Namba tatu ilinikosesha mrembo daaahNingekuwa mimi ningejibu hivi.
3. Kuna rafikiyo ambaye ni msiri wangu ndiye aliyenipa namba yako kwa masharti kwamba nisilitaje jina lake kwako iwapo ungeniuliza. Kwa kuwa nimekula kiapo, siwezi kumsaliti.
Daaah we jamaaaZamani mimi nlikuwa nawaambia NIMEOKOTA SIMU ,SASA KATIKA KUPEKUA KWENYE NAMBA ILI NIMPATE ANGALAU MTU WA KARIBU WA HUYO ALIYEPOTEZA NDO NKAJIKUTA NAKUPATA WEWE KWASABABU NAMBA NYINGINE ZOTE HAZIPATIKANI NA NYINGINE HAZIPOKELEWI , HIVO NLITAKA KUJUA KAMA KUNA MTU WAKO WA KARIBU ALIYEPOTEZA SIMU HIVI KARIBUNI?.. (hapo lazima ataniuliza nimeiokota sehemu gani, mimi ntamtajia eneo lolote tu lenye mkusanyiko wa watu hata kwanye daladala, alafu
na atataka nimtajie hiyo namba aangalie kama anamfahamu huyo aliepoteza simu, nitakata simu kujifanya ndo naangalia alafu ntampigia kisha ntamwambia either namba imefungiwa so haiwezekani kuangalia usajili, au ntamtajia namba yoyte nliokuwa nayo ambayo haipatikani au imefungiwa, yaani nnaeza nkamtajia hata namba yangu ya zamani, BAADA YA HAPO HUO MTEGO NTAKUWA NSHAUEPUKA SO KINACHOENDELEA NI KULA KUKU KWA MRIJA,
zipo njia nyingi saana aisee ila nimeitoa hiyo moja kama mfano tu.
hii ni noumaaaHuwa wanawake wa hivyo Mimi siwatongozagi siku hio hio.
(Simu inaitwa na kupokelewa sauti ya kike upande wa pili inasikika).
Demu: Hello
Mimi: Hello mambo
Demu: poa.
Mimi: Nambie
Demu: Mmmmmh! (Kmya kidogo) kwani nani mwenzangu?
Mimi: ooh sorry. Nitakuwa nimekosea namba.
Demu: Ok.
Mimi: Poa. Bt sorry kwa usumbufu.
Demu: Usijali, kwani ulikuwa unampigia nani?
Mimi: Dada yangu.
Demu: Sawa, utakuwa umekosea namba.
Mimi: poa, ila nimeinjoi kuongea na wewe.
Demu: kwa nini?
Mimi: una sauti nzuri kweli.
Demu: Mmmmh! Ahsante.
Mimi: nadhani unafanana na sauti yako.
Demu: Badae Bhana coz sa hivi ninakazi.
Mimi: Daa samahani kwa kukupotezea muda jaman.
Demu: wala hujanipotezea muda. Badae jioni nipo free.
Mimi: Basi ntakutafuta hiyo jioni.
Demu: sawa ila angalia hiyo namba vizuri.
Mimi: Poa. Byyeee
Demu: oewky.(simu inakatika).
Jioni ikafika.
(Nachukua simu natuma text kwa yule demu).
Mimi: Mambo (inapita dakika tano text haijibiwi. Baadaye text inaingia kwa simu yangu).
Demu: poa nambie.
Mimi: niko fresh mrembo.
Demu: mmmh! Aliyekuambia Mimi mrembo ni nani na hujawahi kuniona?
Mimi: Nilikuambia Sauti yako inatosha kunijulisha kuwa wewe ni zaidi ya mrembo labda uniwie radhi kwa kukuita mrembo kwani wewe ni zaidi ya mrembo.
Demu: mmh! Makubwa(huku akicheka).
Mimi: Umenisamehe lakini?
Demu: nimekusamehe?
Mimi: ndio
Demu: kwani umenikosea nini?
Mimi: si nimekuita mrembo wakati wewe ni zaidi ya mrembo.
Demu: hahaahaaaaa!! Unamambo wewe. Sipati picha demu wako.
Mimi: unanisingizia tuu. Wala sina maneno zaidi ya kuongea ukweli.
Demu: (anacheka kidogo) tuachane na hayo. Ulimpata Dadaako.
Mimi: Ndio. Aah! Kumbe nilikosea namba ya mwisho.
Ila afadhali nilikosea.
Demu: afadhali ulikosea?
Mimi: ndio.
Demu; kwa nini?
Mimi: huoni naongea na mtoto mrembo Kama wewe.
Demu: mmmmh!
Mimi: yaani ni Kama bahati vile.
Demu: Bahati gani?
Mimi: kuongea na wewe.
Demu: wewe unamatatizo sio bure.
Mimi: matatizo kidogo.
Demu: kumbe umejiona eee!
Mimi: wahenga wanasema ukisikia sauti ya malaika lazima upagawe.
Demu: hahahaaaaa! Sasa wewe sauti ya malaika umeisikia wapi?
Mimi: nimeisikia leo tena ninaongea nayo.
Demu: unamaneno wewe.
Mimi: niotee jina lako.
Demu: huwezi kuotea.
Mimi: Na nikiotea...?
Demu: huwezi kuotea nasema.
Mimi: nambie utanipa nini?
Demu: Ntakupa zawadi.(kmya kidogo) ila usije kuwa unanijua alafu unanichora hapa.
Mimi: nikujulie wapi weeye.
Demu: haya otea.
Mimi: unaiii....twaaa...desh desh
Demu: hahaaaaa. Otea sasa.
Mimi: Unaitwa Neema.
Demu: huyooo umekosa.
Mimi: siwezi kukosa Mimi wewe.
Demu: Ndio umekosa sasa.
Mimi: haya nambie unaitwa nani?
Demu: muone mbwembwe zote umekosa.
Mimi: nambie sasa.
Demu: naitwa Grace.
Mimi: hahaaaa!! Huyoooo hata hajui maana ya Grace kwa kiswahili.
Demu: najua. Ila umejitahidi.
Mimi: zawadi yangu.
Demu: nitakupa.
Mimi: sawa.
Demu: Na wewe unaitwa nani?
Mimi: na wewe otea.
Demu: mi siwezi kuotea.
Mimi: basi usijali mtoto malaika, niite Michaelray.
Hiyo ngoma utaendelea kwa wiki zima mpaka mtoto anajaa mwenyewe.
Shida ya wanaume wengi wanaharaka na mbinu hii ambayo huhitaji muda.
Ninauzoefu nayo Sana hii. Kila mwanamke ananamna yake ya kuingiliwa.
Hayo maujanja ya zamani hahaDaaah we jamaaa
hahahaha, hakuna swali linalokera na kuudhi kama umenipendea nini, hili swali huwa linakera sana kwangu mimiHata ukifanikiwa kumjibu swali hilo kuna lingine atakuuliza una .. "shida gani? " hapo lazima jasho likutoke.
Alituma applications fulani chuoni then nikaona picha nikampenda.
Basi siku moha nikapiga nikamwambia nimekosea namba. Siku nyingine tena hivyohivyo. Basi ikawa mwanzo wa mawasiliano na mahusiano.
Swali likaja siku moja akakomaa, namba ulipata wapi? Hahah anakulaga kiswahili mpaka kesho na sina mpango wa kumwambia.
Jasho linatokaje sasa hapo?? Utakuwa na uchz wako mwenyeweHata ukifanikiwa kumjibu swali hilo kuna lingine atakuuliza una .. "shida gani? " hapo lazima jasho likutoke.
Mimi nipo kama wewe kaka, huwa naomba namba kwa muhusika na Mara zote huwa napewa namba ingawaje Mara chache sana nanyimwa namba.Ah mimi ndio maana huwa napenda kuwaibukia na kuwaomba wenyewe. Na bahati nzuri sujawahi kunyimwa namba na siku nikinyimwa nitaacha kabisa kuomba namba
Ukiwa mwongo unafanikiwa 100%Wanaume wamekuwa wakijifanya ni mabingwa kama siyo majabali wa kutongoza lakini mara baada tu ya ujio wa simu za mkononi hakika zimekuwa ni kama ni mateso makubwa kwao.
Nalisema hili kutokana na kwamba unaweza kumkuta mwanaume anapambana au anahangaika kuipata namba ya mwanamke fulani ambaye hajuani nae au labda namba yake kaipata tu kwa mtu ili aanze kumtongoza kwa simu ama kwa kumpigia au kumtumia meseji lakini imekuja kujulikana kuwa hakuna mtihani mgumu au swali gumu ambalo wanaume wengi hukumbana nalo na ambalo wengi wao hushindwa kulijibu na hatimaye kujikuta wanajichanganya na wanamkosa huyo mwanamke.
Utakuta mwanaume anaanza kujitutumua kwa kuwasiliana na huyo mwanamke lakini akiulizwa tu swali hili " je namba yangu umeitoa wapi au kakupa nani? " wengi wao hukata tamaa kabisa na hata kuishiwa tena nguvu za kuendelea kuwasiliana na yule binti au mwanamke kwani hakuna swali ambalo wanaume wengi hawalipendi na hawaliwezi kulijibu kama hilo.
Labda leo tupate uzoefu kutoka kwa wanaume ambao naamini humu mpo wengi ni kwanini wengi wenu pamoja na jeuri zenu zote mkiulizwa tu hilo swali tajwa hapo juu huwa mnajiumauma na hatimaye kusepa na kuishia kulalamika tu?
Na je unadhani majibu sahihi ya kumjibu mwanamke ambaye hujuani nae halafu umepata tu namba yake kwa mtu na unataka kumtongoza endapo atakuuliza hilo swali kuwa " namba yangu umeitoa wapi au namba yangu kakupa nani? " ni yapi au ni lipi?