Kwanini watu wa Pwani wengi ni masikini?

Kwanini watu wa Pwani wengi ni masikini?

Status
Not open for further replies.
Mkuu wabara ni watu wa wapi?

ni opposite ya wapwani.
Anyway the whole idea to my post ni kumjibu mleta mada ya kuwa watanzania wote ni maskini bado nchii hii tuna safari ndefu kufikia maendeleo ya kweli ya kuondokana na umaskini . hakuna cha pwani wala bara wote ni hali moja.
Anaefikiri wanaotoka sehemu fulani katika nchi wameendelea uwezo wake mdogo sana.
kila sehemu kuna waloendelea walosoma na wasasa..lakini hawa ni wachache sana na chini ya asilimia 5 ya watanzania
45m .
nchi zilizoendelea hauwezi kuona tofauti kati ya watu waishio mijini na wale wa country side.tuna safari ndefu kufika huko
 
Ulimuona wapi MTU wa pwani akawa omba omba,Dar wamejaa watu Dodoma,Morogoro,Singida,Mwanza,Shinyanga,wanalala kwenye mabaraza ya wahindi,na watoto wao.Maeneo yote ya bara alikopita mzungu maisha magumu.Ndio mana wabara wengi wanakimbilia mikoa ya Pwani.Dar imeanzishwa na muarabu angalia ilivyo na maendeleo.Na ustaraabu wa wenyeji,na mji ulivyo na bandari nzuri aliyoianzisha muarabu.Lakini miji aliyokuwako mzungu mpaka leo maendeleo hakuna,umaskini wa kutupwa.Miji haikupangika,miundombinu ya ovyo.
you are very dumb my friend, watu wa pwani wanaoishi dsm wengi wao bado ni masikini sana, wanaishi buguruni, temeke, pugu, gongo la mboto, mbagala, manzese, tandale, magomeni, kigogo to mention a few. nenda kimara, mikocheni, mwenge na maeneo mengine ya watu wa bara uone kama hali yao sawa na ya wapwani. tatizo kubwa la watu wa pwani ni elimu, hawajali kabisa elimu kama wanawake wanawaza tu kuolewa, kama wanaume wanawaza tu kazi ndogondogo kuchoma chips na kuoa mitara.
 
Hayo ya kireno na kiingereza Ndio POROJO!
Kwanza hilo neno "POROJO" peke yake linatokana na neno la KIARABU "BUROJJ"!!!

Yaani unaweza kuadhirika hapa.y

Na KUADHIRIKA pia ni neno la KIARABU litamkwalo ".. ilaa haadhira"

naona niishie hapa. Manake kila nilikiendelea basi na kiarabu kinaongezeka tu!
hakuna..kiswahili ni kibantu tumekopa kiarabu maneno mengi lakini kiswahili ni kibantu.
 
Wengi watadhani walosababisha umasikini wa Pwani ni Waraabu lakin sio Waarabu!!!!!!Soma historia vizuri na miongoni mwa miji iliyokuwa kibiashara miji iliyomasikini leo ndo iliwika katika Historia. Angalia miji ya wenzetu Afrika miji iliyosifika leo ikoje? Ni vyema watu wakatafakari na kufanya utafiti na kuja majibu, Nikirejea historia vyama vya kupigania uhuru vilianza Pwani mfano katika mashamba ya mikonge yanakopatikana Pwani na kwingineko maeneo ya Pwani (kwa maana hiyo walikuwa na upeo mpana wa kutafuta maisha bora kuliko jamii nyingine). Umasikini wa Pwani, Tanga, Lindi, Mtwara, Kigoma, Tabora, Morogoro na Singida ni wa kufanyia uchunguzi (utafiti ni nini chanzo cha kurudi nyuma) pasije pakawa na hila za kuzamisha jamii za Pwani na watu wa aina hiyo. Ni vyema Waarabu wasilaumiwe kwa umasikini wa Pwani kwani ni Uongo wa dhahiri kuwa wamesababisha umasikini. Nakataa kwa mujibu wa vitabu vya historia ya Tanganyika, Afrika mashariki na Afrika kwa ujumla. Kama vitabu vya historia vinasema uongo basi Waraabu hawakuja, Wazungu hawakuja na Wamisionari hawakuja. Kama wote walikuja Tanganyika basi Umasikini hujasababishwa na Waraabu tutafute sababu nyingine lakini sio kuwalaumu Waraabu kwa kusababisha umasikini Tanganyika hasa jamii iliyoiga mila na mienendo na tamaduni za Kiarabu.
 
Hiyo pwan mmesahau kuwa ndio ilikua miji mikubwa afrika iliyoendelea na iliyokua inamiliki dola mpaka bara vasco da gama alipofika kilwa aliikuta newyork jiulize uko bara miaka hiyo kulikuaje
 
Hao maskini unawalisha ? Unawavesha? Unawasomeshea? Au kila ulifikirialo unatoka nalo?
Blood msondongoma wee!
 
Unapozungumzia watu wa pwani unazungumzuia wakazi au wazaliwa wa Pwani popote walipo? Kwakukumbusha tu Mkoa wa Singida na Tabora ni masikini zaidi ya Pwani.

maeneo mengi yaliyotawaliwa na waarabu ni masikini.kwanza utakuta elimu duni, miundombinu duni
 
Watanzania walio wengi ni masikini haijalishi wanatoka pwani au bara.

Kuwa tajiri na kwenda mbinguni ni mtihani ambao Nyerere alisema ni sawa na "ngamia kupita katika tundu ya sindano".

Unamuamini Nyerere?

Faiza hayo ni maneno yaliyo kwenye vitabu vya dini Nyerere alinakili tu.
 
Wamisionary walikopita walieneza elimu jiulize huko unakotaja kiwango cha elimu kikoje kwa wazaliwa.kazi unaweza kufanya lakini maarifa kidogo na tija ni ndogo
Ha ha ha!
Waliipata wapi kama si kutoka kwa Waislamu?

Najua leo utashangaa sana kusikia kuwa baada ya kuanguka Roman Empire ni Waislamu ndio waliokuwa wakisambaza elimu na maendeleo duniani.

Kumbuka miji kama Cordoba, Valencia na mingineyo ya Iberia au Spain ilipokuwa chini ya Waislamu ilikuwa na taa za barabarani, mifumo ya kusambaza maji,barabara, vyuo vikuu n.k wakati miji kama ya Paris na london ikiwa giza.

Kuifunika historia hii Wazungu wanakiita kipindi hiki kuwa ni "dark ages"
 
you are very dumb my friend, watu wa pwani wanaoishi dsm wengi wao bado ni masikini sana, wanaishi buguruni, temeke, pugu, gongo la mboto, mbagala, manzese, tandale, magomeni, kigogo to mention a few. nenda kimara, mikocheni, mwenge na maeneo mengine ya watu wa bara uone kama hali yao sawa na ya wapwani. tatizo kubwa la watu wa pwani ni elimu, hawajali kabisa elimu kama wanawake wanawaza tu kuolewa, kama wanaume wanawaza tu kazi ndogondogo kuchoma chips na kuoa mitara.

Hao wa mbezi wengi wao ni mijizi tu serikalini
 
Unapozungumzia watu wa pwani unazungumzuia wakazi au wazaliwa wa Pwani popote walipo? Kwakukumbusha tu Mkoa wa Singida na Tabora ni masikini zaidi ya Pwani.

Takwimu sahihi zinasema Watanzania wengi ni masikini, na wanaishi kwa dola moja au chini ya dola moja ya kimarekani kwa siku.

Hao watu wa Pwani wengi unaodai ni masikini wanawakilisha chini ya robo ya Watanzania wote, sasa unasemaje watu wa Pwani ni masikini? Labda wewe umetembelea Pwani zaidi ya sehemu nyingine za Tanzania, lakini mimi naona sehemu kubwa ya Watanzania waliopo vijijini ni masikini.

Hali ya umasikini vijijini ipo Dodona, Singida, Tabora, Kigoma na sehemu nyingine. Kama ipo tofauti ni ndogo sana, ambayo kwa sehemu kubwa inasababishwa na miundo mbinu duni.
 
Watanzania walio wengi ni masikini haijalishi wanatoka pwani au bara.

Kuwa tajiri na kwenda mbinguni ni mtihani ambao Nyerere alisema ni sawa na "ngamia kupita katika tundu ya sindano".

Unamuamini Nyerere?

Faiza, Nyerere alikuwa anamnukuu Yesu.

Kwa hiyo swali lako liwe...unamwamwini Yesu?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom