Kwanini watu wanaogopa kufa?

Kwanini watu wanaogopa kufa?

Bonge moja la somo hili. Kumbe sasa kinachotusumbua ni hofu ya future lakini kiuhalisia kama tungeishi the moment hakuna cha kuogopesha si ndio?
Very interested, kumbe hofu ni kuogopa yajayo ambapo si kweli.
Hofu, hasira , upendo na nk hizi ni njia za asili tu za mwili kupata taarifa kuweza kujilinda na kukabiliana na mazingira tu
 
Hofu, hasira , upendo na nk hizi ni njia za asili tu za mwili kupata taarifa kuweza kujilinda na kukabiliana na mazingira tu
Kuna jamaa wanadai haya yote ni jambo lilelile moja ila mawanda tofauti "dichotomy of the same continuum"
Chuki ni upendo katika mawanda ya chini
Kifo ni uhai katika mawanda ya chini.
 
terminal rally ipo na inajulikana , kuomba maji ipo kitabibu kabisa kwa baadhi ya watu , pia baadhi ya watu huwa wanajua wanakaribia kufa, hivyo huweza kuwaomba wapendwa wao ,wakalete kitu ili wa siwaone kwenye hiyo hali.
Unayosema ni sahihi, terminal rally hutokea kwa watu wachache zaidi wanaofariki ila ndio story kubwa zaidi kuliko ya wale wengi ambao huwa wanakufa bila terminal rally yoyote.

Hiyo pia ya baadhi ya watu kutotaka kuonwa saa wanakufa ni kawaida duniani kote, cultures nyingine mtu kama hataki kuonwa huwa anaambia watu wazi kabisa wampishe kidogo saa imefika ila sisi nafikiri ni tofauti ndio mtu anatafuta namna ya kuwaondoa watu kwa kutuma vitu.
 
Unayosema ni sahihi, terminal rally hutokea kwa watu wachache zaidi wanaofariki ila ndio story kubwa zaidi kuliko ya wale wengi ambao huwa wanakufa bila terminal rally yoyote.

Hiyo pia ya baadhi ya watu kutotaka kuonwa saa wanakufa ni kawaida duniani kote, cultures nyingine mtu kama hataki kuonwa huwa anaambia watu wazi kabisa wampishe kidogo saa imefika ila sisi nafikiri ni tofauti ndio mtu anatafuta namna ya kuwaondoa watu kwa kutuma vitu.
Yeah
 
Mimi nimeshuhudia mtu akitapatapa akaitwa jamaa mtu mzima akashauri apewe maji baada hapo alikufa Sasa nilijiuliza huyo aliyeshauri apewe maji alikuwa anajua au hajui alichokifanya mpaka Leo sijapata jibu.
Huenda hata asingempa bado angekufa tu. Ni vile kwa kuwa hamku-experience upande wa kutokupewa maji ungekuaje ndio maana washauri wa kumpa maji wanakuwa blamed
 
Acha uoga na ufungue akili yako.Kuzaliwa na kufa ni biashara ileile moja.

Watu wengi mnaishi kama watumwa wa uoga. Mnaogopa kuzikwa ardhini wakati mmesahau kuwa mmetoka kwenye giza nene kule tumboni kwa mama zenu.

Na Kifo ni kurudi huko huko ulipokuwa kabla ya kuzaliwa, maana hii ni hali moja.

Mimi siogopi kufa hata sekunde moja, kwa sababu najua kabisa sikuogopa wakati nazaliwa. Kuzaliwa na kufa ni jambo lilelile. Wale wanaopiga mayowe na kulia sana kwenye mazishi ni watu wasiojua hesabu rahisi za maisha.

Kifo ndicho kinachofanya maisha haya yawe na thamani, maana tunarudi kule kule tulipokuwa kabla ya kuzaliwa.

Mimi na wewe ni wasafiri tu hapa. Acha kulialia na kuleta uoga wa kijinga. Tunarudi kule tulikokuwa kabla hatujazaliwa.

Ulikuja hapa duniani huna hata nguo ya ndani, huna jina, huna hata mia mbovu mfukoni.

Hivyo basi hakuna haja ya kuogopa kufa ingali unajua hukuogopa kabla hujazaliwa...

Kifo ni kurudi kule kule. Kama hukulalamika ukiwa ndani ya tumbo unazaliwa, unalalamika nini unaporudi kufa?.

Wakati hali ni zile zile, kufa na kuzaliwa ni kitu kile kile...

Kwaiyo hakuna haja ya kuogopa utakufaje kufaje.

Wewe kazi yako ni kuishi, Kwani siku unazaliwa, ulijua utazaliwa vipi? Ulijua kama utazaliwa salama au kwa shida? Hukujua! Asili ilikutoa huko ulikokuwa na ikakuleta hapa duniani salama. Ikiwa asili iliweza kukuleta, ina uwezo wa kukurudisha bila kukuomba ushauri.

Acha kimbelembele cha kutaka kupangia asili namna ya kukutoa!

Unajifanya unawajali sana ndugu zako, lakini ukweli ni kwamba unaogopa nafsi yako! Kabla hujazaliwa, hao ndugu walikuwa wanakula na kulala vizuri tu. Na ukishasepa, wataendelea na maisha yao, watakula pilau kwenye msiba wako, na maisha yataendelea.

Wacha wasikuelewe, wacha waone unaweweseka, lakini wewe simamia ukweli mmoja Kuzaliwa na kufa ni biashara moja, Hakuna kuogopa.
Hii ni stoicism, mawazo waliyokuwa nayo akina Zeno of Citium na kuendelezwa na akina Markus Aurelius na wengine Stoicism (Stanford Encyclopedia of Philosophy).

Ndio tutakufa kama tulivyozaliwa lakini that's not all about life. Na ukipenda kujua maisha yana maana gani, basi yape maana wewe mwenyewe. Bila hivyo utafikiri maisha ni kuzaliwa na kufa basi.
 
Kuna dini zinaambia watu wakifa usiku wa kwanza kaburini watawekwa mtu kati.😀

Nani haogopi kipigo?
 
Back
Top Bottom