Kwanini Zitto nisikuite msaliti?

Kwanini Zitto nisikuite msaliti?

CCM ikimpitisha EL imejiua yenyewe, isipompitisha EL imejiua yenyewe, ACT kama mwana wa CCM akimchukua EL imejiua yenyewe, asipomchukua ili hali ndo mfadhili mkuu wa ACT imejiua yenyewe, duuuu.

Vyovyote itakavyokua CCM na ACT kufaaaa ni lazima, na kila karata wanayocheza itaishia kifo chao, yaani siku ya kufa nyani au tuseme chama, wanachama wote hukimbia kwa kutawanyika kama hakuna jiwe litabaki juu ya jiwe lingine. Dhambi ya USALITI itaitafuna CCM kwa miaka 54 imeaminiwa na kuwasaliti watz, ACT na ZZK ndo wasaliti wa wazi, lazima dhambi ya USALITI iue vyama vyenu.

Ni heri uwe UKAWA leo kwa kuchagua mwenyewe, kuliko kuingia UKAWA kesho kwa kukosa sehemu ya kufanyia siasa zako wakati CCM na ACT is no more. HILI NI WAZO KUU, heri hiyari kuliko shurti ya mazingira.

Nawasilisha
 
Wananchi hatukutaka uongeze idadi ya vyama vya upinzani, tunachotaka sisi ni UKOMBOZI jitihada zako za kugawa nguvu ya Upinzani wakati wa uchaguzi mkuu hakika ni kwamba unasaliti umma, kama CDM walishitukia mbinu zako za kihalamia ktk kusaka uongozi, je kwani baada ya kufukuzwa usijiunge na NCCR au CUF ili kuongeza nguvu ya upinzani kuliko kuigawa???

Kimsingi wewe ni msaliti wa UKOMBOZ na pengine umekuwa mzito kuelewa jamii ya watanzania wanavyokuona na kukuchukulia, utahongwa na kumwaga pesa za mafisadi lakn utu wako ulipaswa kuja kwanza, sio pesa zao mafisadi.

Ulisema kwa mdomo wako wanasiasa wasiaminiwe, watu wakabaki midomo wazi, leo wewe ni nani??? mwanasiasa ambaya hupaswi kuaminika au msaliti ambaye pia hupaswi kuaminika na chama chochote cha upinzani wa kweli?

Ungekuwa mwepesi zitto ungeelewa kuwa umeikosea jamii ya Tz tena sana, huwezi jaribu kugawa nguvu za ukombozi harafu utugawie kadi kwenye malori shame on you msaliti. Usaliti ulioufanya hao unaowapa kadi kwenye malori utawahakikishia vipi kuwa hutawasaliti??? Ulisema hujaanzisha ACT kukakiri ulianzisha, Ulisema hutaki cheo kikubwa Ukaomba uwe Supreme Leader, Chuuuuuuuuuuu, ube ni kinhu ki ishi? a walking and talking disaster by itself or what?

Hatutaki utititi wa vyama bali ukombozi, vita yako kwa umma ni dhidi ya umma mzima kutoa hao wafadhili wako na vibaraka wenzako. Kama ulitaka KUUNGANA na UKAWA ungewaita wasaka tonge? Je si ungeingia chama kimoja wapo UKAWA kuliko kuanzisha chama kipya? Usizuge raia wako macho tena jicho la saa 6 mchana

Nawasilisha
 
Watakuja mashabk wa ayatoll°ah watajibu

Acha waje vibaraka wenzake kumtetea na ID zao za juzi juzi, ukweli ni kwamba kilichoandikwa kimeandikwa UMMA haupendi na hautakaa upende usaliti, leo anampeleka kinyume na umbo lake sele, sele yule wa simba wa afrika leo ni kenge wa africa
 
Wananchi hatukutaka uongeze idadi ya vyama vya upinzani, tunachotaka sisi ni UKOMBOZI jitihada zako za kugawa nguvu ya Upinzani wakati wa uchaguzi mkuu hakika ni kwamba unasaliti umma, kama CDM walishitukia mbinu zako za kihalamia ktk kusaka uongozi, je kwani baada ya kufukuzwa usijiunge na NCCR au CUF ili kuongeza nguvu ya upinzani kuliko kuigawa???

Kimsingi wewe ni msaliti wa UKOMBOZ na pengine umekuwa mzito kuelewa jamii ya watanzania wanavyokuona na kukuchukulia, utahongwa na kumwaga pesa za mafisadi lakn utu wako ulipaswa kuja kwanza, sio pesa zao mafisadi.

Ulisema kwa mdomo wako wanasiasa wasiaminiwe, watu wakabaki midomo wazi, leo wewe ni nani??? mwanasiasa ambaya hupaswi kuaminika au msaliti ambaye pia hupaswi kuaminika na chama chochote cha upinzani wa kweli?

Ungekuwa mwepesi zitto ungeelewa kuwa umeikosea jamii ya Tz tena sana, huwezi jaribu kugawa nguvu za ukombozi harafu utugawie kadi kwenye malori shame on you msaliti. Usaliti ulioufanya hao unaowapa kadi kwenye malori utawahakikishia vipi kuwa hutawasaliti??? Ulisema hujaanzisha ACT kukakiri ulianzisha, Ulisema hutaki cheo kikubwa Ukaomba uwe Supreme Leader, Chuuuuuuuuuuu, ube ni kinhu ki ishi? a walking and talking disaster by itself or what?

Hatutaki utititi wa vyama bali ukombozi, vita yako kwa umma ni dhidi ya umma mzima kutoa hao wafadhili wako na vibaraka wenzako. Kama ulitaka KUUNGANA na UKAWA ungewaita wasaka tonge? Je si ungeingia chama kimoja wapo UKAWA kuliko kuanzisha chama kipya? Usizuge raia wako macho tena jicho la saa 6 mchana

Nawasilisha
Ndo maana unaitwa fikri kwanza,nakuomba fikri kwanza ndo ule uzi wa fikra na facts na si ngojera za toka 2013,mwacheni msaliti afanye mambo yake mbona mmemng'ang'ania sana,jamaa kawapuuza mnaongea kama hawasikii,hadi akina Mnyika nao wameingia kichwa kichwa na tukawaona uj*nga na busara yao ilipo..mwacheni ZZK bana na usaliti wake,watanzania sio wajinga km unavyodhani wewe au km anavyodhani yeye.
Chadema sasa hivi imeniskitisha sana maana maneno na kashfa walizozitoa kwa CUF wakati ule ni sawa na hizi wanazorusha kwa ACT_wazalendo,kwa nini lakini? kwa nn mkutano yenu hamuachi kumtaja ZZK.Inavyoelekea mna wivu sana naye,ni sawa na kumpa talaka mke wako lakini ukiona kaolewa kwingine unaanza kuendeleza gubu...ni upuzu huu mnaofanya watu mnaojiita Chadema,nadhani nyie ni vichaa flani mi naamini chadema makini wapo kimya wanapiga kazxi kufuata sera zao na sii kukalia upuzi huu kila siku.....huu ni uj*nga kabisa
 
Ndo maana unaitwa fikri kwanza,nakuomba fikri kwanza ndo ule uzi wa fikra na facts na si ngojera za toka 2013,mwacheni msaliti afanye mambo yake mbona mmemng'ang'ania sana,jamaa kawapuuza mnaongea kama hawasikii,hadi akina Mnyika nao wameingia kichwa kichwa na tukawaona uj*nga na busara yao ilipo..mwacheni ZZK bana na usaliti wake,watanzania sio wajinga km unavyodhani wewe au km anavyodhani yeye.
Chadema sasa hivi imeniskitisha sana maana maneno na kashfa walizozitoa kwa CUF wakati ule ni sawa na hizi wanazorusha kwa ACT_wazalendo,kwa nini lakini? kwa nn mkutano yenu hamuachi kumtaja ZZK.Inavyoelekea mna wivu sana naye,ni sawa na kumpa talaka mke wako lakini ukiona kaolewa kwingine unaanza kuendeleza gubu...ni upuzu huu mnaofanya watu mnaojiita Chadema,nadhani nyie ni vichaa flani mi naamini chadema makini wapo kimya wanapiga kazxi kufuata sera zao na sii kukalia upuzi huu kila siku.....huu ni uj*nga kabisa

Uupuuzi ni ulioandika wewe, kama ulikuwa hujui upuuzi ukoje basi soma tena ulichoaandika
 
Nawaona vibaraka tayari washaingia mkuu kumtetea msaliti Ayah tolah
 
Usaliti ni ile hali ya kwenda kinyume na makubaliano na matarajio ya wengi kwa makusudi hususani baada ya kuwa umezingatia maslahi binafsi zaidi kuliko umma. Nafikiria hii kwa leo inatosha

Msaliti huwa pia anasifa ya uongo, Msaliti agharabu ni Mwizi na mbinafisi.

Uongo: Akiulizwa mfano umeanzisha chama, Anakataa, kesho yake anakili chama ni chake; Anaulizwa kuhusu MM anakana baadaye MM1 MM2 wanamtaja na kuomba samahani, Anazunguka akijinasibu eti ndo aliiangusha serikali kwa hoja ya Escrow ile hali TUMBILI ndo alifanya kazi hiyo kubwa. Unafadhili na EL ili ACT ipae anakana baadaye anasema vyama rafiki mara yuko tayari kumpisha u ayatolaaaah iwapo EL atajiunga ACT

Mwizi: Escrow ulichukua 10m, kama kawaida anaanza kwa uongo, anakataa. Eti CCM na TISS walikupa mafedha anaamua kukaa kimya asijibu chochote, eti msomi mjanja kumbe mjingaaa, umejificha tunakuona. Kaiba chama kuwa msaada wa CCM, maana huwezi kubadili katiba ya Chama ili hali kesi iko mahakamani, hakuna chama ACT wazelendo lakni msajili wa CCM yuko kimya, LIMBU atathibitisha hilo kama bado unamashaka.

So kifupi zaidi ili uwe msaliti lazima uwe muongo na mwizi.

Je Uongo na Wizi ndo sifa ya EL, ambaye bunge na rais walijiridhisha, hivyo EL kuelekea kuwa msaliti pia na LAZIMA wasaliti wapate platform ya siasa ambayo ni ACT, marafiki wanasifa za kufanana hilo halina ubishi.

Nawasilisha
 
  • Thanks
Reactions: jme
nadhani kila chama kifanye yake halafu wananchi ndio tutaamua.
usitumie muda mwingi kumsema mwenzako just tuambie umefanya nini na una mpango wa kufanya nn
 
Na yule ambaye anachukuaga fedha za CCM hadi za JK 2005 alikunja akastaajabu hajui zina malengo gani
 
- Sijawahi ona kokote siasa inakofanywa mwanachama wa chama kimoja kwa wakati huohuo ni mwanzilishi wa chama kingine cha siasa, sijawahi.

- Sijawahi kuona mtu anajiunga na chama fulani baada ya siku tano anapewa uongozi mkuu wa chama hicho, sijawahi

- Sijawahi kuona popote siasa inapofanywa, mwenyekiti wa chama yupo chini ya mtu fulani. Yahani kikatiba kabisa kuna mtu yupo juu ya mwenyekiti, hii pia sijawahi kuona.

- Sijawahi kuona popote pale chama cha upinzani kukipinga chama cha upinzani na si chama tawala. AGAINST CHADEMA TANZANIA(ACT). Kwa maneno au hata vitendo. Chama kinafanya sherehe kikipata wafuasi wa upinzani kuliko wa chama tawala.

- Sijawahi kuona chama cha upinzani kinafadhiliwa na chama tawala kiuchumi na kimikakati. Tumefanya uzinduzi wa chama chako Zuberi kwa gharama kubwa sana, air time ITV, chakula, ukumbi expensive, na mbwembwe nyingi. Lakini mbona hujawahi kuchangisha pesa toka kwa wanachama wako? Kama kuna mtu anachangia ni nani huyo? Mtamlipaje baadae?

- Sijawahi ona chama cha upinzani popote pale siasa inapofanywa, wafuasi wake ni wale wanachama na wafuasi wa chama tawala. Le mutuz, laki si pesa, musa alani n.k, hii nayo sijawahi ona.

Kwa yote hayo juu Zuberi kwa nini nisikuite kwamba wewe ni msaliti halisi wa demokrasia hapa nchini. Kama kweli wewe siyo msaliti mbona hujawahi kujitokeza na kukataa zile namba za simu walizozitoa chama chako cha zamani kuwa zilitumika katika ufisadi? Mbona sijasikia kuikana ile akaunti ya benki wa yule dada kule ujerumani?

UKINIJIBU HAYO KWA UFASHA WEWE KWELI SI MSALITI.

Kabla hatujaaminishwa hiki kilichoandikwa juu ya Zitto kabwe na ACT,ni bora tupate kwanza majibu ya maswali haya.

Nataka kurudi Chadema mara baada ya .....
Nitayaamini maneno yanayotolewa na
wanachadema siku siku haya maswali
yakipatiwa majawabu
Natamani sana kuwa Kamanda lakini haya
yananitatanisha,naombeni majibu ili nifanye
maamuzi magumu.
1.Walituambia kuwa chama cha wananchi CUF
ni tawi la ccm,wakaenda mbali kwa kuwaita
kuwa ni chama cha Mashoga ghafla wakasahau
matusi yao na wakaanza mashirikiano
Mapya,Je ile tuhuma iliishia wapi?
2.Chadema walituaminisha kuwa Chama cha
NCCR mageuzi kimejaa Usalama wa
Taifa,wakaenda mbali wakamkejeli Mbatia, tena
ndani ya Bunge kuwa,yupo Upinzani huku
akiitumikia ccm,ghafla tu Mbatia ni Mshirika
namba Mbili wa Ukawa bila watanzania
kuelezwa kama zile tuhuma zilikuwa za kweli
au za kutunga kwa nia ya kuwalaghai watu.
3.Chadema kwenye Ilani yake 2010
walituambia kuwa tukiwachagua hawatachukua
posho kama hatua mojawapo ya kuonyesha
kwa vitendo kuchukizwa na matumizi mabaya
ya serikali.Je Kwanini wamekiuka Ilani yao?
4.Chadema Mwaka 2011 walikataa kushirikiana
na vyama vya Upinzani ili kuunda kambi ya
Upinzani yenye sauti na nguvu,wakatuambia
kuwa Vyama vyote ni mawakala wa ccm
isipokuwa Chadema,hivyo kushirikiana nao ni
kurudisha nyuma harakati za ukombozi,ghafla
tu baraza kivuli la mawaziri likavunjwa na wale
vibaraka wa ccm wakaingizwa kwenye kambi
ya upinzani bila sisi wafuasi kuambiwa ni lini
ukibaraka wao umeisha mpaka wakaaminiwa.
5.Tuliambiwa kuwa David Kafulila ni mtu hatari
kwa ustawi wa Upinzani hasa
Chadema,tukaambiwa ni Sisimizi ambae hana
umuhimu wowote ndani ya Chadema ,ghafla tu
Sisimizi kageuka tembo,Mtu hatari kageuka
Shujaa na sasa ananadiwa na viongozi wa
Chadema kuwa ukawa imepata tuzo,Je ni lini
kafulila alianza kuaminiwa ?
6.Tuliambiwa tena kuwa ,Serikali kutumia
mashangingi huku Zahanati hazina dawa ni
kiwango cha juu cha Ubinafsi,Mbowe akalikataa
Shangingi la Kiongozi wa Upinzani....ghafla
nimemuona Bukoba akiwa na Shangingi lenye
maandishi KUB. Je ndio lilelile alilolikataa
hadharani au ni lingine?
7.Mbowe alituahidi kwenda mahakamani,na
kudai kuwa wanasheria wake wanaandaa
mashtaka dhidi ya Zitto Kabwe baada ya Zitto
kumtuhumu kuwa alipokea fedha toka kwa
makada wa ccm na kuwa alicheza dili ns
Kinana kuhusu deni analodaiwa na NSSF.Je
taratibu za ufunguaji kesi ziliishia wapi ?
8. Chadema Mwaka 2011 ilitangazia Umma
kutomtambua Rais Kikwete kwakuwa
alishindwa na Slaa,ghafla wanatangaza kuomba
mashauriano na Rais waliemkataa,wakafika
Ikulu kujadiliana juu ya maswala mbalimbali ya
Kitaifa,wakanywa Juice na kupiga picha,Je ni
lini Chadema ilianza kumtambua Rais na
kwanini sisi wananchi hatukuelezwa kuwa
kuanzia sasa Kikwete ni Rais?
Sina nia ya kuibua Marumbano yasiyotujenga
bali nataka mtu mwenye uelewa mkubwa kuliko
mimi anaondoe Uvulivuli ili nami nijitambue.
Naomba nijibiwe hayo ili nami niwe Kamanda
nitakaeitetea Chadema popote.
Hayo Majawabu yakipatikana,ndio utakuwa
mwisho wa Chama cha ACT-Wazalendo maana
umma utaiamini Chadema na hivyo kuiunga
mkono.
Kama Maswali yakikosa Majibu basi Chadema
itakosa uhalali wa kutuhumu ACT-Wazalendo na
viongozi wake na hivyo wananchi wataendelea
kujiunga na ACT-Wazalendo kwa kuamini kuwa
maneno yoyote yanayotolewa na Chadema ni
Ulaghai.
Karibuni kwa majibu Makamanda ili nasi tupate
chakuwaambia wananchi ili waipuuze ACT-
Wazalendo.
 
Back
Top Bottom