Kwanini Zitto nisikuite msaliti?

Kwanini Zitto nisikuite msaliti?

Wewe narudia huu si muda wa siasa za chuki,fitina una miezi 4 mbele unakalia chuki unategemea nini? weka mazuri ya chamalako watu waone wapime na si kumzungu mzia mtu kilasiku hum



Baada ya watanzania kuwasikiliza ccm siasa za ugaidi,udini,ukabila na kupandikiza mamluki,sasa hivi hawako tayari kurudi nyuma chadema,Cuf,NLD na Nccr ndio habari ya mjini
 
Sasa umesha sema unatarajia yaani wewe pekeyako, sasa hakuna shida endelea kutarajia hivyohivyo


Ni weke sawa,
Kwa kuwa chadema amekiita chama cha wachagga na kuna ubaguzi,natarajia hata Msando atamfukuza Act kwani nae ni Mchagga,
Natarajia,hatawahusisha wachagga na shemeji zao maana anahofu na madaraka,

Natarajia hataungana na UKAWA kwa kuwa wote wanaudini na maadui wake wamo ndani ya Umoja wa Ukawa
Shemeji za wachagga kama,Wasukuma,wahaya,wakurya,wamasai,wagogo,wahehe,wapare,wanyaturu,wanyiramba,waruguru wapogoro nao hatawahitaji ndani ya Act maana ni shemeji za wachagga au yeye anaugomvi na Mbowe, Dr.Slaa na Mzee Mtei tu?
 
Wana JF,
ninaomba japo kwa kifupi sana tulijadili hili la zzk na act yake,mtu huyu ametokea cdm ambako ameondolewa baada ya kubainika kuunda mtandao ambao ulikuwa na lengo la kufanya mapinduzi ndani ya chama alichokuwa,akisaidiwa na kina kitila mkumbo na samson mwigamba,na bila ya shaka na wengineo wengi kulingana na filamu ilivyoanzia kwa kina mwampamba ,shonza,na wengi wengineo.

sasa basi,kwanza alikanusha kwa nguvu zote,lakini kwa wale tunaomjua tulielewa kilicho ndani yake na hasa baada ya tuhuma zile kuwekwa mtandaoni ikiwemo humu JF.siku si nyingi akatangaza kujiuzuru ubunge baada ya kukosa sifa hizo kulingana na hukumu ya mahakama iliyomvua haki hiyo.kwa kuwa iliridhia maamuzi ya cdm.

lakini hii haikuwa bahati mbaya bali ulikuwa ni mpango mahsusi wa kukamilisha usaliti wake baada ya team A ya kitila na mwigamba kukamilisha uporaji wa madaraka ndani ya ACT-tanzania ya Kadau limbu na kumtupa nje ya chama kwa msaada wa nguvu ambayo hadi sasa haieleweki ni nani yuko nyuma ya mpango huo,maana bwana limbu amemlalamikia had msajili wa vyama kwa kumtendea ndivyo sivyo.

-zitto amegeuka na kauli ya kusema alikimbia cdm wakati si kweli bali alifukuzwa.

meengi yamekwishaandikwa humu kumhusu zitto,na hata saed kubenea tayari amejikuta matatani kisa kuanika ukweli kuhusu zitto na tayari ameanza kuandamwa na serikali kisa zitto.

-leo zzk amegeuka mtetezi wa wangwe wakati alishiriki vikao vyote vilivyochukua maamuzi juu ya wangwe ndani ya cdm wakati huo

wakati watanzania na wapenda mageuzi nchini tunafurahia kitendo cha vyama vya upinzani nchini kuunda ukawa kwa nia ya kuunganisha nguvu na kuikomboa nchi kwenye utawala wa kifisadi,yeye zzk anakuja na mpango mahsusi wa kuimegua ukawa.

wakati watanzania tukiwa tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu,na wakati tume ya uchaguzi ikiwa inasua sua na BVR,hatumsikii zzk na ACT akitoa tamko lolote kuhusu hilo kwenye mikutano yake zaidi ya kuishambulia ukawa na kumkaribisha Lowasa kwenye ACT.

wakati zitto huyu akiwa chadema mbona hakuwa anaweka nguvu nyingi kama sasa? na hata wakati fulani aliacha mikutano ya cdm na kwenda musoma kukisaliti chama kwa mkono.na hata alipobanwa hakuweza kutoa maelezo ya ni kwa nini,

zitto huyu huyu amekula fedha za NSSF zaidi ya milioni mia sita na zaidi,kwa kushirikiana na ramadhan dau kupitia kampuni yake ya leka dutigite lakini hakuwahi kuyakubali hayo hadharani na wala hataki yaongelewe.zzk pia alipewa fedha takriban milioni 33,kutoka kwa Rugemalira wa V.I.P engineering,lakini ya kwake yalinyamaziwa.na hata baada ya baadhi ya watuhumiwa wa escrow kumtaja yeye pia lakini mpaka sasa hajatamka lolote zaidi ya kukaa kimya.

sasa kwa kutumia umaskini na njaa za baadhi ya kundi la watanzania wenye tamaa na wasioweza kuzizuia tamaa zao,na kwa kuwa anapewa sapoti kwa nguvu iliyojificha.anakuja na mpango wake huu wa kununua watu sambamba na mtindo anaoutumia lowasa na kundi lake,na hata baada ya mawasiliano ya kati yake na mwigulu kunaswa kwa njia ya e-mail,na kwa kuwa anajuwa ni ukweli na yameanikwa mbona hayakanushi ili tumuelewe alipo.

hitimisho langu kwa sasa nawaomba wale wote mliopangwa kama team ya mtandaoni na huyo zzk -------- mumrudie mungu na maombi yenu yanaweza kusikilizwa nae akawapa njia mbadala ya kujipatia kipato kingine tofauti na hii ya kupewa ujira kwa kuutumikia usaliti,maana utakiandama hata kizazi chenu kijacho


-
 
acheni kuweweseka mlisema hana madhara na oondoke tu chama kitakuwa bora mara dufu
 
Zito amekitenda vibaya sana CDM sababu ya tamaa yake ya fedha na huko aendako tabia hii hawezi kamwe kuiacha na lazima awatumikie waliomtuma na kumpa fedha hivyo ni mtu wa kuogopwa sana sana!
 
Devide and rule kwa mtu mliyemfukuza wenyewe? Huku kama sio kuweweseka ni nini?

Unasema ACT ni mtoto wa CCM, mbona husemi kama na CHADEMA ni chama cha Wachaga amboa ndo nyie akina MISS CHAGA?

Wewe au chakisa nikikuta mnaitetea chadema siwezi kushangaa kwan ni haki yenu.... nastaajabu ninapowakuta akina karubandika wanatoa povu kupigania maslahi yenu.
kama ni only chaganism,ilikuwaje -------- zitto akakulia hapo chadema? acha kuweweseka na kwa kuwa wewe ni mke...reketwa wa zzk endelea kumsapoti kiongozi mkuu.shame on you:lol::lol:
 
Sijawahi kuona mtu anaongea pumba kama wewe sijawahi.

Sijawahi kuona watu wanapata taabu hawalali wanatafuta umbea juu ya maisha ya mtu ambayo hayakuhusu hata kidogo sijawahii..

Sijawahi kuona mtu aliyetoka chama kimoja kwenda kingine akaendelea kusakamwa kama zzk bila sababu za msingi kwani hamuathiri mtu na itikadi zake na hawalazishi kumfuata kwa itikadi.

Hata kama zitto ni msaliti kwa chadema haiwahusu wala kuwaathiri kwani hayupo chadema sasa.

Kila siku zitto zitto zitto hamna cha kufanya wangapi wametoka vyama vyao na kujiunga na vyama vingine hawajadiliwi ...

Stop non sense bwana Amekuathirije yeye kuwa msaliti na je anahusikaje na maisha yako baada ya kusaliti chadema

acha kuongea ki hongwa hongwa we mke...reketwa wa zitto usijifanye kwamba sisi tunaomsema humu tunamfuata bali tunamchukia yeye na wewe na nyinyi wasaliti wachumia njaa mliodhani kila ukishafika ka chuo ni lazima cdm iwape nafasi za kutunisha matumbo badala ya kupanua akili kupigania nchi yenu mnatpanua midomo kuwatetea mafisadi,shame on all of you:lol:
 
Teh bavicha bwana mnachekesha sana'. Mnajitekenya kisha mnacheka wenyewe.
Vp ulitaka kwanza akalime kama mwaka mmoja hv kabla hajaenda act?

hapana,tulitaka amuombe hela Lowasa ili amuandalie chama cha kukimbilia akienguliwa ndani ya ccm:biggrin1:
 
Mda mwingine ni bora kua na adui kuliko rafiki adui. Bora kura yangu ni wape CCM ijulikane moja kwamba tupo chini ya mafisadi kuliko ukawa iliyo changanyika na akina Zitto au Hamad Rashidi.. Huku ni kuwatukana watanzania yaan watu mlio waaminisha kwamba ni wasaliti leo tuungane nao!!! No way! Ukawa msije mkaingia mkekenge kuwakaribisha hao vibaraka wa CCM wanao vaa ngozi ya upinzani
 
Commonmwananchi, wewe ni zaidi Ya geneous..... Congrts ndugu. Ni watanzania wachache sana wenye upeo na uwezo wa kuchanganua mambo kama wewe
 
Mkuu Bramo kiongozi mkuu wa mapinduzi ya Iran ni abuse language ?.Nimempachika cheo hicho kwasababu nchi ya Iran Rais yupo lakini mwenye madaraka ya mwisho ni Kiongozi mkuu.Zitto ni kiongozi mkuu wa ACT mwenyekiti yupo lakini hana madaraka makubwa kama Zitto ambae ndiye kila kitu ACT Mwenyekiti ni boya tu hana lolote kazi yake kubwa ni kumsikiliza kiongozi mkuu anataka nini.

Sheria mpya ya JF ambayo haijandikwa mahali popote Ayatollaah ni abuse language.

Mkuu hapo juu kwenye RED dash dash utakuwa ulitumia abusefully Language, usirudie tena.

cc mwekundu
 
Last edited by a moderator:
Nakupa hongera kijana kwa kazi nzuri ya kujipambanua rangi yako na wa Tanzania kukufahamu ya kuwa ww ni mbwa mwitu uliuekuwa umejivisha ngozi ya kondoo na kumbe ni chui tena hatari kwa maisha yetu hakika haitaji uwe mpaka na master's kuelewa lakn kumbuka heri mwisho wa jambo kuliko mwanzo wake"hakuna mtu awaye yeyote ambae alikuwa modal Wang kama zzt bt kwa hizi comedians zmenifanya nfke kwenye mkutano wako na kuthibitisha kwa macho yang kama ndo ww ama hakika historia itakukumbusha. bt wa Tanzania tunataka mabadiiko sio ngojera na unafiki kama naoshuhudia kwa Sana.
 
Wanajukwaa mimi namchukulia Kiongozi Mkuu(ingawa anaonaa soo kujiita Kiongozi Mkuu) wa ACT Wazalendo kuwa ni mtu makini kuanzia juu mpaka chini,yaani kuanzia unywele mpaka unyayo. Naomba kuweka kumbukumbu ya kauli alizowahi kunukuliwa ili kuonyosha umakini wake
  1. Nitakuwa wa Mwisho kuondoka Chadema VS Tulianzisha ACT Wazalendo kutokana na kubinywa kwa demokrasia kwenye chama.
  2. Sitagombea tena ubunge, nitagombea uraisi 2015 VS Sitagombea tena uongozi,ninataka kufundisha
  3. Sitagombea tena uongozi,ninataka kufundisha VS Sitagombea tena Kigoma Kaskazini,nitagombea Kigoma Mjini
  4. UKAWA wachumia tumbo VS Tupo tayari kuungana na UKAWA
  5. Sitagombea uongozi ACT,waliotegemea wameumbuka VS Kiongozi Mkuu wa ACT
  6. Ni kweli CHADEMA ni wadini na wabaguzi VS Kilimanjaro na Arusha zina maendeleo sana lakini hazipo juu katika kuchangia pato la Taifa
Aidha katika suala la uwiano kati ya mchango kwenye pato la Taifa na Maendeleo ya Mkoa husika, Kiongozi Mkuu ameonyesha umakini mkubwa sana. Msome Mwana Duru Nguruvi3 uone jinsi gani Supreme Zitto K alivyo makini zaidi

DAHANA POTOFU INAYOENEZWA NA ACT

NI KUHUSU MGAWANYO WA RASILIMALI NA MAENDELEO

MBEGU INAYOPANDWA NA ACT NI CHAFU NA HATARISHI


Sehemu ya I

Ilipojadiliwa kama Rwanda na Burundi zijiunge EAC, iliundwa tume kukusanya maoni.

Mjadala huo uliingia bungeni . Zitto alinukuliwa akisema Tanzania haipaswi kuhofua kujiunga EAC kwasababu tofauti za kiuchumi hazipo EAC tu, zipo nchini.

Akasema mbona Tanzania ni nchi moja lakini kuna tofauti ya maendeleo kati ya Kigoma na Kilimanjaro!

Zitto na ACT wamenukuliwa akiongelea mgawanyo wa rasilimali, kwamba mikoa inayochangia zaidi pato ipo nyuma kimaendeleo.

Ametolea mfano wa Arusha na Kilimanjaro ikiwa na mchango michache , kimaendeleo ikiwa mbele

Kauli ya supreme leader haina ukweli kuhusu maendeleo bali kutafuta siasa rahisi na umaarufu butu

Supreme ameficha ukweli akijua, kutumbukiza mbegu ya ukabila na ukanda, itasaidia ima kumnyanyua kisiasa, au chama chake .
Ni mbegu ile aliyoikataa alikotoka japo alikuwa ni sehemu ya uongozi

Kauli imelenga kuwagawa wananchi kwa hoja dhaifu bila ukweli ina matatizo si kwa taifa tu bali kwa ACT ya ‘kizalendo ‘inayogawa wazalendo kwa misingi ya kikandaKauli hiyo imekuja kwa shinikizo la kisiasa linaloikabili ACT.

Matarajio ya haraka yanonekana kuwa na ugumu , kila mbinu safi na chafu zitatumika. Wazungu wanasema ‘shoot any moving object''

Tuangalie dhana ya kwanini kuna tofauti za maendeleo kutoka sehemu moja hadi nyingine

Inatosha kusema tatizo la uwiano wa maendeleo si la Tanzania tu. Nchi zilizoendelea zina matatizo hayo kutokana na sababu tofauti

MAENDELEO

Ni hatua ya mabadiliko chanya kwa mtu, watu, jamii na taifa na ni zao la jitihada .
Maendeleo yana vichocheo vingi, vikiwemo elimu, mwamko, mazingira, maeneo na rasilimali kwa uchache wa kutaja

Katika nchi yetu, maendeleo yanaelezwa kwa vigezo kama Historia, jamii, na jiografia.

Hivyo kuangalia maendeleo bila kuangalia chanzo na vichocheo ni kupotosha umma.

Haiwezekani kuongelea Tanzania bila kuzungumzia ukoloni na athari zake, elimu, mwamko wa jamii, matumizi ya rasilimali na eneo husika kwa kuitazama jiografia ya nchi yetu.

Kauli za rahisi za eneo fulani ni tofauti na jingine bila kufafanua, ni za kichochezi, kufilisika kisiasa na dalili mbaya kwa jamii yetu.

Inaendelea…


OMBI: Mods Mnisamehe kama kauzi kangu katawaudhi
 
Back
Top Bottom