Kwanini wanaume wa bara wanapenda vidosho wa Pwani?

Arabian queen

JF-Expert Member
Nov 23, 2016
2,557
4,824
Katika Kijiji cha Tombo, Kaunti ndogo ya Kakamega kaskazini, kuna mama mwenye upweke mwingi.

Bwanake alienda jijini Mombasa kutafuta riziki, hali ambayo imegeuka kuwa dhiki.
Bi Shikwekwe alibubujikwa na machozi alipokuwa akinihadithia jinsi bwanake alivyonaswa na kidosho wa Mombasa.

Baada ya kumsikiza kwa makini, niliamua kufanya utafiti kuhusu kwanini wanaume kutoka bara wanawapenda vidosho wa Pwani.

Ni nini ambacho wanawake wa Pwani hufanya ambacho wenzao hawajui?

Hili ndilo swali nilililowauliza wanaume ambao wamekaa Pwani kwa muda mrefu, bila kurudi nyumbani kuona familia zao.

Wanaume hao walisema kuwa mabinti wa Pwani ni warembo sana na pia wana heshima ya kupigiwa mfano.

Waliwamiminia sifa tele kama vile; kinga kwa kila ndwele, ghala la baraka, mabawabu wa penzi na chemichemi ya furaha.

Warembo wa Pwani ni vivuli juani na miavuli mvuani. Wao ni mwanga gizani, mavazi vulini na ngao vitani.

Wanafahamu fika mahitaji ya kujirembesha, na matamshi yao ni kama muziki sikioni na asali kwa ulimi wa mume.

Wanaume hao walisema kuwa wanawake wa Pwani ni amani rohoni, na pia ni kama chakula cha moyo.

“Sifa hizo ndizo sababu sitamani kurudi nyumbani. Siwezi ishi na mwanake ambaye haniheshimu, hajui kunipikia na hana madaha ndoani,” alisema mwanamume mmoja.

Aidha, walisema kuwa wanawake kutoka bara wanapaswa kuwaiga wenzao wa Pwani iwapo wanataka ndoa zao zidumu.
 
Mapenzi mubashara kuogeshewa kwenye beseni kama mtoto
upload_2017-2-17_14-49-31.png
 
Nani kakuambia Mtu wa kazi-kazini anapenda hao unaoita vidosho wa pwani?

Nani kakuambia mwanaume wa kazi kazini anapenda mwanamke ambaye ukimwacha asbh barazani unamkuta hapohapo akipakwa rangi?

Nani kakuambia Mwanaume wa kazikazini anahitaji mwanamke anayependa kwenda saloon kuliko bank?

Nani kakuambia Mwanaume wa kazikazini anapenda mwanamke anayehusudu vigodoro kuliko semina za ujasiriamali?

Umekutana na wasukuma halafu unageneralize?

Poor you.
 
Hamna lolote, mm nipo tanga mwaka wa tano na nimehamishia makazi huku hakuna lolote ni maneno tu.

Kikubwa wanawake wa tanga wanapenda sna mapenzi yaan unamkuta mmama saa11 jioni ameshapika, ameshaogesha watoto asuburi mumewe aje.

Akija watakaa ndani, wataangalia movie mala wacheze kalata siku ipite. Mume akinogewa anampa kamoja anaenda zake tembea kidogo akirudi mambo Mubashara chuzi shatashata.

Kinachowaponza wanawake wa bara hawana muda na waume zao, Tanga mume anapewa kipaumbele alafu Lugha sasa hawapeani maneno ya shombo na mumewe ni Mahaba tu.

Alafu cha mwisho wanajua kujistili, humkuti mwanamke alieolewa kavaa short pens anatembea barabaran hakuna mambo hayo. Wanajua kujistili na wanajua kujipodoa, sio kujipodoa kama wanawake wa dar full make-up sura nzito muda wote. Tanga mume anapakiwa wanja wa kungu na kapoda kwa mbaliii jicho tu linaongea....
Mpo hapo!!!!!
 
Back
Top Bottom