Gulio Tanzania
JF-Expert Member
- Jan 30, 2018
- 2,130
- 4,469
Waambie waache kwanza kupiga mizinga waache dharau waache ujuaji wawe wanyenyekevu kwa wanaumeHello WanaJf
Bibi yangu Rukia kuna siku aliniuliza Mjukuu wangu unajua kwa nini wanawake wengi wa kizazi cha sasa hawaolewi?
Mimi: Hapana Bibi
Bibi: Hii ndiyo sababu mjukuu wangu "Kuonja onja umeshashiba".
Mimi: Inamaana gani bibi?
Bibi: Nikimaanisha kwamba mambo yanayopatikana kwenye ndoa wanaume wa kizazi cha sasa wanayapata kabla ya kwenye ndoa . Kama vile kufuliwa, kupikiwa na mambo mengine ya ndani ya ndoa. Hii inapelekea kwa kiasi kikubwa kupoteza hamu ya ndoa na zana nzima ya ndoa kati ya wahusika hao wawili na kusababisha kushiba kwa wanaume kunakotokana na kuonja onja na kupelekea kushiba.
HUU NI MTAZAMO WA BIBI YANGU, JE WEWE UNAMTAZAMO GANI KUHUSIANA NA HILI?