Uwekezaji unategemea mambo mengi, ukiona viwanda vilivyopo pwani na dam, ujue waliowekeza siyo individuals/siyo wenyeji pia. Wawekezaji wanaweza kuwa makampuni ya ndani na nje, yanaweza kuwa serikali na mashirika yake n.k kwa kutegemea na mazingira na miundombinu.Kwa nini sasa tusirudi ku-invest kwenu, maana umegusia hakuna viwanda na biashara za kukuza miji, we huoni ni muda sasa wahaya kurejea makwao na kuanza kujenga kama walivyofanya wamisri?
Ki ukweli uwezi kulinganisha maisha ya mtu anayeishi maisha nyumba ya bati dar, na mtu anayeishi nyumba nzuri bukoba... Dar es salaam expenditure ni kubwa kuliko kagera, huyo mtu anayeishi maisha ya kwenye nyumba za bati uchumi wake au pato lake kwa siku anaweza kumzidi mtu anayekaa nyumba nzuri karagwe...
Ifike muda sasa wahaya turudi na kuanza kuboresha majumbani kwetu, na kwenye miji yetu na kufungua biashara za maana... utakuta Mhaya huyo huyo anamiliki mashule, maduka na biashara nzuri Mwanza au Dar, lakini anashindwa kuwekeza kagera
Kwa hiyo usiwalaumu wenyeji