Wanajukwaa mimi namchukulia Kiongozi Mkuu(ingawa anaonaa soo kujiita Kiongozi Mkuu) wa ACT Wazalendo kuwa ni mtu makini kuanzia juu mpaka chini,yaani kuanzia unywele mpaka unyayo. Naomba kuweka kumbukumbu ya kauli alizowahi kunukuliwa ili kuonyosha umakini wake
Aidha katika suala la uwiano kati ya mchango kwenye pato la Taifa na Maendeleo ya Mkoa husika, Kiongozi Mkuu ameonyesha umakini mkubwa sana. Msome Mwana Duru Nguruvi3 uone jinsi gani Supreme Zitto K alivyo makini zaidi
- 1. Nitakuwa wa Mwisho kuondoka Chadema VS Tulianzisha ACT Wazalendo kutokana na kubinywa kwa demokrasia kwenye chama.
2. Sitagombea tena ubunge, nitagombea uraisi 2015 VS Sitagombea tena uongozi,ninataka kufundisha 3. Sitagombea tena uongozi,ninataka kufundisha VS Sitagombea tena Kigoma Kaskazini,nitagombea Kigoma Mjini 4. UKAWA wachumia tumbo VS Tupo tayari kuungana na UKAWA 5. Sitagombea uongozi ACT,waliotegemea wameumbuka VS Kiongozi Mkuu wa ACT 6. Ni kweli CHADEMA ni wadini na wabaguzi VS Kilimanjaro na Arusha zina maendeleo sana lakini hazipo juu katika kuchangia pato la Taifa
DAHANA POTOFU INAYOENEZWA NA ACT
NI KUHUSU MGAWANYO WA RASILIMALI NA MAENDELEO
MBEGU INAYOPANDWA NA ACT NI CHAFU NA HATARISHI
Sehemu ya I
Ilipojadiliwa kama Rwanda na Burundi zijiunge EAC, iliundwa tume kukusanya maoni.
Mjadala huo uliingia bungeni . Zitto alinukuliwa akisema Tanzania haipaswi kuhofua kujiunga EAC kwasababu tofauti za kiuchumi hazipo EAC tu, zipo nchini.
Akasema mbona Tanzania ni nchi moja lakini kuna tofauti ya maendeleo kati ya Kigoma na Kilimanjaro!
Zitto na ACT wamenukuliwa akiongelea mgawanyo wa rasilimali, kwamba mikoa inayochangia zaidi pato ipo nyuma kimaendeleo.
Ametolea mfano wa Arusha na Kilimanjaro ikiwa na mchango michache , kimaendeleo ikiwa mbele
Kauli ya supreme leader haina ukweli kuhusu maendeleo bali kutafuta siasa rahisi na umaarufu butu
Supreme ameficha ukweli akijua, kutumbukiza mbegu ya ukabila na ukanda, itasaidia ima kumnyanyua kisiasa, au chama chake .
Ni mbegu ile aliyoikataa alikotoka japo alikuwa ni sehemu ya uongozi
Kauli imelenga kuwagawa wananchi kwa hoja dhaifu bila ukweli ina matatizo si kwa taifa tu bali kwa ACT ya kizalendo inayogawa wazalendo kwa misingi ya kikandaKauli hiyo imekuja kwa shinikizo la kisiasa linaloikabili ACT.
Matarajio ya haraka yanonekana kuwa na ugumu , kila mbinu safi na chafu zitatumika. Wazungu wanasema shoot any moving object
Tuangalie dhana ya kwanini kuna tofauti za maendeleo kutoka sehemu moja hadi nyingine
Inatosha kusema tatizo la uwiano wa maendeleo si la Tanzania tu. Nchi zilizoendelea zina matatizo hayo kutokana na sababu tofauti
MAENDELEO
Ni hatua ya mabadiliko chanya kwa mtu, watu, jamii na taifa na ni zao la jitihada .
Maendeleo yana vichocheo vingi, vikiwemo elimu, mwamko, mazingira, maeneo na rasilimali kwa uchache wa kutaja
Katika nchi yetu, maendeleo yanaelezwa kwa vigezo kama Historia, jamii, na jiografia.
Hivyo kuangalia maendeleo bila kuangalia chanzo na vichocheo ni kupotosha umma.
Haiwezekani kuongelea Tanzania bila kuzungumzia ukoloni na athari zake, elimu, mwamko wa jamii, matumizi ya rasilimali na eneo husika kwa kuitazama jiografia ya nchi yetu.
Kauli za rahisi za eneo fulani ni tofauti na jingine bila kufafanua, ni za kichochezi, kufilisika kisiasa na dalili mbaya kwa jamii yetu.
Inaendelea
For wise people, his or her focus is to see how the man is able to express the matter but not how the man is looks like. Be a wise man. ACT is the pathway to revolution.- Sijawahi ona kokote siasa inakofanywa mwanachama wa chama kimoja kwa wakati huohuo ni mwanzilishi wa chama kingine cha siasa, sijawahi.
- Sijawahi kuona mtu anajiunga na chama fulani baada ya siku tano anapewa uongozi mkuu wa chama hicho, sijawahi
- Sijawahi kuona popote siasa inapofanywa, mwenyekiti wa chama yupo chini ya mtu fulani. Yahani kikatiba kabisa kuna mtu yupo juu ya mwenyekiti, hii pia sijawahi kuona.
- Sijawahi kuona popote pale chama cha upinzani kukipinga chama cha upinzani na si chama tawala. AGAINST CHADEMA TANZANIA(ACT). Kwa maneno au hata vitendo. Chama kinafanya sherehe kikipata wafuasi wa upinzani kuliko wa chama tawala.
- Sijawahi kuona chama cha upinzani kinafadhiliwa na chama tawala kiuchumi na kimikakati. Tumefanya uzinduzi wa chama chako Zuberi kwa gharama kubwa sana, air time ITV, chakula, ukumbi expensive, na mbwembwe nyingi. Lakini mbona hujawahi kuchangisha pesa toka kwa wanachama wako? Kama kuna mtu anachangia ni nani huyo? Mtamlipaje baadae?
- Sijawahi ona chama cha upinzani popote pale siasa inapofanywa, wafuasi wake ni wale wanachama na wafuasi wa chama tawala. Le mutuz, laki si pesa, musa alani n.k, hii nayo sijawahi ona.
Kwa yote hayo juu Zuberi kwa nini nisikuite kwamba wewe ni msaliti halisi wa demokrasia hapa nchini. Kama kweli wewe siyo msaliti mbona hujawahi kujitokeza na kukataa zile namba za simu walizozitoa chama chako cha zamani kuwa zilitumika katika ufisadi? Mbona sijasikia kuikana ile akaunti ya benki wa yule dada kule ujerumani?
UKINIJIBU HAYO KWA UFASHA WEWE KWELI SI MSALITI.
Aisee jamani tumeshachoka sasa, zito mmefukuza kaondoka bado maneno hayaishi?
Hivi mfano umempa talaka mke wako alafu akaondoka ww uliyetoa talaka unalalamika tuu, mara oohh ulikuwa unanisaliti, maara oohh mwananmke gani wewe? sasa talaka umeshatoa na mtalaka kaondoka wewe bado unalalamika nini?
Nyie Chadema acheni upuuzi tumeshawachoka na kulialia kwenu haaa
Mkuu mansakankanmusa, moja ya misimamo yangu humu jf, ni kuheshimu mawazo ya kila mtu hata ziwe pumba kiasi gani!, hivyo naheshimu mawazo yako japo una matatizo katika kujenga hoja maridhawa!.Habari yako msomaji,
Napenda nifungue hoja hii Kwa kuelezea kidoogo kuhusu ufahamu wa demokrasia na mageuzi duniani.
Zitto kama msomi kijana katika karne hii hakupaswa kutenda kosa hili la kiufahamu katika siasa. Tena katika muongo Huu tunaotaka kufanya mageuzi Kwa maslahi ya mamilioni ya Watanzania. Huu ni utovu wa nidhamu kisiasa na ataadhibiwa na siasa yenyewe.
Katika sehemu ya PILI ya hoja hii ni uwazi au usiri wa matakwa ya mabepari. Nikizungumzia mabepari kwa wataalamu wa siasa za kimataifa watakubaliana nami kwamba hii inayoitwa anakiki lazima uishi Kwa kusurrender baadhi ya mambo yako Kwa Mataifa makubwa. Zitto kuunda upinzan ndani ya upinzani anachimba shimo ambamo hawezi kuchomoka.
Wamagharibi hawana Shida ya nani awe Rais lakini rais dhaifu atajuta. Udhaifu wa ZZK unaonekana pale anaposhindwa kusoma alama kwamba UPINZANI ndani ya UPINZANI kosa na disunity ambayo wamagharibi hata akiwa Rais 2030 watatumia udhaifu. Na ZZK atapigwa na watanzania kwa kosa hata dogo tu kwa kuwa ashasaliti CHADEMA. Kuondoka CHADEMA hakumaanishi CHADEMA ni chama bora au laa. Kikubwa ni Tabia yako ikoje.
Kikubwa katika hili ni kwamba ZZK hawezi kuunda chama kitakacholeta upinzani wa kweli kutokana na kosa la kiufahamu. Ondoka CHADEMA sawa lakini uwe na nidhamu katika siasa.
Act hamna kamanda
Kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa siasa za Tanzania, utakubaliana na mimi CHADEMA imepitia misukosuko mingi mpaka kuwa chama chenye nguvu na ambacho sasa kiko tayari kuchukuwa nchi.
Katika kipindi chote hicho cha kukua kwa CHADEMA lengo kubwa lilikuwa ni kumkombowa mtanzania dhidi ya ufisadi, dhuluma pamoja na aina zote za kumnyima haki mwananchi, mambo ambayo CCM wameyashindwa. MALENGO hayo makuu ndiyo yaliyoijenga CDM.
BAADA YA KUONEKANA KUWA CHADEMA INAIMALIKA, Hapo ndipo kidudu mtu kikaanza harakati zake za usaliti kwa kutufitinisha wanachadema na wapenda mabadiriko wote. Kwanini naita fitina ? ni kwasababu walitumia waraka wa siri, ambao waandishi wake walitumia majina bandia mf M1, MM nk kitu ambacho kinadhihirisha wazi kuwa hawakuwa na nia nzuri na mshikamano wetu.
Nasema hawakuwa na nia nzuri kwa sababu kwanza mmoja wao alikuwa ni kiongozi wa juu na kwa nafasi yake angeweza kujenga hoja kwa uwazi ili kutushawishi, pili hawakuwa na nia nzuri kwa vile walifahamu wazi kwamba kwa wakati tulionao ni rahisi kutugawa kwa kuleta hoja ndogo ndogo tena kwa njia ya panya na yakichonganishi hivyo kututoa katika lengo kuu la kupambana na mafisadi na ufisadi.
JE HUYU SIO WASALITI? Kiongozi bora na mwenye nia nzuri hujenga hoja na kuwashawishi wanachama/wananchi kwa uwazi ili kuimalisha umoja wetu. Kwa kujilidhisha usome waraka wao wa siri.
NAPENDA KUTOWA PONGEZA kwa wote waliowezesha kupatikana kwa waraka ule wa siri, halafu kuyabaini majina ya wahusika, na licha ya awali kukanusha hatimaye walikiri kuhusika na kujitetea kwa hoja dhaifu.
SABABU KUBWA YA KUANDIKA HAYA LEO
Ni kuwataadhalisha viongozi wetu wa UKAWA kuwa lengo letu kuu kwa sasa ni kumpigania mwananchi apate haki zake dhidi ya ufisadi na aina zote za rushwa. kama vyama kuna mambo tunatofautiana, hivyo vitofauti ndivyo vitatumika na mafisadi kutugawa. HIVYO BUSARA INAHITAJIKA.
Kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa siasa za Tanzania, utakubaliana na mimi CHADEMA imepitia misukosuko mingi mpaka kuwa chama chenye nguvu na ambacho sasa kiko tayari kuchukuwa nchi.
Katika kipindi chote hicho cha kukua kwa CHADEMA lengo kubwa lilikuwa ni kumkombowa mtanzania dhidi ya ufisadi, dhuluma pamoja na aina zote za kumnyima haki mwananchi, mambo ambayo CCM wameyashindwa. MALENGO hayo makuu ndiyo yaliyoijenga CDM.
BAADA YA KUONEKANA KUWA CHADEMA INAIMALIKA, Hapo ndipo kidudu mtu kikaanza harakati zake za usaliti kwa kutufitinisha wanachadema na wapenda mabadiriko wote. Kwanini naita fitina ? ni kwasababu walitumia waraka wa siri, ambao waandishi wake walitumia majina bandia mf M1, MM nk kitu ambacho kinadhihirisha wazi kuwa hawakuwa na nia nzuri na mshikamano wetu.
Nasema hawakuwa na nia nzuri kwa sababu kwanza mmoja wao alikuwa ni kiongozi wa juu na kwa nafasi yake angeweza kujenga hoja kwa uwazi ili kutushawishi, pili hawakuwa na nia nzuri kwa vile walifahamu wazi kwamba kwa wakati tulionao ni rahisi kutugawa kwa kuleta hoja ndogo ndogo tena kwa njia ya panya na yakichonganishi hivyo kututoa katika lengo kuu la kupambana na mafisadi na ufisadi.
JE HUYU SIO WASALITI? Kiongozi bora na mwenye nia nzuri hujenga hoja na kuwashawishi wanachama/wananchi kwa uwazi ili kuimalisha umoja wetu. Kwa kujilidhisha usome waraka wao wa siri.
NAPENDA KUTOWA PONGEZA kwa wote waliowezesha kupatikana kwa waraka ule wa siri, halafu kuyabaini majina ya wahusika, na licha ya awali kukanusha hatimaye walikiri kuhusika na kujitetea kwa hoja dhaifu.
SABABU KUBWA YA KUANDIKA HAYA LEO
Ni kuwataadhalisha viongozi wetu wa UKAWA kuwa lengo letu kuu kwa sasa ni kumpigania mwananchi apate haki zake dhidi ya ufisadi na aina zote za rushwa. kama vyama kuna mambo tunatofautiana, hivyo vitofauti ndivyo vitatumika na mafisadi kutugawa. HIVYO BUSARA INAHITAJIKA.