Kwanini Wapalestina waliisaliti Tanzania na kumuunga mkono nduli Idd Amin kupigana?

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
20,897
63,784
Tanzania ilikuwa moja ya nchi kinara barani Afrika kutetea haki za Wapalestina. Nchi hii ilienda mbali na kuamua hata kuvunja mahusiano ya kidiplomasia na nchi ya Israel mwaka 1973 baada ya shinikizo la nchi za kiarabu zilizokuwepo ndani ya O.A.U kuwa kubwa.

Ikumbukwe Israel walikuwa na mchango mkubwa kwa Tanzania kuliko hata Palestine, kwasababu wao ndiyo walisaidia katika kufundisha maafisa wengi wa jeshi la Tanzania, akiwemo Marehemu Generali Muhiddin Kimario, pamoja na kusuka JKT.

Mwaka 1973, baada ya vita vya Yom Kippur nchi nyingi za Afrika zilivunja mahusiano ya kidiplomasia na Israel, na kuanza kutetea haki za Wapalestina. Ukisoma nyaraka za OAU, moja katika falsafa inazozipinga ni UZAYUNI (ZIONISM) na UBAGUZI WA RANGI (APARTHEID).

Tanzania ilikwenda mbali na kuanza kutetea haki za wapalestina kule UN. Kinachoshangaza ni kwamba Palestine Liberation Organization (PLO), mbali na kuwa marafiki wa Tanzania, walijiunga na vikosi vya Libya katika kumsaidia Idd Amin ambaye alikuwa anapambana na Tanzania.

Ikumbukwe tu, mwaka 1973 Tanzania ndiyo ilikuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuitambua PLO na kuruhusu kundi hilo kujenga makao yake jijini Dar es salaam. Ofisi za PLO jijini , Dar es salaam ndiyo yalikuwa makao makuu ya PLO barani Afrika. Katika moja ya nukuu ambayo Mzee Nyerere aliwahi kuitoa kuhusu Palestina ni hii:

"Kizazi chetu kilikuwa kizazi cha mapambano ya utaifa kwa ajili ya uhuru wa nchi zetu … lakini hali ya Wapalestina ni tofauti sana na mbaya zaidi, Wamenyang’anywa nchi yao wenyewe, Kwa hiyo wanastahili kuungwa mkono na Tanzania na dunia nzima"

Najiuliza tu, chanzo kikubwa cha PLO kuisaliti nchi ambayo ilikuwa inawatetea hivi ni nini ?

Arafat 2.jpeg

 
Tanzania ilikuwa moja ya nchi kinara barani Afrika kutetea haki za Wapalestina. Nchi hii ilienda mbali na kuamua hata kuvunja mahusiano ya kidiplomasia na nchi ya Israel mwaka 1973 baada ya shinikizo la nchi za kiarabu zilizokuwepo ndani ya O.A.U kuwa kubwa. Ikumbukwe Israel walikuwa na mchango mkubwa kwa Tanzania kuliko hata Palestine, kwasababu wao ndiyo walisaidia katika kufundisha maafisa wengi wa jeshi la Tanzania, akiwemo Marehemu Generali Muhiddin Kimario, pamoja na kusuka JKT.

Mwaka 1973, baada ya vita vya Yom Kippur nchi nyingi za Afrika zilivunja mahusiano ya kidiplomasia na Israel, na kuanza kutetea haki za Wapalestina. Ukisoma nyaraka za OAU, moja katika falsafa inazozipinga ni UZAYUNI (ZIONISM) na UBAGUZI WA RANGI (APARTHEID). Tanzania ilikwenda mbali na kuanza kutetea haki za wapalestina kule UN. Kinachoshangaza ni kwamba Palestine Liberation Organization (PLO), mbali na kuwa marafiki wa Tanzania, walijiunga na vikosi vya Libya katika kumsaidia Idd Amin ambaye alikuwa anapambana na Tanzania.

Najiuliza tu, chanzo kikubwa cha PLO kuisaliti nchi ambayo ilikuwa inawatetea sana ni nini ?​
Porojo la kanisani hili ulioandika
 
Tanzania ilikuwa moja ya nchi kinara barani Afrika kutetea haki za Wapalestina. Nchi hii ilienda mbali na kuamua hata kuvunja mahusiano ya kidiplomasia na nchi ya Israel mwaka 1973 baada ya shinikizo la nchi za kiarabu zilizokuwepo ndani ya O.A.U kuwa kubwa. Ikumbukwe Israel walikuwa na mchango mkubwa kwa Tanzania kuliko hata Palestine, kwasababu wao ndiyo walisaidia katika kufundisha maafisa wengi wa jeshi la Tanzania, akiwemo Marehemu Generali Muhiddin Kimario, pamoja na kusuka JKT.

Mwaka 1973, baada ya vita vya Yom Kippur nchi nyingi za Afrika zilivunja mahusiano ya kidiplomasia na Israel, na kuanza kutetea haki za Wapalestina. Ukisoma nyaraka za OAU, moja katika falsafa inazozipinga ni UZAYUNI (ZIONISM) na UBAGUZI WA RANGI (APARTHEID). Tanzania ilikwenda mbali na kuanza kutetea haki za wapalestina kule UN. Kinachoshangaza ni kwamba Palestine Liberation Organization (PLO), mbali na kuwa marafiki wa Tanzania, walijiunga na vikosi vya Libya katika kumsaidia Idd Amin ambaye alikuwa anapambana na Tanzania.

Najiuliza tu, chanzo kikubwa cha PLO kuisaliti nchi ambayo ilikuwa inawatetea sana ni nini ?​
Kumbuka hata walipoteka ndege ya Israel waliipeleka uganda idd amin akawasaidia kuhifadhi mateka.
Hii iko wazi walikuwa karibu na Idd Amin zaidi
 
Kwenye vita kila mmoja huchagua upande kulingana na muono wake,huenda Palestine kupitia PLO waliona Idd Amin alikuwa sahihi hivyo kujivua unafiki wa kutoa msaada kwa rafiki ambaye anavunja haki za msingi za wengine.

Mimi binafsi huwa najiuliza nini sababu kuu ya vita ya Kagera ikiwa tayali kulikuwepo kwa Mogadishu accord ya 1971 ( Sina hakika sana na mwaka na niko tayali kusahihishwa).
 
Kwenye vita kila mmoja huchagua upande kulingana na muono wake,huenda Palestine kupitia PLO waliona Idd Amin alikuwa sahihi hivyo kujivua unafiki wa kutoa msaada kwa rafiki ambaye anavunja haki za msingi za wengine.

Mimi binafsi huwa najiuliza nini sababu kuu ya vita ya Kagera ikiwa tayali kulikuwepo kwa Mogadishu accord ya 1971 ( Sina hakika sana na mwaka na niko tayali kusahihishwa).
Vita vya Uganda kumuondoa iddi amini ............
 
Idd Amin alituwin kwenye propaganda na alifanikiwa kuzishawishi nchi za kiarabu kwamba Nyerere anamvamia yy kwa sababu mi mwisilamu, ndo maana dictator Gadafi alikua aggressive sana kumsaidia Amin
Huwezi ona taifa jirani linahifadhi waasi alafu ukawa unawachekea hovyo,hiki ndicho alicho kuwa anafanya Tanzania kwa kuwa hifadhi baadhi ya viongozi walio pinduliwa wa Uganda.

Pia Kuna Mogadishu accord ilisainiwa Kati ya Tanzania na Uganda ili kutoa tishio la Vita.
 
Huwezi ona taifa jirani linahifadhi waasi alafu ukawa unawachekea hovyo,hiki ndicho alicho kuwa anafanya Tanzania kwa kuwa hifadhi baadhi ya viongozi walio pinduliwa wa Uganda.

Pia Kuna Mogadishu accord ilisainiwa Kati ya Tanzania na Uganda ili kutoa tishio la Vita.
Mkuu kua serious kidogo!

Kwa hyo ndo sababu ya Uganda kuvamia nchi yetu?
 
Mkuu kua serious kidogo!

Kwa hyo ndo sababu ya Uganda kuvamia nchi yetu?
A delegation from Brunei Kingdom inspects one of the sites in Nkozi, Mpigi District on Friday for the establishment of a University in memory of Idi Amin. PHOTO | JOSEPH KIGGUNDU
...
Propaganda za kanisa dhidi ya Iddi Amin
 
Tanzania ilikuwa moja ya nchi kinara barani Afrika kutetea haki za Wapalestina. Nchi hii ilienda mbali na kuamua hata kuvunja mahusiano ya kidiplomasia na nchi ya Israel mwaka 1973 baada ya shinikizo la nchi za kiarabu zilizokuwepo ndani ya O.A.U kuwa kubwa. Ikumbukwe Israel walikuwa na mchango mkubwa kwa Tanzania kuliko hata Palestine, kwasababu wao ndiyo walisaidia katika kufundisha maafisa wengi wa jeshi la Tanzania, akiwemo Marehemu Generali Muhiddin Kimario, pamoja na kusuka JKT.

Mwaka 1973, baada ya vita vya Yom Kippur nchi nyingi za Afrika zilivunja mahusiano ya kidiplomasia na Israel, na kuanza kutetea haki za Wapalestina. Ukisoma nyaraka za OAU, moja katika falsafa inazozipinga ni UZAYUNI (ZIONISM) na UBAGUZI WA RANGI (APARTHEID). Tanzania ilikwenda mbali na kuanza kutetea haki za wapalestina kule UN. Kinachoshangaza ni kwamba Palestine Liberation Organization (PLO), mbali na kuwa marafiki wa Tanzania, walijiunga na vikosi vya Libya katika kumsaidia Idd Amin ambaye alikuwa anapambana na Tanzania.

Najiuliza tu, chanzo kikubwa cha PLO kuisaliti nchi ambayo ilikuwa inawatetea sana ni nini ?​
Ilikuwa udin...


God Bless Israel
 
Back
Top Bottom