Kwanini wanaume wengi hufeli swali hili wakitongoza?

Kwanini wanaume wengi hufeli swali hili wakitongoza?

Hili la namba silifahamu sana. Ila huwa napenda sana kuanzisha mazoea. Hata haichukui wiki 2. Hata humtamkii Nakupenda. We call it love by action.
 
Ningekuwa mimi ningejibu hivi.

3. Kuna rafikiyo ambaye ni msiri wangu ndiye aliyenipa namba yako kwa masharti kwamba nisilitaje jina lake kwako iwapo ungeniuliza. Kwa kuwa nimekula kiapo, siwezi kumsaliti.
Namba tatu ilinikosesha mrembo daaah
 
Mwanaume bila kujiamini mi sawa na bure, unamjibu tu kuwa namba yako niliomba kwa baba yako kwa vile nilikuwa na shida ya kuongea na wewe.
Tatizo liko wapi

[emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] eerf ssertS
 
Zamani mimi nlikuwa nawaambia NIMEOKOTA SIMU ,SASA KATIKA KUPEKUA KWENYE NAMBA ILI NIMPATE ANGALAU MTU WA KARIBU WA HUYO ALIYEPOTEZA NDO NKAJIKUTA NAKUPATA WEWE KWASABABU NAMBA NYINGINE ZOTE HAZIPATIKANI NA NYINGINE HAZIPOKELEWI , HIVO NLITAKA KUJUA KAMA KUNA MTU WAKO WA KARIBU ALIYEPOTEZA SIMU HIVI KARIBUNI?.. (hapo lazima ataniuliza nimeiokota sehemu gani, mimi ntamtajia eneo lolote tu lenye mkusanyiko wa watu hata kwanye daladala, alafu
na atataka nimtajie hiyo namba aangalie kama anamfahamu huyo aliepoteza simu, nitakata simu kujifanya ndo naangalia alafu ntampigia kisha ntamwambia either namba imefungiwa so haiwezekani kuangalia usajili, au ntamtajia namba yoyte nliokuwa nayo ambayo haipatikani au imefungiwa, yaani nnaeza nkamtajia hata namba yangu ya zamani, BAADA YA HAPO HUO MTEGO NTAKUWA NSHAUEPUKA SO KINACHOENDELEA NI KULA KUKU KWA MRIJA,
zipo njia nyingi saana aisee ila nimeitoa hiyo moja kama mfano tu.
Daaah we jamaaa
 
unajua mambo mengi yanayofanywa na mabinti au vjana wa siku hz ni sampuli flani ya ushamba mara nyngi binti mtazamo wake unakuwa upo tu pale endapo mwanaume anamjibu vzur ndie anaamini yuko sawa kwa kumuoa,lkn ni jambo ambalo si kwel,unaweza kujibiwa vzur na ukaamin kisha ukalidhika kumbe unajikuta unayatafuta matatzo bila wewe kujijua, na mwanamke ambae anakuuliza umepata wap namba yangu,au nani amekupatia JIBU LAKE NI DOGO TU!MJIBU YA KWAMBA, mtu alie nipa namba si tatzo kwako,au namna niliotumia kuipata namba sio muhimu kwako na kwangu pia ila la muhimu kwako ni kujua mimi ni nani?naishi wapi na pia nataka nini kutoka kwako,na lengo kuu la kukupigia wewe ni nini au kitu gani, kisha muulize je ungependa kunisikiliza au huitaji? Kumuuliza mwanaume hvyo sio tatzo je akikujibu amenipa huyo unae heshimiana nae pia si tatzo ila tatzo ni wewe kushindwa kunisikiliza kama ataki pia BASI ACHANA NAE ,TENA MWAMBIE HUNA ADABU KISHA MKUMBUSHE YA KUWA AJIFUNZE KUWA STARA NA MWENYE HEKIMA, na kingine nyinyi wanaume wachache ndio mnaowafanya wanawake wawe wajinga, na wapuuzi kwa kuwa na vijimaswali vya kishenzi kishenzi kwa lazma muwe na mitazamo ilionyooka na sio kujiwekea uoga tambueni mwanamke ameumbwa na amedhaliwa kuwa mtawaliwa kupitia misingi ilio bora sasa mkiwa mnawa acha tu!wanakuwa na vimatamshi vya ajabu mnawapa uelewa wa kjinga na mke anapaswa kuwa na misingi ya kike ilio ktk stara njema na mke mwenye masuali ya namna hiyo yana ashiria jike hilo ni jike lililo poteza mishipa ya aibu nalipo mahususi kwa kumpanda mwanaume kichwani ,tena nikumbushe kitu hapo wanaume wanao kata simu zao baada ya kuulizwa msiwaone wajinga au hawajui kutongoza jueni kuwa wanaepuka balaa ambalo angelisogeza ndani ya chumba chake kwa hyo usione sifa kwa hlo jambo.namalizia kwa kusema hata wewe unaeuliza jambo hlo unamatatzo na inawezekana ndie/color]
 
Huwa wanawake wa hivyo Mimi siwatongozagi siku hio hio.

(Simu inaitwa na kupokelewa sauti ya kike upande wa pili inasikika).

Demu: Hello
Mimi: Hello mambo
Demu: poa.
Mimi: Nambie
Demu: Mmmmmh! (Kmya kidogo) kwani nani mwenzangu?

Mimi: ooh sorry. Nitakuwa nimekosea namba.
Demu: Ok.
Mimi: Poa. Bt sorry kwa usumbufu.
Demu: Usijali, kwani ulikuwa unampigia nani?
Mimi: Dada yangu.
Demu: Sawa, utakuwa umekosea namba.
Mimi: poa, ila nimeinjoi kuongea na wewe.

Demu: kwa nini?
Mimi: una sauti nzuri kweli.
Demu: Mmmmh! Ahsante.

Mimi: nadhani unafanana na sauti yako.
Demu: Badae Bhana coz sa hivi ninakazi.

Mimi: Daa samahani kwa kukupotezea muda jaman.
Demu: wala hujanipotezea muda. Badae jioni nipo free.

Mimi: Basi ntakutafuta hiyo jioni.
Demu: sawa ila angalia hiyo namba vizuri.
Mimi: Poa. Byyeee
Demu: oewky.(simu inakatika).

Jioni ikafika.
(Nachukua simu natuma text kwa yule demu).

Mimi: Mambo (inapita dakika tano text haijibiwi. Baadaye text inaingia kwa simu yangu).

Demu: poa nambie.
Mimi: niko fresh mrembo.
Demu: mmmh! Aliyekuambia Mimi mrembo ni nani na hujawahi kuniona?

Mimi: Nilikuambia Sauti yako inatosha kunijulisha kuwa wewe ni zaidi ya mrembo labda uniwie radhi kwa kukuita mrembo kwani wewe ni zaidi ya mrembo.

Demu: mmh! Makubwa(huku akicheka).
Mimi: Umenisamehe lakini?
Demu: nimekusamehe?
Mimi: ndio
Demu: kwani umenikosea nini?

Mimi: si nimekuita mrembo wakati wewe ni zaidi ya mrembo.
Demu: hahaahaaaaa!! Unamambo wewe. Sipati picha demu wako.

Mimi: unanisingizia tuu. Wala sina maneno zaidi ya kuongea ukweli.

Demu: (anacheka kidogo) tuachane na hayo. Ulimpata Dadaako.

Mimi: Ndio. Aah! Kumbe nilikosea namba ya mwisho.
Ila afadhali nilikosea.

Demu: afadhali ulikosea?
Mimi: ndio.
Demu; kwa nini?
Mimi: huoni naongea na mtoto mrembo Kama wewe.

Demu: mmmmh!
Mimi: yaani ni Kama bahati vile.
Demu: Bahati gani?
Mimi: kuongea na wewe.
Demu: wewe unamatatizo sio bure.

Mimi: matatizo kidogo.
Demu: kumbe umejiona eee!
Mimi: wahenga wanasema ukisikia sauti ya malaika lazima upagawe.

Demu: hahahaaaaa! Sasa wewe sauti ya malaika umeisikia wapi?
Mimi: nimeisikia leo tena ninaongea nayo.

Demu: unamaneno wewe.
Mimi: niotee jina lako.
Demu: huwezi kuotea.
Mimi: Na nikiotea...?
Demu: huwezi kuotea nasema.
Mimi: nambie utanipa nini?
Demu: Ntakupa zawadi.(kmya kidogo) ila usije kuwa unanijua alafu unanichora hapa.

Mimi: nikujulie wapi weeye.
Demu: haya otea.
Mimi: unaiii....twaaa...desh desh
Demu: hahaaaaa. Otea sasa.

Mimi: Unaitwa Neema.
Demu: huyooo umekosa.
Mimi: siwezi kukosa Mimi wewe.
Demu: Ndio umekosa sasa.
Mimi: haya nambie unaitwa nani?
Demu: muone mbwembwe zote umekosa.
Mimi: nambie sasa.
Demu: naitwa Grace.
Mimi: hahaaaa!! Huyoooo hata hajui maana ya Grace kwa kiswahili.

Demu: najua. Ila umejitahidi.
Mimi: zawadi yangu.
Demu: nitakupa.
Mimi: sawa.

Demu: Na wewe unaitwa nani?
Mimi: na wewe otea.
Demu: mi siwezi kuotea.
Mimi: basi usijali mtoto malaika, niite Michaelray.

Hiyo ngoma utaendelea kwa wiki zima mpaka mtoto anajaa mwenyewe.

Shida ya wanaume wengi wanaharaka na mbinu hii ambayo huhitaji muda.

Ninauzoefu nayo Sana hii. Kila mwanamke ananamna yake ya kuingiliwa.
hii ni noumaaa
 
Nikikwambia Namba nimepewa na Nani itakuwa msala maana aliyenipa pia kasema usinitaje .... Hee hapo utakula kiswahili hadi utasahau
 
Hahaaaa! alafu ndo ukute hata hilo neno CHUO ndo analisikia kwa mara ya kwanza.....Maweeee!

Alituma applications fulani chuoni then nikaona picha nikampenda.

Basi siku moha nikapiga nikamwambia nimekosea namba. Siku nyingine tena hivyohivyo. Basi ikawa mwanzo wa mawasiliano na mahusiano.

Swali likaja siku moja akakomaa, namba ulipata wapi? Hahah anakulaga kiswahili mpaka kesho na sina mpango wa kumwambia.
 
Wenye timamu hawashindwi kujibu hilo swali.

Ni rahisi sana, ili hali una taarifa zake vzr unamtajia jina la mtu yeyote tu. Hapo anapoa kabisa.

Kumbuka: wanawake wanapenda uongo ....they fall in love with lies
 
Ah mimi ndio maana huwa napenda kuwaibukia na kuwaomba wenyewe. Na bahati nzuri sujawahi kunyimwa namba na siku nikinyimwa nitaacha kabisa kuomba namba
Mimi nipo kama wewe kaka, huwa naomba namba kwa muhusika na Mara zote huwa napewa namba ingawaje Mara chache sana nanyimwa namba.
 
Nikiulizwa swali kama hilo huwa najibu kuwa "kwa kuwa moyo wangu unakupenda na kukuthamini daima moyo huu haukusita kukutafuta ili nipate kuexpress my feelings.... Na njia pekee na rahisi ilikuwa ni kupata namba yako ya simu kwa mawasiliano zaidi ila tambua kuwa dhamira yangu kwako ni njema kabisa ndio maana nikaipata namba yako, so plz nakuomba kwasasa tucjadili wapi nimeipata namba yako bali nakuomba tujadili ni kwa namna gani tutawasiliana kupitia namba hii,.. Je kuna masharti yoyote juu ya muda wa kuwasiliana na wewe? Ningependa tuanzie hapo" hapo sasa nakuwa nishamtoa katika mada yake ya kudai nilipoipata namba na sasa napambana nae juu ya muda wa kuwasiliana nae na porojo zingine..... Kidume kamili akiulizwa swali kama hilo kwake ni fursa maana kutongoza ni fani kama fani zingine kwani kuna wakubwa kibao hawajui kutongoza zaidi hutumia pesa tuuuu.
 
Kutokana na uzuri wako Binti,nimetafuta namba yako mpaka nimeipata!! Hapo ukiona hajakata simu ujue tayari huyo wa kuliwa Tu....waoga hawawezi hiyo.
 
Wanaume wamekuwa wakijifanya ni mabingwa kama siyo majabali wa kutongoza lakini mara baada tu ya ujio wa simu za mkononi hakika zimekuwa ni kama ni mateso makubwa kwao.

Nalisema hili kutokana na kwamba unaweza kumkuta mwanaume anapambana au anahangaika kuipata namba ya mwanamke fulani ambaye hajuani nae au labda namba yake kaipata tu kwa mtu ili aanze kumtongoza kwa simu ama kwa kumpigia au kumtumia meseji lakini imekuja kujulikana kuwa hakuna mtihani mgumu au swali gumu ambalo wanaume wengi hukumbana nalo na ambalo wengi wao hushindwa kulijibu na hatimaye kujikuta wanajichanganya na wanamkosa huyo mwanamke.

Utakuta mwanaume anaanza kujitutumua kwa kuwasiliana na huyo mwanamke lakini akiulizwa tu swali hili " je namba yangu umeitoa wapi au kakupa nani? " wengi wao hukata tamaa kabisa na hata kuishiwa tena nguvu za kuendelea kuwasiliana na yule binti au mwanamke kwani hakuna swali ambalo wanaume wengi hawalipendi na hawaliwezi kulijibu kama hilo.

Labda leo tupate uzoefu kutoka kwa wanaume ambao naamini humu mpo wengi ni kwanini wengi wenu pamoja na jeuri zenu zote mkiulizwa tu hilo swali tajwa hapo juu huwa mnajiumauma na hatimaye kusepa na kuishia kulalamika tu?

Na je unadhani majibu sahihi ya kumjibu mwanamke ambaye hujuani nae halafu umepata tu namba yake kwa mtu na unataka kumtongoza endapo atakuuliza hilo swali kuwa " namba yangu umeitoa wapi au namba yangu kakupa nani? " ni yapi au ni lipi?
Ukiwa mwongo unafanikiwa 100%
 
Back
Top Bottom