Watu mnaleta udini,utamaduni kwamba ndio chanzo cha umasikin wa pwani. Kwanza tusahihishane hapa, PWANI YOTE SIO MASIKINI. Point ni hii watu wengi wa pwani hawajakwenda shule tu ila sio masikini. Umasikini upo Tz yote, mikoa ya bara kama singida, rukwa,kagera,ruvuma,iringa ni masikini tu na kiuhalisia Tz yote ni masikini. Suala la utamadun halina mantiki maana huko bara kuna mambo ya ajabu sana. Mimi nimetembea mikoa mingi Tz najua hali ya uchumi wa watu wa vijijin. Wewe umehamia kimara mwaka jana unamcheka wa bugurun masikin kumbuka kuwa wale ndugu zako walio masikin kule kijijin kwenu si wanaendelea kuish palepale miaka na miaka, sasa ulitaka mtu wa mbagala, temeke, bugurun, gongo la mboto, kigogo n.k aende wapi wakati pale ndio kijijin kwao na ile ndio hali yake kiuchumi kama wale ndugu zako kijijin kwenu. Ndio maana ukienda maeneo tajwa hapo juu utakuta nyumba za miaka ya zamani tangu ukolon sababu tangu zaman wanakaa hapo yaani hapo ndio kijijin kwao. Mwaka 1973 manzese ilikua makaz ya watu lkn eneo kilipo kiwanda cha urafiki lilikua mashamba ya minaz na mikorosho just imagine wale wa manzese tangu 1973 unadhan kijiji chao wapi kama sio palepale. Kukaa bonyokwa kimara maeneo ya miliman kule, mwenge,mbezi n.k isiwe sababu bcoz maeneo hayo yanakaliwa na watu waliosoma na wana vipato vizuri. Kamlete yule mjomba wako wa Isimani uone kama ana uwezo wa kukaa mbezi. Suala hapa walikosa elimu watu wa pwani sababu hawakuithamin elimu hii ya mkoloni lakin wachache walisoma pia wana maisha mazuri na sio masikin na wanaish huko huko wanakoish akina masanja, mwaigomole, mihayo, nkya, mndeme n.k. Ndio maana ukimuona mtu wa bara asiye na elimu na kipato hana utamuonea huruma namna anavyoishi. Nenda Moshi uone wakina mama na ndizi kichwani kilometa kadhaa on feet to town looking for their incomes. Tanzania yote masikini tu hasa huko vijijin. Wabara Wachache mlio mjini msiwadharau wa mliowakuta hapa mjini maskin na kuwabeza hapa ndio kijijin kwao. ibada ya swala tano sio kigezo cha kuwa masikin- nchi za kiarabu mbona tajiri na wanaswali kuliko hao watu wa pwani(mwenye point hii hakua na logic) au kuoa mitala na kuzaa watoto wengi nako ni sababu? Wasukuma wanafamilia kubwa kubwa sana tu na Wakurya wanaoa wanawake wengi tena zaid ya waislamu wa pwani na wanafamilia kubwa sana tu na wao masikini sababu ni nn?
Msilete udini na ukanda hapa
MTOA MADA UNGEJIULIZA KWANINI VIJIJIN KUNA UMASIKINI ULIOKITHIRI nafikir ungepata majibu mazuri, hapa watu wanaleta udini na ukanda.....nyambaf
Am out, leave ur comment. ciao