Toka nianze kujua siasa za nchi hii hakuna mwanasiasa aliyewahi kutuhumiwa akakubali kosa hata kama ni kweli...... hata serikali imekuwa ikituhumiwa mambo mengi lakini imekuwa ikikanusha na baadae imekuja kujulikana ni kweli...ninachookiona kwenye sakata la mengi kutaka kuiangusha serikali ya kikwete, mzee mengi hajakurupukaa ana timu yake ya intelijensia hadi kuja kulalamika kwenye vyombo vya habari kuna kitu amekiona na amefanya uchunguzi binafsi akagundua kuna kitu mbele ya sakata hili.......hata kina kitila na mwigamba walipoambiwa wameandaa wa waraka wa mapinduzi chadema walikataaa...ushahidi ulipotolewa kitila alikubali lakini akadai hawakumshirikisha zito kwenye sakata lile
kwenye hili sakata kuna watu wameingia choo cha kike na mwisho wao unakaribia ..hizi tuhuma zina wiki tatu kwa wanasiasa ni hatari sana kuhusishwa na kitu tena kwenye vyombo vya habari ukae kimya hadi mtuhumiwa anapolalamika ndio ukanushe hapa kuna walakini......unaweza kukanusha lakini damage yako kisiasa imeshafanyika na itakugharimu mbele ya safari tofauti na ambavyo ungekanusha siku ya kwanza.........ni sawa na mbowe alivyotuhumu tume ya uchaguzi kuwa wakimuongezea muda Jk patachimbika tuliona siku ya pili tuu mwenyekiti wa tume alijibu tuhuma zile kuwa hakuna atakayeongezewa mda hata kama moyoni unajua jibu lake ni bora ujitokeze mapema kujibu mashambulizi usisubiri damage itokee ndio utafute majibu