Kwanini wanawake wengi wetu hatupendani?

Kwanini wanawake wengi wetu hatupendani?

Btw, watu wengi wanabidi wafanyie kazi sana utu wao wa ndani ndipo watafufuka upya. Wivu, husda, roho mbaya ni dalili za wazi kuwa umekufa "inside you". Ukiwa vizuri inside you vitu vingi havitakupa shida.
 
Naona ushaidi wa wazi huu hapa heloo!

Yaani anakutuhumu wewe ni ME kisa tu umeandika kitu asichokubaliana nacho!!! duuh!
Hata Mimi nimeshangaa sana.Walau Umeona kidogo.Wanawake hatupendani.Na huwa najiuliza kwa nini inakuwa hivyo.
 
Tuna mambo ya ajabu ajabu tuuu yasiyokuwa na msingi na wivu wa kijinga,hatupendi kuona mwanamke mwenzako anafanikiwa katika jambo fulani
 
Mi naona hii ni nature yetu tumeubwa tofaut sana na wanaume so ni kawaida na haiwez kubadlika
 
Huwa nasikia wanawake hampendani ila sjathibitisha kama kweli mpo hivo

Nachojua hata sis wanaume baadhi yetu hatuna upendo kati yetu.
Kweli,Hata baadhi ya wanaume hawapendani
 
Haaa haaa Hata mawifi ndo balaaa( ukiwepo sifa atakazomwagiwa Sasa.Mkiondoka(' kaka bwana Wanawake wote kamuona yule vimguu kama spoku za baiskeli
Hahahaaaa....kama ulikuwepo.,halafu unakuta na wao miguu yao kama stick za meno
 
Actually binadamu wote tuna wivu na wivu huo ukizidi mara nyingi uzaa chuki ndani yake, ila sema kwa wanawake uenda mbele zaidi na kuzianika wazi wazi na hapo ndipo tunapata ile kauli ya "wanawake hawapendani"
Kabisa.
 
Kabisa mkuu inapunguza sana, kuna mtu mnaweza mkaishi nae poa tu nyumba moja kwa kipindi kirefu ila siku mkizinguana tu anakumbushia hadi maudhi yako ya 2013 ambayo wewe ulikuwa huyajui. siku zote hizo alikuwa anaumia tu moyoni.
Huu nao Ni ugonjwa.
 
Wanawake pendaneni basi.

Unajua sisi ndio inatakiwa tujifunze upendo kutoka kwenu. Kwanza nyie ndio viumbe wenye uhuruma sana katika jamii ya binadamu.
Sawa sawa.Ushauri mzurii
 
Wakati nipo chuoni hostel nyingi za wadada unakuta kwenye chumba wanakaa either watatu au wanne na huwa wanajipikia cha kushangaza kila mmoja wao anajipikia kivyake anajiko lake na sufuria zake ikanishangaza kweeli......
 
Huyo mama aliyetaka kupeleka nguo kwa ndugu ni mwanaume? Na hizo nguo alitaka kupelekea wanaume tu? Tabia nyingi ulizotaja hapo zinaendana na uwezo na hadhi. Hata wanaume wa uwezo na hadhi ya chini wana tabia hizo hizo. Wanakaa barazani wakinyoana na kula kashata huku wakimjadili kila anayepita. Kuna msemo kuwa "simple minds discuss people". Ukienda saluni za ushuani utaenda saluni moja mwaka na kitakachokuwa kinaongea ni TV tu. Kila mtu yuko busy na mteja wake na mteja na simu yake au kitabu chake.

Kwenye kupeana kura mwanamke aliyeambiwa hawezi na akaamini anaweza asiamini kuwa mwenzie anaweza. Hata hivyo tuna wanawake wengi tu ni viongozi wa kuchaguliwa na hawajaolewa wala hawana watoto na wamechaguliwa na wanawake wenzao kwani ndo wapiga kura wengi. Kwa hiyo msemo wa wanawake hatupendani ni propaganda zaidi kuliko uhalisia. Mwanamke anayejitambua hawezi kumpa kura mwanamke na kumnyima mwanaume kwa sababu ya jinsi zao.
Point iliyokuwepo 'wengi wetu' hatupendani.Ukiisoma Tena utaelewa.
 
Back
Top Bottom