipenda sana na kweli alikuwa akipiga solo vizuri sana. Pia Mpiga BASS nilikuwa nimemsahau, ndiyo alikuwa mpiga Bass wa kwanza ambaye nilimuona akipiga Bass kama Professional wote duniani, yaani anapiga kwa kutumia vidole vitatu vya katikati vikiwa vyote vimeelekewa chini. Nilisimama na kuwa namshangaa upigaje wake huo wa ajabu huko Tengeru kwenye mashindao.

Mwaka huo Kwaya Kuu hawakushiriki mashindano, nafikiri ili kuwaachia kwaya nyingine wawakilishe Kanisa. Mwalimu wa hii Kwaya ndiyo alikuwa huyo jamaa mwenye Madevu. Tulikuwa na uhusiano mzuri sana na Kwaya Kuu na hasa ukichukulia kwa miaka nikiwa hapo, Mwenyekiti wa UKWATA Mkoa wa Arusha walikuwa vijana wa TCA. Pia hii ilifanya hata Chuo pia kikawa karibu sana na Askofu Alpha Mohamed na gari lake la Alpha Romeo 🙂

Basi ntamuagiza Mdogo wangu akija hapo Arusha mjini, anitafutie hiyo kaseti ya hii Kwaya Kuu.

Siku hizi wamebaki Wakata viuno na Ndombolo zao majukwaani. Anyway, wakati ukuta, ukipigana nao..... Itafika muda watu watawakumbuka hata Wapiga ndombolo Makanisani na kuwasifu na kusema, hawa wa siku hizi (mwaka sijui 2050) ndiyo wabovu sana heri yao........

Nakusubiri kwenye kesi ya Kinanda na habari zaidi.

Naburudika sasa tayari: Kwaya kuu Arusha - YouTube
 
Last edited by a moderator:
Hivi ule wimbo wa upendo...uliimbwa na kwaya gani? Nijaponena kwa lugha.......za wanadamu na malaika....
Kama sinao upendooo..mimi si kitu kabisa.
 
Nikiwa mjini Morogoro au Dodoma, ni wapi naweza kupata CD/DVD ya kwaya ya Vijana Arusha yenye wimbo wa 'Kila mtu atauchukua mzigo wake'?.
 
Hiyo ni kwaya Kuu mjini kati KKKT

Hivi ule wimbo wa upendo...uliimbwa na kwaya gani? Nijaponena kwa lugha.......za wanadamu na malaika....
Kama sinao upendooo..mimi si kitu kabisa.
 
Hivi ule wimbo wa upendo...uliimbwa na kwaya gani? Nijaponena kwa lugha.......za wanadamu na malaika....
Kama sinao upendooo..mimi si kitu kabisa.

mkuu umenikumbusha mbali sana,hizi albamu sijui kama zinapatikana madukani.
 
Mungu alinena nae Musa hicho kiatu kivue kivue
Kuiba waume wa wenzio nakuambia hicho kiatu kivuee
 
Mkuu Ngongo,

Zile nyimbo za Kwaya Kuu nimekuja kuzipata. Zipo Album nyingi sana kuna mtu kaziweka kwenye Program ya SPOTIFY.

Album ambayo nilikuwa nauliza inaitwa (Uzuri wa Mbinguni) Tutaimba Milele ambapo kuwa wimbo huo wa Tutaimba milele na ule wa NJOONI TUMWIMBIE BWANA. Huu wa Njooni tumwimbie Bwana, solo la Sheggy kwa kweli unalizikia lilivyotulia. Jamaa alikuwa kweli ana kipaji si mchezo.

Hiyo Program una-Download na ku install kwenye computer au Android kama sikosei na baadaye kwenye search unaandika album au wimbo unaoutaka. Ukiandika kwaya kuu, utaona album zao nyingi sana kuna mtu kazitupia. Ila tu huwezi kuzi-download zaidi ya kusikiliza.
Pia kama ukilipia, basi unaweza kutengeneza NEW PLAYLIST na ukatengeneza list yako mwenyewe. Juu kulia kwenye list, unaswitch kwenye AVAILABLE OFFLINE. Program itazivuta hizo nyimbo na utaweza kuzisikiliza hata bila ya Internet kuunga. Ila bado huwezi kuzi-download. Hii program kuna nyimbo nyingi sana za kila aina.

Asante tena kwa nondo kuhusu hii kwaya. Ubarikiwe.

Mkuu Sikonge

Ilikuwepo tena kwaya nyingine kali hapo mjini kati ikijulikana zaidi kama Kwaya Kuu hii nayo ilikuwa ikikimbizana sana na kwaya Uijilisti ni kwaya kongwe haswa ilianzishwa miaka ya 70s nayo ilikuwa ikirekodi nyimbo zake nchini Kenya Mzee Moi pia alikuwa akiwaalika sana hasa kipindi cha siku yake ya kuzaliwa na sikuuu nyingine za kiserekali.Mpiga solo wa Kwaya Kuu alikuwa jamaa mmoja akiitwa Sheggy yeye alikuwa akipiga copy za muziki wa majuu hotel 77 baada Kanda Bongo Man alipokuja Tanzania alimzimikia sana akamchukua katika maonyesho yake mbali mbali nchini na nje ya nchi sijui siku hizi yuko wapi jamaa alikuwa balaa katika mpini wa solo magita yote alikuwa akiyamudu sana labda ulikuwa unamzunguzia huyu alikuwa akjipenda sana.Kuna Mwingine jina limenitoka yeye alikuwa akipiga bass gita kabla ajajiunga na kwaya kuu alikuwa akipiga Maquiz enzi za Babu Seya akitamba sana hapa nchi.Nimejaribu kukupa kahistoria kafupi ili ujue hizi kwaya zilikuwa juu kiasi gani

Natanguliza shukrani.
 
Last edited by a moderator:
alafu kumbe zile nyimbo za injiri za kipindi kile zilikua zinatamba katika eneo husika mfano hizo za arusha mnazoongelea mimi wa mza sizijui najua barabara ya 13, mapigano, muungano, kagunga ya sauri. sengerema, sati ya jangwani, makongoro
 
Hizi ndizo nyimbo/muziki bora wa Injili nilipata kusikiliza
************************************
1. Katika Viumbe Vyote
2. Mmoja wa Wanasheria
3. Mtu Ajaribiwapo
4. Mtu Mkubwa Mmoja
5. Neno Alikuwa kwa Mungu
6. Nyumba Juu ya Mwamba
7. Samsoni Mnadhiri
8. Twasoma Mwezi wa Sita
9. Ufunuo wake Yohana
10. Wakati ule wa Nuhu
************************************

ASANTE SAALNA MKUU!

Nakumbuka mwanzoni mwa miaka ya 90s Baba yangu alikuwa mchuuzi wa redio akizitoa singida kuzipeleka burundi.

Testing ya redio hizo aliifanyia kijijini ketu Kigoma(V) (Kamara-Mkunkuba) akipendelea kuweka nyimbo za KWAYA hiyo.
Hadi vijiji & Vitongoji vya jirani vilikusanyikia nyumbani had usiku wa manane .

Ilikuwa ikifana sana. Na namshukuru Mungu jamaa hao wamepewa Uraia kwa mara ya kwanza (juzjuz tu).
 
Hizi ndizo nyimbo/muziki bora wa Injili nilipata kusikiliza
************************************
1. Katika Viumbe Vyote
2. Mmoja wa Wanasheria
3. Mtu Ajaribiwapo
4. Mtu Mkubwa Mmoja
5. Neno Alikuwa kwa Mungu
6. Nyumba Juu ya Mwamba
7. Samsoni Mnadhiri
8. Twasoma Mwezi wa Sita
9. Ufunuo wake Yohana
10. Wakati ule wa Nuhu
************************************

Ni kweli hiyo kwaya ilikuwa inaimba kwa maana ya kumtangaza Mungu awe nuru kwa Ulimwengu.Hivi hiyo kwa ilipotelea wapi?au sifa zilizidi maana Lusifa hajafa
 
Hivi ule wimbo wa upendo...uliimbwa na kwaya gani? Nijaponena kwa lugha.......za wanadamu na malaika....
Kama sinao upendooo..mimi si kitu kabisa.

Hao ni KKT Mabibo,hivi waliishia wapi au sifa zilizidi maana Lusifa bado hajafa
 
Kuna ule wimbo walikuwa wanaimba ''Mungu katuumba kwa mfano wake katutofausisha na vingine,katutofausisha na wanyamaa wasio na akili.................
Huu wimbo title yake ni ipi?

Katika viumbe vyote
 
sasa hivi wamebakia wakina Rose Muhando na mauno yao, hivi umeona video ya Rose ya wololo? huyu dada ananichefua hadi basi, sijui mshauri wake ni nani huyu mwanamke, na sijui halipiti kwenye mitandao likasoma maoni ya watu akajirekebisha? achukue mfano wa Bahati, Christina shusho etc, hizo nyimbo nilizisikia nikiwa mdogo but mpaka leo nikizisikia nasuuzika roho sana sana, hazichuji kabisaa.

Mwenzio anaangalia soko la vijana ambao ndiyo wanaompatia umaarufu.
 
Back
Top Bottom